Sir Carter
JF-Expert Member
- Sep 7, 2017
- 632
- 1,397
Hutakiwi hata kumjibu mtu kama huyo...Huu Uzi nimeukumbuka leo, nipo kwenye mahusiano na binti mmoja wa kigoma huko, (Muha) niliamini ni mtu mmoja understanding kama wengi wanavyowasifia...
Juzi niliahidi kumpa pesa ya kusuka, muda mfupi baadaye nikapigiwa simu mdogo wangu amepata ajali ya pikipiki, anapelekwa hospital, lakini bahati mbaya hakuwa na cash kwa hiyo akaomba nimpige kampani...
Nimemwambia bibie kuwa hatosuka leo asubiri kesho jioni, imekuwa kesi... "Bajeti yangu si ulishaitenga, sasa mdogo wako si ungempa ya dharura mimi nikasuke?, unaninyanyasa kwa sababu sina kazi, haujali mimi kupendeza ndiyo maana unaamua tu kufanya unavyojisikia"
Baada ya hayo majibu, nikakumbuka huu uzi, chap chap nimemwambia, "kama unadhani wewe una umuhimu kuliko mdogo wangu fikiria upya, I'M AN IDIOT TO THAT EXTENT, USINITAFUTE TENA!"
Saa hizi yupo busy kunitumia msg za kuomba msamaha!