BUBE
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 846
- 253
Wandugu wanajamvi. Siku za karibuni kumekuwepo wizi wa kutisha kwenye mabenki kutumia mitandao. Lakini inaonekana benki zetu hawajachukua tahadhari ya kutosha na bado haijulikani liability inakuwa ya nani endapo wizi unatokea.Mwezi Mei 2012 rafiki yangu aligundua ameibiwa kiasi cha mil2 kupitia kwenye Master card. Yeye aliripoti haraka sana, akapeleka vielelezo vyote kule makao makuu ya NBC. Iligundulika kuwa maeneo walikochoka hela ni kule Mlimani city pamoja na kwenye ATM za exim.Hata hivyo waliahidi kumpa majibu sahihi baada ya siku 45! (just imagine kama ndo ilikuwa akiba yako unasubiri muda wote huu). Juzi kati benki wamempigia simu na kumwambia inaelekea hela alizichukua mwenyewe (hawakutoa cctv evidence ju-justify conclusion yao). Sasa ndugu anahaha na mwezi huu ni mwezi wa kuwarudisha watoto shule, lazima kulipia ada. Mbaya zaidi rafiki yangu amechanganyikiwa in terms of what next. Je sheria za kifedha zinamlinda vipi mtenja wa benki endapo tukio kama hili likitokea? Pili huyo rafiki anafikiria kuwachukulia hatua za kisheria....je kuna mtu anaweza kutoa mwongozo (sio wa spika bali wa kisheria) ni jinsi gani rafiki yangu anaweza kupata haki yake?
Kwa maoni yangu:
Inaelekea benki zetu nyingi zimeshindwa kuthibiti wizi huu, lakini kuna uwezekano kabisa wafanyakazi wa benki ama wale wanaohusika na ATM wakawa sio waaminifu wanachukua namba za siri na kuwaliza wateja. This is not acceptaable and should be dealt by all means
Kwa maoni yangu:
Inaelekea benki zetu nyingi zimeshindwa kuthibiti wizi huu, lakini kuna uwezekano kabisa wafanyakazi wa benki ama wale wanaohusika na ATM wakawa sio waaminifu wanachukua namba za siri na kuwaliza wateja. This is not acceptaable and should be dealt by all means