Ya BASATA na Shilole

Ya BASATA na Shilole

Tukiachilia mbali matukio yake mengi yasiyo na staha katika majukwaa.. Ikiwemo fiesta na coco n.k.

Clip zake alizorekodi baada ya kufungiwa ni dhahiri hata adhabu aliyopewa haimtoshi. .. Huwezi kuzungumza kwa dharau na ujinga wa namna ile dhidi ya serikali.. Huu ni mfano ili na wengine wajifunze kupitia yeye..

Kila kazi ina miiko yake na ni muhimu kuzingatia
 
Shilole ameitwa jumla mara tatu kuhusiana na uvaaji wake na uchezaji wake usio na maadili na BASATA

Mara mbili amekua akionywa abadilike na kujihrshimu lakini akawa anachukulia poa tu
Sasa hii mara ya mwisho aliitwa akajitetee kwa yaliotokea ubelgiji na baada ya maelezo yake basata wakajiridhisha huyu shishi ndio zake na hana sababu za msingi wakampiga ban

Kiukweli adhabu ipi very harsh and unfair

Wajinga wajinga kama hawa unatwanga faini tu ya kutosha na atanyooka mwenyewe
I agree with u, heavy fine could be better rather than total ban for 1yr.
 
Tumesikia na kuona kupitia vyombo vya habari kile alichofanya msanii Shilole a.k.a Shishi baby kwenye onyesha alilofanya nchini Ubelgiji. Baada ya taarifa na picha za tukio Hilo kusambaa BASATA ilimuita Shilole kwa mahojiano zaidi. Binafsi Sijui alivyojenga hoja zake katika kujitetea lakini nalaani adhabu iliyotolewa kwa msanii huyu na BASATA.

Mosi kwa sababu adhabu hii imejaa unafiki mwingi ndani yake. Kwa wale wanaoishi miji mikubwa ndani ya nchi yetu watakubaliana nami kuwa hakuna cha ajabu alichofanya. Pili adhabu hii si adhabu bali ni aina fulani ya kukomoana. Najiuliza ni adhabu ya aina gani inayoenda kuua ustawi wa mtu na familia yake.

Mwaka 1bila ya kufanya Sanaa akale wapi binti wa watu. Tatu hii inadhihirisha ile hali ya watendaji wengi ktk taasisi za umma kutokufikiri kwa mantiki. Kwa masikitiko makubwa nakupa pole sana Shilole kwa adhabu hii ya kijinga.

Wito wangu waone wanasheria wakupe ushauri wa kisheria

Kweli asamehewe
 
Wangempiga faini tu,lkni kumfungia mwaka asifanye mziki ni kumkomoa kabisa ,sio haki,binafsi mimi napenda haki itendeke hapo hawaja mtendea haki,mziki ni kazi yake ataishi vipi?wanataka aanze kuuza K....wakati alisema kuuza K...basi.
 
Unapoambiwa usivae ovyo.. Wewe ukavaa ovyo.. Ukajifanya wewe ni mjuaji zaidi.. Wewe imara zaidi.. Utafungiwa tu, eeeh maana lazima tukubaliane BASATA itaongozwa kwa misingi ya sheria ( in Pinda's voice)

Maana hakuna namna nyingine
 
Watu kama nyie..
Hivi mwanao akifanya hivyo au dada yako aoneshe malapa mbele za watu tena watu sehemu tofaui wazione utajisikiaje
 
BASATA iliwalea lea sana hawa wasanii ndo maana wanachukuliaga poa, sasa inatakiwa isimamie maadili kikweli kweli kama inavyotakiwa kisheria
 
ScreenShot_20150811004403.png
 
Na wengine wajifunze, mziki unaimbika na kuchezeka hata ukiwa umevaa nguo sio lazima wakae uchi
 
Back
Top Bottom