Wizi wa Mamilioni Longido,Wasomi kumburuza mahakamani Ded na mwenyekiti wa halmashauri

nyamadoke75

Member
Apr 1, 2020
87
280
Wadau wa Maendeleo na wasomi wilayani Longido wamejipanga kuishtaki mahakamani Halmashauri ya Longido kwa ubadhirifu wa fedha za umma baada ya kubaini kwamba Mkurugenzi wa Halmashauri ,Stephen Ulaya na Mwenyekiti wa halmashauri hiyo,Simon Oitesoi ndio chanzo cha uchochoro wa upotevu wa fedha za Umma.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari ,Mkurugenzi huyo anadaiwa kushinikiza baadhi ya miradi hewa kutengewa fedha zinazomnufaisha yeye na Mwenyekiti wa Halmashauri ikiwemo upotevu wa sh.Million 81 fedha ya ujenzi wa kituo cha afya Ketumbeine pamoja na sh.Million 17 mradi hewa zahanati ya Irikaswa.

Katika hatua nyingine halmashauri hiyo imekua ikiidhinisha fedha kuelekezwa kwenye miradi iliyoibuliwa na wananchi na baadaye kurudi nyuma na kuzitaka fedha hizo kinyume na taratibu ikiwemo kwenye miradi ya afya na Elimu.

Hivi karibuni halmashauri hiyo ilitenga kiasi cha sh million 35 kwa ajili ya kukamilisha zahanati ya Naadare iliyopo kata ya ilorienito tarafa ya Ketumbeine lakini baada ya fedha hizo kufika kwenye Account ya kijiji Mkurugenzi alitoa maelekezo ya kulipwa mzabuni hewa anayeishi mto wa mbu ambaye hata kamati ya ujenzi haimfahamu.

Wakili wa kujitegemea ,Samaito Laizer amesema tunahitaji kufahamu ukweli na Tunahitaji kuona watu Wakiwajibika Kwa matendo yao,ndio maana nimechukua siku nzima,kupitia sheria na kuufahamisha Umma haki zao Ili wawe na Msimamo na wasitishwe Kwa lolote.

Alisema wamejipanga kufungua Kesi Mahakama Kuu, High Court Arusha,tunajua baadhi ya maazimio yalopitishwa na Baraza la Madiwani yamekuwa paralyzed,hatazingatiwi Wala kutekelezwa,pamoja na ukiukwaji mkubwa wa Kanuni za makusanyo na Uthibiti wa Matumizi wa FEDHA.

.....

Pichani Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Longido, Steven Ulaya kushoto na mwenyekiti wa halmashauri hiyo,Simon Oitesoi.
images%20(5).jpg
IMG-20230224-WA0003.jpg
 
Hiyo halmashauri haina madiwani? Hakuna mkaguzi wa fedha , muhasibu ? Timu ya ufuatiliaji ya mkoa na TAMISEMI wote hao hawajawahi kufika hapo kufuatilia hiyo miradi? Wakaguzi wa nje CAG hawajawahi kufika na kuhoji matumizi ya fedha hizo za miradi.?

Huko kwenye halmashauri mmekaa kimajungu sana hii hakuna mtu mwenye akili timamu atakaekuelewa.
 
Namjua nje ndani mkurugenzi wa longido ndugu yangu ulaya, hana makandokando hayo alikuwa monduli akaenda longido nampaka sasa anadumu Kwa uadilifu kazini. Ulaya ni jembe ni jembe la kazi anajua kazi yake kusema ana kashfa ni uongo mtupu. Acha Roho ya uchuro wewe lofa
 
Hiyo halmashauri haina madiwani? Hakuna mkaguzi wa fedha , muhasibu ? Timu ya ufuatiliaji ya mkoa na TAMISEMI wote hao hawajawahi kufika hapo kufuatilia hiyo miradi? Wakaguzi wa nje CAG hawajawahi kufika na kuhoji matumizi ya fedha hizo za miradi.?

Huko kwenye halmashauri mmekaa kimajungu sana hii hakuna mtu mwenye akili timamu atakaekuelewa.
Hata vyombo vya uchunguzi kama TAKUKURU hawapo?

Hata hivyo kama ni kweli basi this could be a good move!!! Hatua kama hazichukuliwi basi umma uchukue hatua ikiwemo kwenda mahakamani
 
Namjua nje ndani mkurugenzi wa longido ndugu yangu ulaya, hana makandokando hayo alikuwa monduli akaenda longido nampaka sasa anadumu Kwa uadilifu kazini. Ulaya ni jembe ni jembe la kazi anajua kazi yake kusema ana kashfa ni uongo mtupu. Acha Roho ya uchuro wewe lofa
Akikununulia bia mbili tatu tu unadhani DED ni mwadilifu... usijidanganye bwashee, hawa DEDs ni wezi kweli kweli
 
Nimeona kuna Mbunge kabebwa na vijana Sita, kisa miradi imekamilika na hela zimetumika kihalali

Sasa ndio nimejua kwanini alibebwa ingawa wengine wanasema ooh kwani hela ni zake? Ni wajibu wa serikali na yeye kusimamia tu

Sasa bila kuzisimamia ndio wanatokea majambazi kama haya yasiyokuwa na huruma

Kuwe na kipengele wanapopewa kazi kuwa ukiiba hela za umma jela miaka 30 Saini hapa ...........
 
Hata vyombo vya uchunguzi kama TAKUKURU hawapo?

Hata hivyo kama ni kweli basi this could be a good move!!! Hatua kama hazichukuliwi basi umma uchukue hatua ikiwemo kwenda mahakamani
Usiamini huo uzushi kama unavosema inamaana hata TAKUKURU hiyo wilaya hakuna?
 
Back
Top Bottom