Wizi-vodafone m-pesa ubungo plaza

Manyanza

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
9,489
14,356
Habari zenu wana Jamii!
naandika habari hii kwa masikitiko, jana majira ya saa 5 asb nilienda kupata huduma ya M-Pesa pale Ubungo Plaza, nilikua naenda kutoa pesa katika account yangu. cha kushangaza yule dada aliyekua ananihudumia aliniambia nifanye process zote mpaka alipopata msg kwenye simu yake, baada ya hapo akachukua simu yangu akawa ana bonyeza bonyeza, akanipa pesa ambayo nilikuwa natoa ilikuwa ni shilingi elfu Hamsini (50,000), akaomba kitambulisho nikampa akafanya process zote akanirudishia kitambulisho pamoja na simu yangu.
niliondoka pale na kuelekea Mlimani City,sasa nikawa nataka kununua muda wa maongezi kwa M-Pesa, kila nikajaribu ikawa inaniletea ujumbe kuwa sina Pesa ya kutosha kununua Muda wa maongezi na nilikuwa nataka kununua sh 5,000, nilijaribu mara tatu bila mafanikio nilipoangalia salio la M-Pesa ikaniambia ni sh 1370, nilipigwa na butwaa kwa sababu wakati naenda kutoa M-PESA nilikua na sh 62,250, moja kwa moja nikajua yule dada atakua amechakachua hela yangu zaidi ya shiling 11,000. sikutaka kurudi kuuliza wala kupiga simu Voda com.
naandika hapa najua kuna watu wa Vodacom mtaona na kujua kuwa baadi ya wafanyakazi wenu sio waaminifu. na anaharibu sifa ya kampuni.
WANA JAMVI KAMA MNATAKA KUTHIBITISHA NENDENI MKAJARIBU KUTOA PESA ZENU PALE UBUNGO PLAZA MAANA TABIA YA MTU MWIZI HAIKOMI SIKU MOJA NA NYINYI MTAKUJA KUTOA USHUHUDA..
KUNA RAFIKI NIMEMWAMBIA AKAJARIBU KESHO NA ACC0UNT YAKE IWE NA PESA NYINGI KIDOGO ILI AWEKE MTEGO.
NAWASILISHA
 
Hakili mukichwa kila mtu sasa hivi analazimisha kuwa fisadi katika eneo lake la kazi.ila mkuu pia nina mashaka kidogo.1 alijuaje passwod yako? 2 kila baada ya kutuma/kutoa pesa kuna msg ambayo huwa inakuja ikikutaarifu ukamilishwaji wa uhamishaji wa pesa.je hukupokea msg? Haya unaweza kusema hiyo msg aliifuta je hukusikia mlio wa msg ambao natumai ungekupa hamu ya kutaka kujua nani kakutumia msg? Je kwann umepuuzia kufuatilia ili hali unajua kabisa wewe uliweka sahihi kuonyesha ulichukua kiasi gani.?nadhani ingekua vema kama ungepiga simu voda wao wangekwambia hizo pesa zimeenda kwa nani na ni saa ngapi ungepima muda na kuona kama kweli kwa muda huo ulikuwa hapo ubungo.
 
Oh Pole sana mkuu,mimi sikuwahi kukutana na tatizo hilo nadhani kuna haja ya kuwa makini zaidi.
 
Hakili mukichwa kila mtu sasa hivi analazimisha kuwa fisadi katika eneo lake la kazi.ila mkuu pia nina mashaka kidogo.1 alijuaje passwod yako? 2 kila baada ya kutuma/kutoa pesa kuna msg ambayo huwa inakuja ikikutaarifu ukamilishwaji wa uhamishaji wa pesa.je hukupokea msg? Haya unaweza kusema hiyo msg aliifuta je hukusikia mlio wa msg ambao natumai ungekupa hamu ya kutaka kujua nani kakutumia msg? Je kwann umepuuzia kufuatilia ili hali unajua kabisa wewe uliweka sahihi kuonyesha ulichukua kiasi gani.?nadhani ingekua vema kama ungepiga simu voda wao wangekwambia hizo pesa zimeenda kwa nani na ni saa ngapi ungepima muda na kuona kama kweli kwa muda huo ulikuwa hapo ubungo.

usemayo ni kweli mkuu!
lakini kama umenisoma vizuri, huyo dada aliniambia nifanye procedure zote mpaka ilipoingia sms kwenye simu yake, ndio akaomba simu yangu na kitambulisho, akawa anafanya mambo yake. na mimi sikuwa na shaka hata kidogo na kuhusu suala la kupata alert ya sms nadhani hilo ni tatizo la voda wenyewew karibu mwezi sasa kuna tatizo la kutopata alert yoyote, sijui kama ni mimi pekee yangu au vipi.
 
ASANTE KWA CHANGAMOTO HII....PENDA KUANGALIO SALIO LAKO MARA KWA MARA ...UTAGUNDUA WIZI MKUBWA WA KIMTANDAO.....!b
 
usemayo ni kweli mkuu!
lakini kama umenisoma vizuri, huyo dada aliniambia nifanye procedure zote mpaka ilipoingia sms kwenye simu yake, ndio akaomba simu yangu na kitambulisho, akawa anafanya mambo yake. na mimi sikuwa na shaka hata kidogo na kuhusu suala la kupata alert ya sms nadhani hilo ni tatizo la voda wenyewew karibu mwezi sasa kuna tatizo la kutopata alert yoyote, sijui kama ni mimi pekee yangu au vipi.

nadhani kutopata alert inaweza kuwa ni kosa lao.ila kuna mjumbe mmoja hapo juu kasema kuna wizi unaoweza tokana na mitambo.nadhani hapo napo ni muhimu.sio voda tu karibu kila kampuni sasa hivi wizi wanaufanya tena watu wanatajirika mno. (japo sina ushahidi)mfano wale ma programmer waki amua kucheza html code wakaiba tsh 100 ambayo mtu hutokuwa na uchungu kama ambavyo ulivyo fanya wewe pale ubungo. 100 kwa watu 1mil.sawa na 100ml ambazo wakiamua muda wowote wanazipata.
 
Kama huyo dada kafanya wizi basi kafanya kitu cha kijinga na ataumbuka. Kwanza ni dhahili alikuomba password/pin code yako ambayo baada ya yeye kufanya vijiprocess kwa niaba yako alitakiwa akupe simu uingize wewe mwenyewe password/pin code yako. uwezekano mkubwa alitumia muda huo kuhamisha hiyo tofauti ya 11,000 kwenda akaunti yake au ya jamaa yake na kukupa karatasi uweke sahihi ya shs 50,000 tu ili vitabu vyake viwe clean na wewe uonekane umehamisha shs 11,000 kwenda mahala pengine anapopajua yeye. Ukifuatilia ataumbuka tu ingawaje kuwa pinned moja kwa moja inaweza kuwa ngumu. lakini waswahili husema mkono uliozoea kukomba mboga hauishi kufanya hivyo - wengi watajitokeza kumlalamikia. USITOE PIN CODE YAKO HATA KWA MIZINGA.
 
Hivi kwanini wanataka kuangalia simu yako ili iweje? Maana kama mie sitapenda mtu apekue simu yangu na ndio hapo alipoiba labda aliangalia balance na kujitumia ujumbe tena au?
 
Hapa sijaelewa mkuu tembe mwenzie...
Kwamba uligawa hadi pasiwedi? Kama ulimpa pasiwedi nakuweka kwenye kundi la craps mkuu...
 
Hapa sijaelewa mkuu tembe mwenzie...
Kwamba uligawa hadi pasiwedi? Kama ulimpa pasiwedi nakuweka kwenye kundi la craps mkuu...

nadhani baada ya kumpa kitambulisho changu cha Mpiga Kura, ambacho kina tarehe na mwaka wa kuzaliwa, na namba ya siri ni ule mwaka wangu wa kuzaliwa, nafikiri akili yake ililenga palepale kwenye mwaka wa kuzaliwa ndio maana akaweza kuniibia.
 
nadhani baada ya kumpa kitambulisho changu cha Mpiga Kura, ambacho kina tarehe na mwaka wa kuzaliwa, na namba ya siri ni ule mwaka wangu wa kuzaliwa, nafikiri akili yake ililenga palepale kwenye mwaka wa kuzaliwa ndio maana akaweza kuniibia.
Kwenye Tigo pesa mwaka wa kuzaliwa hauwezi kuwa password.Na Vodafone nao wafanye hivyo kuepusha usumbufu kama huo.

 
Kuibiwa kwa style hii naweza sema ni uzembe wako mwenyewe na usipoangalia utaendelea kuibiwa kwa mtindo huo huo.
 
Nakubaliana na wewe pale Ubungo Plaza vodashop kuna matatizo. Mi nilienda ku2ma fedha, nijuavyo mimi huku mitaani ma agent wanakubali ku2ma hata kama mimi si mtumiaji wa Vodacom, ajabu pale nikalazimishwa kuwa ni lazima fedha iingie kwenye account yangu kwanza ndo niitume mimi, nikamwambia mhudumu basi subiri niweke hyo laini ya voda hewani maana natumia handset moja, nadhani akaona usumbufu kusubiri na kulikuwa na wateja wengi akaamua kuendelea na zoezi na nikatuma pesa ile kwa rafiki yangu.
 
Wafanyakazi wa Hizi Voda Shops ni lazima wawe wezi kwani wanalipwa mshahara mdogo sana kwa sababu wao wameajiriwa na MYGOLI erolink na wanalipwa pesa kidogo with less benefits. voda imeleta usanii wa ku outsource part of HR na hii inapunguza gharama lakini pia inapunguza efficiency. Wengi wao ukiwauliza wanalalamika. Jamani management acheni kujilipa mishahara mizuri na maruprupu minono chini kunaanguka. Ndio maana Vodacom inaongoza kwa kuibiwa na wafanyakazi wake.
 
Hii story ukiifuatilia sana utajichanganya, nijuavyo mimi mwaka wa kuzaliawa ni default password ambayo unatakiwa kuibadili mara tu unapoanza kutumia huduma ya M-Pesa, ingawaje kwa M-Pesa unaweza kuendelea kuitumia bila kuibadili (haishauriwi).

Sasa swala la kumpa mtu simu linakujaje kwenye kutoa pesa jamani, kumbuka we hii sio mara ya kwanza kutumia huduma hii.

Mi nafikiri ufafanuzi zaidi unahitajika isiwe ndio kuanza kuchafuana hapa, hii biashara inaongoza kwa kuharibiana.
 
Pole sana ndg,watumiaji wengi wa voda m-pesa hu2mia mwaka wao wa kuzaliwa kama pswd hivyo ni rahisi kuibiwa endapo m2 atafanikiwa kupata kitambulisho chako.Angalizo:ndg wa jf 2sipende kutumia pswd zenye mwaka wa kuzaliwa
 
Unawezaje kumtuhumu huyo dada kwa ushahidi wa hisia??

Mimi nadhani bado hujapoteza kitu kwa sababu kama ni yeye ndiyo alichukua itabidi akurudishie tu hana ujanja. Nenda Vodacom Customer Care uwaombe wakuchapishie akaunti yako kwa tarehe unazohisi kufanyiwa ufirauni halafu angalia uone hiyo elfu 11 ambayo huioni iko wapi. Sasa ukishajua inabidi uifuatilie pesa yako kwa sababu ushahidi tayari unao mkononi.
 
Ukienda kujisajiri M-PESA huwa wanachukua mwaka wako wa kuzaliwa kuwa ndio password yako. Mimi niliwahi kuiulizia huduma hii na nilipoliona hilo nilistuka kidogo. Kwa data security hii ni weakness kubwa.
 
Ukienda kujisajiri M-PESA huwa wanachukua mwaka wako wa kuzaliwa kuwa ndio password yako. Mimi niliwahi kuiulizia huduma hii na nilipoliona hilo nilistuka kidogo. Kwa data security hii ni weakness kubwa.

Sio lazima mbona mimi ninayo ambayo si ya mwaka wa kuzaliwa
 
Back
Top Bottom