Wizi kwenye mabenki nbc na zingine kwa kutumia master card

Mkuu hebu niambie ni Benki gani nzuri katika hao washirika wa Umoja Switch? Hizi zingine naona sasa zinatishia uasalama wa pesa zetu

Ukiongelea huduma za ATM ukijiunga na benki yeyote ambayo ni member wetu utakua salama, ukijua hatua za kufata hakuna hata shilingi moja inaweza kupotea (labda uibiwe ATM card, na mara nyingi na mtu anayekufahamu na anajua PIN yako), tunaanza elimu kwa umma katikati ya mwezi ili wateja wetu wajue wapi pa kwenda inapotokea wamepata shida.

Ila unapokuja kwenye products nyingine hizi benki zinatofautiana sana, na zote zinashindana, mfano zipo zinatoa islamic banking zingine hazitoi, zipo zinatoa akaunti maalum za savings zingine hazitoi, rate za interest pia inatofautiana kutokana benki moja hadi ingine, sasa kushauri uende benki gani itategemea wewe unataka huduma gani.

 
Wandugu wanajamvi. Siku za karibuni kumekuwepo wizi wa kutisha kwenye mabenki kutumia mitandao. Lakini inaonekana benki zetu hawajachukua tahadhari ya kutosha na bado haijulikani liability inakuwa ya nani endapo wizi unatokea.Mwezi Mei 2012 rafiki yangu aligundua ameibiwa kiasi cha mil2 kupitia kwenye Master card. Yeye aliripoti haraka sana, akapeleka vielelezo vyote kule makao makuu ya NBC. Iligundulika kuwa maeneo walikochoka hela ni kule Mlimani city pamoja na kwenye ATM za exim.Hata hivyo waliahidi kumpa majibu sahihi baada ya siku 45! (just imagine kama ndo ilikuwa akiba yako unasubiri muda wote huu). Juzi kati benki wamempigia simu na kumwambia inaelekea hela alizichukua mwenyewe (hawakutoa cctv evidence ju-justify conclusion yao). Sasa ndugu anahaha na mwezi huu ni mwezi wa kuwarudisha watoto shule, lazima kulipia ada. Mbaya zaidi rafiki yangu amechanganyikiwa in terms of what next. Je sheria za kifedha zinamlinda vipi mtenja wa benki endapo tukio kama hili likitokea? Pili huyo rafiki anafikiria kuwachukulia hatua za kisheria....je kuna mtu anaweza kutoa mwongozo (sio wa spika bali wa kisheria) ni jinsi gani rafiki yangu anaweza kupata haki yake?

Kwa maoni yangu:
Inaelekea benki zetu nyingi zimeshindwa kuthibiti wizi huu, lakini kuna uwezekano kabisa wafanyakazi wa benki ama wale wanaohusika na ATM wakawa sio waaminifu wanachukua namba za siri na kuwaliza wateja. This is not acceptaable and should be dealt by all means



Pole sana kwa rafiki yako, ila usikubali. Kuna wakati lilinitokea hilo na wakataka kunipotezea, hawakutaka hata nionane na bank manager. Nikawaambia nikitoka hapa naenda kwa waandishi wa habari, waliitafuta wenyewe hiyo hela wakairudisha. Mshauri aikubali mpaka wampe hela yake.
 
Mkuu asante. Nadhani suala la kutumia media linaweza kuwa zuri, kwa kuwa image yao itagundulika kirahisi. Kwa sasa nadhani wanawadharau wateja wao
 
Mkuu asante. Nadhani suala la kutumia media linaweza kuwa zuri, kwa kuwa image yao itagundulika kirahisi. Kwa sasa nadhani wanawadharau wateja wao

kutumia media ku-expose maujinga kama haya ni move nzuri sana!
 
kuna matatizo kwenye bank zetu na sisi wateja kama mnakumbuka kuna kipindi wabulgaria walikamatwa wakifanya wizi kwenye ATM walifikishwa mahakamani wakapewa dhamana na baadae wakatoroka sikusikia vyombo vya habari vikifatilia ,polisi walikuwa kimya na wale waliohusika na kuwapa dhamana walichukuliwa hatua gani?
nije kwa wateja wengi wanapopata matatizo wanakimbilia bank kumbuka huo uliofanyika ni wizi na wizi huo mara nyingi unahusisha wafanyakazi wa bank kwa hiyo unaporipoti bank wanachofanya ni kuharibu vielelezo ndio maana wanakwambia njoo baada ya si iku 45 ili baadae iwe rahisi kukukatisha tamaa.Nawashauri mnapopata tatizo hilo mbali na kutoa taarifa bank inabidi muwasiliane na bank kuu,mripoti polisi na pia waifungulie kesi bank husika kwani unapoweka pesa bank bank hiyo inapaswa kuhakikisha usalama wa pesa zako.
namshauri huyo mtu afungue kesi mahakamani pia awaombe wale wote waliopata tatizo kama lake wajitokeze ili waungane na kufungua mashitaka.
hakuna bank inayotaka kupoteza heshima yake kwa jamii ila jambo hili likiwekwa hadharani litawafanya watendaji wakuu wa bank washituke na kuchukua hatua kwani mara nyingi hayo mambo yanazimwa kabla hayajafika ngazi husika kwa hiyo tusiishie kulalamika bila kuchua hatua kwani hili tatizo limekuwa likijirudia bila kuchua hatua inabidi tulikomeshe kuna sheria za bank kuu,kuna sheria za polisi na kuna sheria za nchi tuzitumie
 
jamani naanza kuingiwa nawoga kuhusu hizi bank, hii taarifa ni mnzuri lakini jibu muafaka halijapatikana
 
Samahani nilikwenda mashambani tangu nimetuma thread jana. Lakni ndo nimerudi sasa. Nilitaka kusema kuwa mhusika ameprint hivyo vyote, yeye amekuwa makini kwa kuwa kila mara anapodraw hela kwenye ATM anachukua na kutunza slip zile. Sasa alipokwenda NBC aliawapatia nakala za zile slip ambazo zilifuatiwa na wizi, akaambatanisha na barua ya malalamiko. Jambo la kushangaza ni kwamba NBC walipompigia simu kumweleza kuwa hawatampa, alikwenda ofisini kwao tena, Mshituko ukawa kuwa kwenye barua yake ya malalamiko hakuna zile attachments...haijulikani ni nani amezichukua!

Otherwise unalosema ni kweli ni vema kuweka hela nyumbani vijisenti vyako kuliko kuhangaika na vibenki uchwala. Changamoto ni watoto wa kova, wakizinusa nyumbani kwako umekwenda na maji. Pia hela zinashawishi, sometimes you end up spending on unnecessary things. Otherwise kwa mfumo wetu wa Tz hakuna mtu ambaye angependa kuweka (achilia mbali kukopa fedha benki). Kimsingi mifumo ya kibenki kwa Tz inabakia kiama kwa wtz wengi. Kama mfano tu, rafiki yangu alikopa kiasi cha Tz mil 24, gharama za loan processing wakamkata Tzs .9mil. Huo mkopo analipa tz 745,000 kwa mwezi muda wa miaka minne (4). Zidisha 48monthsx745,000 unapata 35.8mil. Kwa maana nyingine kwkt miaka 4 mtu analipa almost Mil 12 kwa mkopo wa mil 24! Sasa ukija kwenye reality, unaona kuwa kwa mfumko wa bei tulio nao pengine benki za mikopo zipo sahihi....maana items (hasa za ujenzi) za kiasi cha mil 24 gharama yake kwa sasa ni zaidi ya 40milion! QuOTE=Kwetunikwetu;4278226]Nafikiri anaweza kuomba bank statement then aangalie hizo fedha zilitokaje......then afungue kesi ya madai dhidi ya benki. My experience kuna jamaa yangu aliwahi kulizwa 4,000 USD toka Barclays Uganda, alikomaa nao mpaka wakamrudishia. Sometimes hivi vijisenti ni bora kuvifungia ndani tu badala ya kuhangaika na mabenki uchwara
[/QUOTE]

Mkuu Print out Bank Statement inakua na mtiririko wote wa Transactions coz hakuna m2 anaweza kutoa Pesa nje ya System.

Hata kama zile attachment zimepotea basi atapata taarifa yake ya fedha kwa kuprint Bank Statement anaanza upya kusotea pesa yake

Milioni mbili is not a JOKE
 
Huu wizi upo jamani. Nimeshuhudia rafiki yangu alikuwa masomoni nje. Akawa amenunua credit skype. Basi baada ya muda kazaa wakakomba hela zake benk ya NBC. Akafikiri ni frauding ya kwenye mtandao ikabidi aulize benk. Alipofuatilia akakuta kwanza iliingizwa sh laki 8 kwenye akaunti yake halafu siku ya pili ikatoweka na hela yake pia akaambia ametumia hela kwenye suermaket huko nje wakati hajatumia. Alipewa bank statement akauliza hii laki 8 imeingizwa na nani? Maana kwenye statement haineshi nani kaingiza. Alianzia UDSM branch wakamzingua kwa majibu yasiyoeleweka. Akaenda makao makuu na corprate branch pale wakamwambia hapa pana tatizo, yule dada pale akataka kumsaidia lakini alipoenda kwa boss wake akachomoa. Jamaa akaambia aende samora branch ambako kuna kitengo cha mawasiliano. Pale samora alivyokuwa anaelezea akatokea mama mmoja mfanyakazi akawa anambinya yule dada kaunta. Tukaona hapa kuna mchezo ambao umefanyika. Yule dada wa kaunta akataka kutusaidia kwasababu aligundua kuna kitu pale, lakini yule mama akaja tena akamwambia yule dada hii kesi ngumu kidogo rafiki yangu aandike barua ili apewe majibu. Tukagundua kuwa huu mchezo ni wa wale wa samora mawasiliano, udsm branch na makao makuu. Kwahyo huu ni mchezo wa wafanyakazi wa benki

Jamani na mie nimeibiwa kwenye M-pesa kwa mtindo huu huu wakuingiziwa kwanza fedha laki moja then kesho yake nikakuta hazipo pamoja na balance yangu ya Tsh 100,000/=, nimewapigia Customer care wala sipati majibu mazuri toka kwao sasa naomba ushauri wa JF nifanye nini kupata haki yangu?
 
Back
Top Bottom