Ngwananzengo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2012
- 1,911
- 1,320
Tumesikia na kuona kupitia vyombo vya habari kile alichofanya msanii Shilole a.k.a Shishi baby kwenye onyesha alilofanya nchini Ubelgiji. Baada ya taarifa na picha za tukio Hilo kusambaa BASATA ilimuita Shilole kwa mahojiano zaidi. Binafsi Sijui alivyojenga hoja zake katika kujitetea lakini nalaani adhabu iliyotolewa kwa msanii huyu na BASATA.
Mosi kwa sababu adhabu hii imejaa unafiki mwingi ndani yake. Kwa wale wanaoishi miji mikubwa ndani ya nchi yetu watakubaliana nami kuwa hakuna cha ajabu alichofanya. Pili adhabu hii si adhabu bali ni aina fulani ya kukomoana. Najiuliza ni adhabu ya aina gani inayoenda kuua ustawi wa mtu na familia yake.
Mwaka 1bila ya kufanya Sanaa akale wapi binti wa watu. Tatu hii inadhihirisha ile hali ya watendaji wengi ktk taasisi za umma kutokufikiri kwa mantiki. Kwa masikitiko makubwa nakupa pole sana Shilole kwa adhabu hii ya kijinga.
Wito wangu waone wanasheria wakupe ushauri wa kisheria
Mosi kwa sababu adhabu hii imejaa unafiki mwingi ndani yake. Kwa wale wanaoishi miji mikubwa ndani ya nchi yetu watakubaliana nami kuwa hakuna cha ajabu alichofanya. Pili adhabu hii si adhabu bali ni aina fulani ya kukomoana. Najiuliza ni adhabu ya aina gani inayoenda kuua ustawi wa mtu na familia yake.
Mwaka 1bila ya kufanya Sanaa akale wapi binti wa watu. Tatu hii inadhihirisha ile hali ya watendaji wengi ktk taasisi za umma kutokufikiri kwa mantiki. Kwa masikitiko makubwa nakupa pole sana Shilole kwa adhabu hii ya kijinga.
Wito wangu waone wanasheria wakupe ushauri wa kisheria