Ya Kikwete yanafurahisha

Ya Kikwete yanafurahisha

Mimi ninamkubuka sana Rais mstahafu Mh. Jakaya kwa mambo mazuri kumi (10) yafuatayo:

1. ustawi wa demokrasia
2. Barabara nyingi
3. Madaraja marefu yaliyoshindikana kule Kigamboni, Msata na Malagalasy
4. Jakaya Kikwete Hospitali ya Moyo
5. Mwendo kasi
6. Nyumba za wanajeshi
7. Gesi ya Mtwara
8. Upanuaji wa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere
9. Ndoto ya ujenzi wa flyovers Dar es Salaam.
10. Vikoba

Je, wewe unamkumbuka kwa mazuri yapi?
mimi namkumbuka kwa baya moja tu ambalo linayafuta hayo mazuri yote.

hili la ku force issue na kutuletea huyu!!
 
Sisapoti maandamano ila waandamanaji wana hoja za msingi muhmu gvt ingewajb hoja zao nawe ndo ujbiwe zako
Matukio ya utekaj na utesaj kushambulia kijana huyaon na hadi leo watu hawajulikan achana na yote rejea tukio la nape mtu ameonekana ila ameambiwa hajulikan

Huyo rais ndo anatoa ahad kw hao watumish na hatekelez ajibu hoja kwnza sio kuish kw saund
Pia mzunguko pesa ulipokuw mzr mie mwnyewe ni shuhuda nilipewa pkpk na mtumish nikawa napga bdabda katoro buseresele ila tatizo lako wew kama la mjomba anachukia walionacho huo ni umaskn wa fikra na hupelea mtu kuzeeka kbla y umr wake na akifa huenda jehanam ingaw tz ynyew kw sasa n kama jehanam tu.
 
Kwa Miaka Kumi Wananchi Hawana Maji Vijijini Huduma Za Afya Vijijini Za Hovyo Tu Miundombinu Sehemu Nyingi Alikuwa Mpigaji Kama Wapigaji Wengne Elimu Yenyewe Magumashi Wanafunzi Kaacha Wanakaa Chini Madarasa Hovyo Kwenye Uongozi Wake Nampa 40% Ndiyo Aliweza Mengine Yalimshinda Siku Yakitimizwa Haya 1 Maji Nchi Nzima Umeme Uhakika Afya Miundo Mbinu Elimu Kilimo N K
Naogopa wale watu wanaokaa Kimara, Mbezi, Kibamba, Ubungo na wengine wanaotumia usafiri wa mabasi yaendayo haraka kurahisisha maisha yao wakikusikia watakupuza na kukucheka sana.
 
Namkumbuka kwa kujenga shule za kata + UDOM
Shule za kata ni ubunifu wa hali ya juu sana, leo hii kila mtaa wa Tanzania kuna watoto wanaosoma sekondari tofauti na zamani ambayo kila kata kulikuwa na wastani wa watoto 2 tu wanaosoma sekondari.
 
Anzia AHM BWM JK wote ni wa hovyo tu hakuna hata aliyeonyesha dalili ya kuwajali wote walitumika kuwahujumu wananchi hasa wakulima waishio vijijini ambao ni wengi mnatuletea drama za madaraja na udom hapa wote hao ni mafisadi hata huyu aliyepo ni zao la hao hao kina jk so usitegemee jipya tatizo letu watu huwa tunawapima viongozi kwa vitu vya kipumbavu eti madaraja na udom wengine wanapambana kuboresha huduma za kijamii na ilikuwaje kwa miaka 57 wameshindwa kuondoa tatizo la maji elimu afaya miundombinu? watanzania tunaridhika kwa vitu vidogo sana nchi imezungukwa na mito maziwa mabwawa lakini wananchi hawana maji sekta ya kilimo imejaa hujuma tatizo la serikali inatoa huduma mbovu ili iendelee kutawala viongozi wote ni wa hovyo tu hakuna aliye na uchungu na taifa kila mmoja anaangalia tumbo lake tu
Wewe ndio umechanganyikiwa kabisaa huna nafuu. Hayo unayoyasema hayapo pahala popote kusini mwa jangwa la Afrika, haiwezekani kuwa viongozi woooote wa Afrika na vyama vyao tawala vyooooote Afrika ni wapumbavu.
Hata ukipewa wewe nchi uiongoze hautakuwa na tofauti sana na wenzio wa Afrika kwakuwa lazima utoe kwanza majibu ya mitaji, masoko, na malighafi ili uweze kuwahuhumia wananchi kama unavyotaka.

Lazima kuna common factor moja ambayo inatumiwa na watu au kundi fulani la watu kuifanya Afrika ya weusi ionekane kama ilivyo sasa. Kama CCM ya tanzania ndicho chanzo cha maendeleo duni basi tungetegemea hali ingekuwa nzuri Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, malawi, Congo, Msumbiji, Sudani, Afrika kusini, ethiopia, nk. Ndiyo maana hapa tunafananisha viongozi wa awamu sio vyama.
 
wizi ulishamili watu kukaaa kijiweni wakiwa Na uhakika wa pesa za ubwetee. moja kaitia nyumba yake sokoni iseee jpm walegezee hawa jamaa watakua wamejifunza bar hivi sasa wote tunakutana walewale hadi wahudumu wametukariri anajua hadi unacho kunywa hatarareeee mzunguko uko chini ila kwa ambao hatukua na magumashi mambo yame yumba kidogo tu. ushindani umekuavwa haki kutesa kwa zamu
 
wizi ulishamili watu kukaaa kijiweni wakiwa Na uhakika wa pesa za ubwetee. moja kaitia nyumba yake sokoni iseee jpm walegezee hawa jamaa watakua wamejifunza bar hivi sasa wote tunakutana walewale hadi wahudumu wametukariri anajua hadi unacho kunywa hatarareeee mzunguko uko chini ila kwa ambao hatukua na magumashi mambo yame yumba kidogo tu. ushindani umekuavwa haki kutesa kwa zamu
Kipindi cha kikwete kilikuwa cha wananchi kutafuta mitaji na kuwekeza kwenye maeneo ambayo yatatoa ajira kwa wananchi mijini na vijijini.
Watu wengi waliweza kulima, kufuga na kujenga kwa urahisi tofauti na sasa ambapo kupata mtaji ni jambo gumu sana. Taifa ni lazima liwe na mahali pakuanzia. Shule, hospitali, vyuo, viwanda, bank, petrol station, vyombo vya habari, mabwa ya samaki na mashamba vilijengwa na kuajiri watu wengi sana.

Migogoro ya ardhi ilizuka kwakuwa kila MTU alitaka kulima, kufuga na kujenga. Haya yalikuwa mapinduzi makubwa sana kwa Taifa hili, asitokee MTU kumdhihaki JK.
 
Tatizo la village elder ni kua anataka kila kitu awe nacho yeye na aabudiwe mfano logic ya kupunguza mishahara iwiane na wengine bado yoote ni kuona watu wengine wanaliowa 40,000,000 kwa mwezi roho inamuuma sana yani
Fact
 
mimi namkumbuka kwa baya moja tu ambalo linayafuta hayo mazuri yote.

hili la ku force issue na kutuletea huyu!!
Kweli Kabisa, Ila Leo Hata Yeye Anajuta Mno, Akitazama Uchumi Alivyopambana Kuukuza Leo Unaporomoshwa Kwa Kasi Ya 4G Na Bwana Faru, Roho Inamuuma Sana, Anaona Ni Bora Ata Angemaliza Tofauti Yake Na Blaza Edo Mamvi Akamwachia Nchi Hii Miaka Mitatu Tungekuwa Mbali Mno. Ila Ndugu Yenu Anafurahia Tu Kariakoo Kudoda, Mabenki Kufungwa, Biashara Kufungwa, Mahoteli Anayafunga Tu Huku Anachelea, Fedha Inashuka Thamani Anataka Aprint Mpya Yan Duh. Kagame Katuloga Sisi
 
Hivi Ile Mikakati Ya Kiuchumi Ya MKUKUTA, MKUZA, MKURABITA,SAGOT, KILIMO KWANZA Ambayo Awamu Ya Tatu Na Nne Waliibuni Ili Kukuza Uchumi Wa Nchi Mbona Hii Awamu Siisikii, Au Kuna Mikakati Mipya, Maana Wimbo Ninaousikia Ni KODI Tu
Twafaaa..
 
Nina uhakika wewe ni miongoni mwa waliombeza kuwa ni mpole, anachekacheka tu, anasafiri sana, ila sasa umegeuka baada ya kuona na upande mwingine
huwezi kuuona ubaya wa ukoloni kabla ya kuuona uzuri wa uhuru.
 
hata umkosoe vipi hajui kuchukia wala hakua mtu wa chuki na visasi,, alikua anafahamu wakosoaji na wanaomsifia wote ni ndugu wenye nia njema ingawa wanatumia njia/mbinu tofauti kujenga hoja zao
Nadhani alijua kuwa kuna maisha baada ya Urais kwisha. nadhani sasa hivi anaweza kwenda kusakata dance lake hata kule uwanja wa fisi bila ya kuhitaji msaada wa walinzi wake.
 
Mimi ninamkubuka sana Rais mstahafu Mh. Jakaya kwa mambo mazuri kumi (10) yafuatayo:

1. ustawi wa demokrasia
2. Barabara nyingi
3. Madaraja marefu yaliyoshindikana kule Kigamboni, Msata na Malagalasy
4. Jakaya Kikwete Hospitali ya Moyo
5. Mwendo kasi
6. Nyumba za wanajeshi
7. Gesi ya Mtwara
8. Upanuaji wa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere
9. Ndoto ya ujenzi wa flyovers Dar es Salaam.
10. Vikoba

Je, wewe unamkumbuka kwa mazuri yapi?
kwa kuleta meli ya dar bwagamoyo
 
Yaan Kikwete hata kama alikuwa na mapungufu ya ki ungozi jamaa alikuwa ana utu alijua siasa ni. Nn na hakuwa mchoyo kwa wana nchi wake.
He is way better than huyu wa sasa
 
Back
Top Bottom