Wizi Tengeru jijini Arusha

Wizi Tengeru jijini Arusha

Tengeru? Aaaah ni hatari nakumbuka kipindi flani Nilikua nakusanya ushuru wa soko wakaniibia risiti
Tengeru sina hamu nako risiti zilikua za laki mbili
 
Mwaka juzi mmoja alikwapua simu yangu apo tengeru ila nilikua faster nikaiwahi na Mimi nikakwapua .alivyonadharau akaondoka uku anacheka.cha kushangaza watu waliopo karibu wanamuangalia tu hakuna anayechukua hatua yeyote.nilijuta kwa nini mkono wake sikuushika.angeimba aleluya
 
Wadau wa JF habari za jioni. Nimetoka Masama Moshi kwenye mazishi ya Mama EvaGrace Emmanuel Lazaro Mwasha mke wa Askofu mstaafu wa kanisa la TAG. lakini ajabu tulivyofika TENGERU basi zima tumetangaziwa kuwa makini na wezi wa simu na vitu vingine kwa abiria. Hii imenitokea mara nyingi sana nikisikia Tahadhari hii. Nyie watu wa TENGERU badilikeni kwa kweli. Mkuu wa wilaya ya Arumeru Alexander Mnyeti na mbunge Joshua Nassary je hamuwezi kufanya kitu kuondoa Sifa hii mbaya kwa eneo hili, jiji la Arusha na Tanzania kwa ujumla? Maana hata watalii wengi "wamelizwa" Mali zao hapa.
Nawasilisha!
Kazi ya police ni ulinzi wa raia na mali zao, siyo kazi ya mbunge.
 
Mwaka juzi mmoja alikwapua simu yangu apo tengeru ila nilikua faster nikaiwahi na Mimi nikakwapua .alivyonadharau akaondoka uku anacheka.cha kushangaza watu waliopo karibu wanamuangalia tu hakuna anayechukua hatua yeyote.nilijuta kwa nini mkono wake sikuushika.angeimba aleluya
Haaaa nilitaka nije bora nifute safari tuuu kama ndo ivyo
Ukiwakata mikono si watakuwa wanatembea na mavi watachambaje? Watafutie adhabu nyingine
 
Wanaume wa mkoani mnatia aibu

Yani watu 30+ mnamuogopa mwizi mmoja
Mkuu embu angalia wanaume wa dar
6592e1f91817b6b5aa3c4ae94a4fb22e.jpg
 
Hahahaaa.....Hawa wanaume wa Sing'isi wakiingia shamba la anaeitwa mwekezaji ni dakika sifuri unaona vifusi na visiki

Nimekaa Tengeru kiasi fulani na ni jamaa fulani wakora kuliko maelezo....wazee wa mapanga na visu
Wameru wana LAANA. Usithubutu kuanzisha mahusiano nao.
 
Hapo kazi ni ndogo Peleka Malalamiko kwa Mshili huyu ni Kiongozi wa kabila la Wameru,Huko wana Adhabubya fimbo 70 kwa yeyote anayekiuka taratibu na maadili ya kabila hilo atashughulikiwa bila huruma.
 
Wameru wana LAANA. Usithubutu kuanzisha mahusiano nao.
Umeenda mbali sana mkuu, mimi sio mmeru lkn historia ya wameru wa sing'isi naijua sana, hicho kitongoji chao sio pure Meru bali ni Hybrid ya makabila mengi hadi kaburu.
Si kweli kuwa wameru wote hawafai japo wana udhaifu sawa na makabila mengine
 
Mkuu umepita njia tu umeshaanza kuhukumu! Je ungeshuka na hiyo simu yako ingekuwaje..?!

Kiuhalisia hayo matukio yalikuwepo kwa wingi hapo nyuma ila kwa sasa ni nadra sana kuyasikia.
 
Back
Top Bottom