Wodi Mpya ya wazazi Muhimbili tayari, Jionee Mwenyewe!

Kasi ya namna hii Tanzania haijawahi kuiona, kwa hivyo watu hawa amini wanachokiona, kilichobaki kwa sasa hivi ni watu waliokuwa wana uchuki na mfumo wa zamani kuendelea kuikosoa kila kukicha, na ni haki yao... ila kubadili tabia nchi unaanza na walio kabidhiwa nchi mpaka ngazi ya chini kabisa ambaye ni raia wa kawaida mitaani... hii kitu siyo kazi ya wiki au miezi michache tu! Kadri muda unavyo songa mbele, na mambo mengi yatanyooka tu..

Nina imani na ninacho kisema.. kwani siioni chama kinachotawala kwa sasa hivi, bali anaye kiendesha.. na nina imani pia kwamba anafanya kila anachoweza kwa moyo mmoja.. msione hana changamoto zilizojificha ambazo sisi waraia hatuwezi kuziona kirahisi hivyo..

Anajitahidi sana kuimulika kila sekta iwezekanavyo, na bado mengi tu yatamulikwa, kwa uwezo wa mwenyezi mungu. Kama mheshimiwa ana mapungufu yake kwa sasa hivi na zile ambazo anamulikiwa yeye za zamani, kuna binadamu aliyenyooka mia kwa mia? Mbona mheshimiwa wa Monduli tulitaka kumkubali? Sababu zilikuwa kumkubali kwa sifa zake tu, au kwa sifa tulizo aminishwa ambaye ingebadili mwelekeo wa chii hii?

Kama mheshimiwa wetu sasa hivi hatoweza kubadilisha mfumo wa chama tawala kwenye miaka mitano ijayo, itakuwa vigumu sana kumpata mwingine atakayeweza.. Na misingi ukisha sawazishwa, iije chama chochote tu kile, tabia nchi ndio utatawala! Kwani tabia naye ni mjeuri sana..

Sahihisho -> mwenyezi Mungu
 
safi lakini hupaswi kujisifia na kujipongeza kwa kutekeleza jukumu lako ambalo ulipaswa kulitekeleza miaka 40 iliyopita.
 
Baada ya watu kushinda kwenye viyoyozi siku nzima wakati wagonjwa wakilala chini kwenye jumba linalovuja maji ya choo, Raisi aliagiza wafanyakazi wahame ili wapishe wagonjwa na hilo lilifanyika mara moja kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini!

Angalia mwisho kabisa ya ukuta utaona flat screen TV hawa ndiyo waliokuwa wanalilia kuona Bunge live TBC wakati wa kazi huku wagonjwa wakiwa wamelala chini na hawa wafanyakazi watakuwa wanachadema Tu!

FSA_6540.jpg




FSA_6443.jpg




FSA_6416.jpg


Waziri wa Afya Bi.Umi Mwalimu akiratibu zoezi zima!
3.JPG


4.JPG


6.JPG


7.JPG


Wagonjwa wakiwa tayari juu ya vitanda vipya na wodi mpya, namna hii hata Mungu ni lazima atubariki kwa kujali watu wetu wenye udhaifu!
Hongera Raisi Magufuli hongera Waziri Mwalimu!



8.JPG



HAPA KAZI TU!
Kwa kweli Mungu ambariki Magufuli. HAPA KAZI TU katika ubora wake
 
Wrwe
Mshaanza maigizo eeeeh...!
Vitanda vya zile sherehe za bunge kuuzindiliwa mlipiga promo hivi hivi mkadai vingine wanalalia paka juzi mmeumbuka!
sasa mtasema na lile jengo ambalo halijakanilika ndani ya miaka 30 nalo lishakamilika na wamehamia...!
Mnaudhi sana!
Wewe huna jema.
 
Waziri wa afya hakuwa ameliona hilo kabla? kama hakuliona hadi raisi atoke ikulu aende hadi huko kwani kuna umuhimu gani wa kuwa na mawaziri mizingo
...........mawazili wa namna hii nao ni majipu
 
Kuna umuhimu Serikali ikatilia mkazo wa nguvu ile dhana ya uwajibikaji. Rais hawezi kuwepo mahala pote kwa wakati.
 
Je tujiulize jengo hilo lina miundombinu inayofaa kuwa wodi? nikimaanisha vyoo pamoja na bafu kwani jengo hilo lilijengwa mahususi kama ofisi na specificatons za idadi ya vyoo vinavyotakiwa kuwepo katika ofisi na wodi ni tofauti kabisa kuringana na idadi ya watu aina na mahitaji yao pia, maana tunaweza kukurupuka kusifu lakini mwisho wa siku tukazalisha tatizo lingine.
 
Wakuu hili jambo la kuwa na wodi mpya ya wazazi yenye vitanda vizuri hili kila mzazi alale katika kitanda chake nalo liliitaji maelekezo kutoka kwa rais Magu?

Kwani hakuna viongozi wenye dhamana?
 
Wewe nae utakua namatatizo huko kujenga kunachukua siku ngapi? Mbona akili huishughulishi? Hii ni kama dharula ndo maana mheshimiwa Rais alisema kama tatizo ni mkandarasi basi basi apigwe chini.
Ila kama tatizo ni fedha kwa ajili ya majengo ambayo toka enzi za mwinyi yana jengwa atatoa pesa yamaliziwe
So wewe ulitakaje Labda? Hao wamama waendelee kulala chini watanowatano? Huoni angalau imepunguza hao kina mama 120 wamepata mahala pa kulala.kuhusu ofisi kwa sababu hao si madaktari wala manesi watatafuta sehemu ikiwezekana hata wizarani wakaegeshe kwa muda.

Mawazo ya kimagumashi hayo. Hao wamama waliongezeka ashubuhi?? Huyo daktari aliye waandikia wakalazwe hapo ndiye wa kuwajibisha.
Dala dala tu ndiyo haijai vingine vyote vina jaa. Angewapa ref kwenda hospitali nyingine za kando na Muhumbili. Boresheni vituo vya afya, pawe na magari tayari hapo Muhumbili ya kuwapeleka huko wakajifungulie huko. Sii lazima Muhumbili compound. Kwani hapo ndipo roho hukaa??
Records zikipotea au kuharibika ni mangapi yameharibiwa?
 
Je tujiulize jengo hilo lina miundombinu inayofaa kuwa wodi? nikimaanisha vyoo pamoja na bafu kwani jengo hilo lilijengwa mahususi kama ofisi na specificatons za idadi ya vyoo vinavyotakiwa kuwepo katika ofisi na wodi ni tofauti kabisa kuringana na idadi ya watu aina na mahitaji yao pia, maana tunaweza kukurupuka kusifu lakini mwisho wa siku tukazalisha tatizo lingine.


Wewe mbona ulizaliwa bila ya uwepo wa Miundo Mbinu iliyofaa na umekuwa na mpaka leo hii uko hapa unaandika Pumba!
 
Namshauri Rais, hata huyu anaekaimu sasa Muhimb. hafai. kwani siku ile alikuwa anatoa mafanikio ya siku 100 za rais wakati wagonjwa wanalala chini. Ja Rais asingeenda kule watu tungefikir Muhimb imebadilika kumbe ovyo. Rais tafuta mwingine, ni lazima Muhimb ifike sehemu iwe ni sehemu ya kukimbilia kila mtu. Mbona regency siku hizi watu wa kawaida wanaenda na unapata huduma nzuri?
 
Wewe mbona ulizaliwa bila ya uwepo wa Miundo Mbinu iliyofaa na umekuwa na mpaka leo hii uko hapa unaandika Pumba!
Ndugu kila kitu kinaenda kitaalamu katika karne hii sio unaandika upumbavu kwa kuwa tu unashabikia yanayofanyika, jitahidi kutafakari kwa kina na kuushirikisha vizuri ubongo wako nafikiri unaweza kujikwamua kutoka hapo ulipo kwenda hatua nyingine inayofaa.
 
Back
Top Bottom