Wizi Tengeru jijini Arusha

dafity

JF-Expert Member
Aug 16, 2008
1,849
2,036
Wadau wa JF habari za jioni. Nimetoka Masama Moshi kwenye mazishi ya Mama EvaGrace Emmanuel Lazaro Mwasha mke wa Askofu mstaafu wa kanisa la TAG. lakini ajabu tulivyofika TENGERU basi zima tumetangaziwa kuwa makini na wezi wa simu na vitu vingine kwa abiria. Hii imenitokea mara nyingi sana nikisikia Tahadhari hii. Nyie watu wa TENGERU badilikeni kwa kweli. Mkuu wa wilaya ya Arumeru Alexander Mnyeti na mbunge Joshua Nassary je hamuwezi kufanya kitu kuondoa Sifa hii mbaya kwa eneo hili, jiji la Arusha na Tanzania kwa ujumla? Maana hata watalii wengi "wamelizwa" Mali zao hapa.
Nawasilisha!
 
Hao machalii wa hapo noma sana, zamani kabla ya ile kambi ya jeshi kuwekwa pale watu walikuwa usiku hawawezi kushuka kule chini
 
Wadau wa JF habari za jioni. Nimetoka Masama Moshi kwenye mazishi ya Mama EvaGrace Emmanuel Lazaro Mwasha mke wa Askofu mstaafu wa kanisa la TAG. lakini ajabu tulivyofika TENGERU basi zima tumetangaziwa kuwa makini na wezi wa simu na vitu vingine kwa abiria. Hii imenitokea mara nyingi sana nikisikia Tahadhari hii. Nyie watu wa TENGERU badilikeni kwa kweli. Mkuu wa wilaya ya Arumeru Alexander Mnyeti na mbunge Joshua Nassary je hamuwezi kufanya kitu kuondoa Sifa hii mbaya kwa eneo hili, jini la Arusha na Tanzania kwa ujumla? Maana hata watalii wengi "wamelizwa" Mali zao hapa.
Nawasilisha!
Mkuu Tengeru inaitwa soko la simu hasa siku ya j5 na jmosi...siku ya soko, wamelizwa watu wengi, kuna wezi wa simu profesheno waiba hada gari iko kwenye mwendo, ukiweka sikioni imeenda.
Jkt walisaidia sana walikuwa na mradi wa ujenzi pale Chuo cha ualimu Patandi kilichoko Tengeru stand waliwadhibiti sana.
Kwasasa kuna nafuu flani, kuna vijana wa mtaa flani unaitwa SING'ISI yaani hawafai weka mbali na jamii, polisi haingii pale kizembe ni zaidi ya hatari. Ukipata ajali na eneo la Sing'isi haijalishi ni saa ngapi mchana wew mwite Yesu mnazareth.
 
Back
Top Bottom