Upekuzi101
Senior Member
- Aug 28, 2020
- 134
- 348
Habari wana JF,
Kumekuwa na tatizo kubwa Sana hasa kwenye wizara ya Mali Asili na utalii. Wizara ya Mali Asili na utalii inaonekana kama kila mtu yupo huru kuamua kuamka tu na kuweka tozo, gharama na malipo ambayo inaonekana hakuna wa kuhoji uhalali wake au umuhimu wake.
Kuachilia mbali kuwa mtalii anapokuja Tanzania analipa kodi kupitia visa yake na gharama nyingine ukijumuisha, malazi, usafiri, Chakula pamoja gharama za safari kwa wale wnaotembelea mbuga zetu, kote huku Serikali inapata mapato yake bila kipangamizi.
Pamoja na yote haya sasa hivi unapopita wilaya ya Siha na mgeni kwa maana ya mtali ukiwa na gari yoyote lazima ulipe tena.
Wamejianishia tozo zao wameweka hapo wanasubiri kutoza watu. Naomba wizara ya Mali Asili na utalii angalieni hili na kulikemea pia kwa sababu huu utaratibu utakuja kuwa ndio utamaduni wa watu kuamua kulipisha tu makodi yasiokuwa rafiki kwa biashara bila Serikali kujua na wakati mwingine hata hayo mapato kutofika Serikali.
Hili lilijitokeza halina mantiki wizara ya Mali Asili na utalii toeni tamko kuhusu hili maana halina mwisho mzuri wala halimfaidishi yoyote zaidi ya kuumiza biashara ya Utalii maana inaonekana ndiyo sekta kila mtu anaweza Kuja kuchuma tu pesa burebure kwa kutumia vifungu vya sheria ambavyo havina maslahi yoyote kwa Mtanzania.
Kumekuwa na tatizo kubwa Sana hasa kwenye wizara ya Mali Asili na utalii. Wizara ya Mali Asili na utalii inaonekana kama kila mtu yupo huru kuamua kuamka tu na kuweka tozo, gharama na malipo ambayo inaonekana hakuna wa kuhoji uhalali wake au umuhimu wake.
Kuachilia mbali kuwa mtalii anapokuja Tanzania analipa kodi kupitia visa yake na gharama nyingine ukijumuisha, malazi, usafiri, Chakula pamoja gharama za safari kwa wale wnaotembelea mbuga zetu, kote huku Serikali inapata mapato yake bila kipangamizi.
Pamoja na yote haya sasa hivi unapopita wilaya ya Siha na mgeni kwa maana ya mtali ukiwa na gari yoyote lazima ulipe tena.
Wamejianishia tozo zao wameweka hapo wanasubiri kutoza watu. Naomba wizara ya Mali Asili na utalii angalieni hili na kulikemea pia kwa sababu huu utaratibu utakuja kuwa ndio utamaduni wa watu kuamua kulipisha tu makodi yasiokuwa rafiki kwa biashara bila Serikali kujua na wakati mwingine hata hayo mapato kutofika Serikali.
Hili lilijitokeza halina mantiki wizara ya Mali Asili na utalii toeni tamko kuhusu hili maana halina mwisho mzuri wala halimfaidishi yoyote zaidi ya kuumiza biashara ya Utalii maana inaonekana ndiyo sekta kila mtu anaweza Kuja kuchuma tu pesa burebure kwa kutumia vifungu vya sheria ambavyo havina maslahi yoyote kwa Mtanzania.