doup
JF-Expert Member
- Feb 26, 2009
- 2,346
- 2,151
Jana nimesimuliwa kisa cha ajabu sana kutoka kwa jirani yangu, ambaye ni mama wa makamo wa kunizaaa hivi. Mama alikwenda kwenda kuchukua pesa kwenye ATM kwa ajili ya manunuzi ya sikukuu (kwa wenyeji njia ya kwenda Kitunda au Gongo la mboto) ni pale banana - ukonga kwenye tawi la Akiba.
Basi anatoka tu kwenye ATM, kaja mama mwingine na kujifanya ametoka Tanga, anaulizia Ofisi za wizara nishat na madini, huku wanatembea kulekea kituo cha daladala jirani akamwabia office hizi anafahamu ziko mjini, kabla hajatoa maelezo ya kina kijana kwa nyuma yao akadakia, aaah office hizo ziko town unauliza huku? mi naelekea huko, ghafla gari saroon inapiga breki, anaelekea town buki(1000), jammaa anawambia kina mama mi nachukua hii niwahi, na yule mama mgeni wa tanga na yeye anasema ngoja na mimi ni pande hii. Jirani bila hisia zozote akajua hawa ni wasafiri wenzangu tumekutana hapa hapa na katika harakati za kutaka kuwai akaamua kupanda hiyo gari wakamuweka kati kiti chanyuma.
safari akiaanza, wanakaribia Tazara, jirani anawambia mi nashuka hapo, bahati mbaya ilikuwa mida ya kama saa tatu asubuhi hivi, hivyo akuna foreni, jamaa wakapita taa za tazara, jirani akaanza kuhoji imekuwaje? bila hiyana gari nzima wakabadirika mama toa kila kitu ulichonacho kwa usalama wako, kwanza leta hiyo simu!, kung'uta begi. Kufika kituo kinaitwa banda la ngozi wakamshusha hapa kapigwa na butwaa asijue la kufanya.
Anafika Polisi, anaambiwa mama hata usipoteze muda wako, tumeshapata matukio ya watu hao mengi, lakini hakuna mtu anayetuletea namba ya gari, hivyo hakuna cha kufanya. Jirani akabaki amechoka zaidi, Mungu si Athumani, begi lilikuwa na tundu kwa ndani katika kukagua anapata mia tano ilijificha huko siku nyingi anapanda daladala na kurudi nyumbani kwa uzuni kubwa.
Tujihadhali, cha kuchangaza kama Polisi wanataalifa na watu hawa, intelejensia yao imeshindwa kufanya kazi kuwanasa?? kweli polisi yetu kimeo kama hakuna maslahi hakuna msada kabisa.
Basi anatoka tu kwenye ATM, kaja mama mwingine na kujifanya ametoka Tanga, anaulizia Ofisi za wizara nishat na madini, huku wanatembea kulekea kituo cha daladala jirani akamwabia office hizi anafahamu ziko mjini, kabla hajatoa maelezo ya kina kijana kwa nyuma yao akadakia, aaah office hizo ziko town unauliza huku? mi naelekea huko, ghafla gari saroon inapiga breki, anaelekea town buki(1000), jammaa anawambia kina mama mi nachukua hii niwahi, na yule mama mgeni wa tanga na yeye anasema ngoja na mimi ni pande hii. Jirani bila hisia zozote akajua hawa ni wasafiri wenzangu tumekutana hapa hapa na katika harakati za kutaka kuwai akaamua kupanda hiyo gari wakamuweka kati kiti chanyuma.
safari akiaanza, wanakaribia Tazara, jirani anawambia mi nashuka hapo, bahati mbaya ilikuwa mida ya kama saa tatu asubuhi hivi, hivyo akuna foreni, jamaa wakapita taa za tazara, jirani akaanza kuhoji imekuwaje? bila hiyana gari nzima wakabadirika mama toa kila kitu ulichonacho kwa usalama wako, kwanza leta hiyo simu!, kung'uta begi. Kufika kituo kinaitwa banda la ngozi wakamshusha hapa kapigwa na butwaa asijue la kufanya.
Anafika Polisi, anaambiwa mama hata usipoteze muda wako, tumeshapata matukio ya watu hao mengi, lakini hakuna mtu anayetuletea namba ya gari, hivyo hakuna cha kufanya. Jirani akabaki amechoka zaidi, Mungu si Athumani, begi lilikuwa na tundu kwa ndani katika kukagua anapata mia tano ilijificha huko siku nyingi anapanda daladala na kurudi nyumbani kwa uzuni kubwa.
Tujihadhali, cha kuchangaza kama Polisi wanataalifa na watu hawa, intelejensia yao imeshindwa kufanya kazi kuwanasa?? kweli polisi yetu kimeo kama hakuna maslahi hakuna msada kabisa.