Fanya jambo kutokana na mapenzi yako, usifanye jambo kufata mkumbo.
Kama unamfulia au haumfulii liwe uamuzi binafsi.
Hakuna anayetumia mashine Wote mnatumia mikono; kwahio sio swala la mwanamke au mwanaume kama wote mnasaidia ndani ya nyumba.
Utamaduni wa zamani mama zetu walikaa nyumbani kufanya kazi za ndani ni swala linakubalika.
Sasa wote tunaenda kazini kwahio ni muhimu kama mtu hana mashine au mfanyakazi wa ndani mkajikusanya mkaosha nguo zenu huku mnataniana na kusimama mnaenda kupiga game mnarudi kumalizia na mnaendelea.
Kama swala la kupika. Gf/mkeo anapika sio lazima huwe mbali, nenda jikoni pale pale unampa maneno matamu, unammchezea wala hawezi kuona kupika adhabu.
Tatizo tunafata mkumbo. Kuna njia nyingi sana ya kuimarisha mapenzi.
Jibu kwa swali lako , fanya unachokiona wewe ni sawa.
unastail kusifiwa kwa ushauri mzuri ulotoa.... mtu hutakiwi kuishi maisha ya mwingine