Wizara zipi si za kimuungano?

Wizara zipi si za kimuungano?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,137
Reaction score
48,364
Kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania zipo wizara za mambo ya muungano na zipo ambazo si za kimuungano.

Kwa mujibu wa makubaliano ya Tanganyika na Zanzibar ya mwaka 1964, kutakuwa na mambo ya muungano na yasiyo ya Muungano.

Jee kuna maelezo mahali ya kisheria kuonesha ni wizara zipi ni za kimuungano na zipi si za kimuungano?

Je, zile zisizo za kimuungano watu wa upande mwingine wa muungano wana haki ya kuajiriwa?
 
Hizi hapa mwanangu wa Kambo yaliyobakia yote si ya Muungano Zingatia Expressio unius est exclusio alterius
IMG_1577.jpeg

IMG_1578.jpeg
 
Wizara zisizo za kimuungano zinazohusu mambo ya Tanganyika, jee wazanzibari hawaajiriwi?
Wizara gan ya tanzania ambqyo inawatoa wazanzibar?. Hiv unajua kama unazungumzia familia na mtoto wa kambo. Zanzibar ni kama mtoto wa kambo katika familia. Vya familia apate sabab ya mzazi wake lakin vya kwake ni vya kwake. Ndio mana zanzibar ina usalama wa zanzibar tu, ambao sio wq muungano wakat huohuo wa muungano zanzibar wapo
 
Wizara gan ya tanzania ambqyo inawatoa wazanzibar?. Hiv unajua kama unazungumzia familia na mtoto wa kambo. Zanzibar ni kama mtoto wa kambo katika familia. Vya familia apate sabab ya mzazi wake lakin vya kwake ni vya kwake. Ndio mana zanzibar ina usalama wa zanzibar tu, ambao sio wq muungano wakat huohuo wa muungano zanzibar wapo
Umetoa mfano sahihi Sana!
 
Kwenye Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania zipo wizara za mambo ya muungano na zipo ambazo si za kimuungano.

Kwa mujibu wa makubaliano ya Tanganyika na Zanzibar ya mwaka 1964, kutakuwa na mambo ya muungano na yasiyo ya Muungano.

Jee kuna maelezo mahali ya kisheria kuonesha ni wizara zipi ni za kimuungano na zipi si za kimuungano?

Je, zile zisizo za kimuungano watu wa upande mwingine wa muungano wana haki ya kuajiriwa?
Tanzania ni nchi moja ya JMT yenye uraia mmoja wa Tanzania, raia wote wa Tanzania wakiwemo Wazanzibari, wana haki zote sawa kwa mambo yote ya JMT, hivyo wana haki kuajiriwa popote.

P
 
Back
Top Bottom