Wizi mpya wa VodaCom, Tuwakatae!

Wizi mpya wa VodaCom, Tuwakatae!

Crimea

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2014
Posts
26,801
Reaction score
38,842
Wadau, vodacom imekuja na wizi mpya baada ya kuona ule wa mb 8 umenyamaziwa, ambapo sasa hakuna vocha ya 500 bali 450. Aina hii ya wizi ni kwamba ukienda dukani hiyo vocha utainunua kwa sh.500 huku wewe ukipata sh.450 kwenye salio lako.

Ikumbukwe kwamba hao vodacom hawana kifurushi cha chini ya 499, sasa mtu kama unanunua vocha ya sh.500 alafu unapata sh.450, maana yake utakuwa unalazimika kununua vocha mbili za 1000 ili upate 900, au ya elfu moja ili uweze kujiunga!

Jaman hii nchi tunaelekea wapi? Kwa maisha gani ya mtanzania kuweka elfu moja kila siku kwa ajili ya vocha?

Hawa jamaa ni kuachana nao kabisa, leo hii R.I.P lain ya voda, sina hamu na ninyi tena!
 
miongoni mwana mtandao nilioshindwa kutumia .... karibu halotel au smart
 
Kwa kweli voda kuna matatizo bas tu cc watz hatujui kudai haki zetu na tcra ndo hawajARI HATA KDG
 
V6dacom! kazi ni kwako, hii ndio Slogan yao hawa jamaa, ila ktk Slogan hii kuna kitu wanamaanisha,, Tafakari chukua hatua.
 
..ila hili suala gumu;bado halijaniingia kwa brain, yaani nitoe 500/- kununua vocha halafu mimi wanipe 450/-
this is an absolute joke; but if it's true....
 
Pia Vodacom wameondoa huduma ya kuongea na muudumu wao bure Sasahivi ni shilingi 100 kuongea nao. Ndio Tanzania imefikishwa na Mfumo m'bovu hapo. Kila Mtu anajiamulia atakavyo.
 
Back
Top Bottom