Wizara ya Kilimo: Wadudu waliozua taharuki sio nzige. Ni panzi wanaofanana na nzige na hawana madhara

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Serikali imechukua tahadhari ili kuhakikisha nzige wa jangwani ambao ni tishio kwa mazao ya chakula na nyasi hawaingii nchini na kuleta madhara kwa wakulima na wafugaji, ikizingatiwa kuwa Tanzania inapakana na nchi zilizoathiriwa na wadudu hao.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya aliliambia HabariLEO kuwa, kutokana na hofu iliyokumba baadhi ya wakulima katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Kilimanjaro kutokana na kuibuka makundi makubwa ya wadudu waliodhaniwa kuwa ni nzige.

Alisema baada ya wizara yake kupata taarifa hizo ilipeleka wataalamu wake katika mikoa iliyoripoti wadudu hao hususani katika wilaya za Korogwe mkoani Tanga, Mwanga mkoani Kilimanjaro na Ilala jiji la Dar es Salaam.

Hata hivyo Kusaya alisema uchunguzi wa wizara ulibaini kuwa wadudu hao si nzige kama wananchi walivyodhani, bali ni panzi wanaofanana na nzige wasio na madhara katika sekta ya kilimo.

Alisema wadudu hao mara nyingi hujitokeza kila mvua zinaponyesha na imekuwa kawaida katika mikoa ya Tanga na Kilimanjaro kujitokeza kwa makundi katika vipindi vya mvua za vuli pamoja na za masika.

“Mpaka sasa serikali haina taarifa yoyote ya uwepo wa nzige wa jangwani nchini, hao walioonekana katika mikoa hiyo ni panzi wa kawaida ambao si tishio kwa mazao ya kilimo,”alisema.

Kwa mujibu wa katibu mkuu huyo, baada ya taharuki ya wananchi kutokana na uwepo wa wadudu hao na baada ya kujiridhisha kuwa hawana tatizo, wizara iliamua kutuma maofisa wengine kwa ajili ya kuwadhibiti ili kuondoa hofu kwa wananchi.

Hata hivyo, Uongozi wa Mtaa wa Buguruni Kisiwani jijini Dar es Salaam kulikokutwa makundi makubwa ya panzi, ulifikia maamuzi ya kuteketeza mazalia ya panzi hao ili kuondoa hatari inayoweza kulikabili eneo hilo katika siku za baadaye.

Viongozi wa mtaa huo walitumia moto kuteketeza mazalia ya wadudu hao ili kuweka mazingira salama ya wakulima wa mbogamboga katika eneo hilo linalozalisha mbogamboga kwa wingi katika jiji la Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Buguruni Kisiwani, Uwesu Uwesu, aliwatoa hofu wananchi na wakulima wa eneo hilo akisema wadudu hao watadhibitiwa ili kuondoa hofu iliyotanda kwa wananchi kuhusu hatari inayoletwa na uwepo wa wadudu hao.

“Hapa walikuja wataalamu wa Wizara ya Kilimo wakatuthibitishia kuwa wadudu hawa si nzige wa jangwani, bali ni panzi wanaofanana na nzige ambao hawana madhara kwa mazao ya wakulima,” alisema Uwesu.

Aliongeza kuwa, baada ya wataalamu kutoka wizarani kuwaelimisha kuhusu wadudu hao, waliwaita watu wa kupulizia sumu hali iliyowafanya wadudu hao kufa, ingawa baadaye lakini baadaye wakagundua kuwa wadudu hao walilikuwa wametaga mayai mengi.

Mkulima katika Wilaya ya Mwanga, Msami Mkwizu alithibitisha kuwepo kwa wadudu hao katika kata za Kifaru, Kileo, Usangi na Ugweno huku akisema kwa wakulima wazoefu wanawajua wadudu hao lakini kwa wakulima wapya walipata hofu na kiwewe wakidhani ni Nzige walioko Kenya.

Tanzania ni miongoni mwa nchi tatu kati ya nchi sita za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambazo hazijaguswa na nzige wa jangwani tangu mwaka jana mpaka sasa. Nchi nyingine ni Rwanda na Burundi ambazo nazo hazijaripoti uwepo wa nzige wa jangwani katika maeneo yao.

Nzige wa jangwani walianzia katika nchi za Ethiopia, Sudan Kusini na Somalia na kuenea katika nchi ningine kama Eritrea, Kenya, Uganda na nchi za Mashariki ya Kati kama vile Saudi Arabia, Yemen, Pakistan na India.
 
Hawana madhara wakati niliwashuhudia kwenye TV wakitafuna majani? Mambo mengine yanachekesha sana. Kumbe kuna panzi wakubwa vile kweli kila siku najifunza.

Au ninasema uongo ndugu zangu?
 
Hawana madhara wakati niliwashuhudia kwenye TV wakitafuna majani? Mambo mengine yanachekesha sana. Kumbe kuna panzi wakubwa vile kweli kila siku najifunza.

Au ninasema uongo ndugu zangu?
Kibwakizo chako cha Mwisho wananchi wanaitikia KWELIIII
Sasa mimi huwa sielewi huwa wanakubali kuwa anasema uongo au huwa wanaitikia wakimaanisha nini.​
 
Hawana madhara wakati niliwashuhudia kwenye TV wakitafuna majani? Mambo mengine yanachekesha sana. Kumbe kuna panzi wakubwa vile kweli kila siku najifunza.

Au ninasema uongo ndugu zangu?
Ni kweli ndugu, wapo shambani kwangu wanakula sana majani ya mihogo. Nimepulizia dawa baada ya muda ikiisha nguvu wanarudi wengi zaidi kushambulia shambani kwangu.
 
Ni kweli ndugu, wapo shambani kwangu wanakula sana majani ya mihogo. Nimepulizia dawa baada ya muda ikiisha nguvu wanarudi wengi zaidi kushambulia shambani kwangu.
Hao wadudu mimi niliwaona kwenye TV wakati wa habari wanatafuna majani kama vile mtu anakula mkate. Sasa nashangaa hawa kusema hawana hatari. Sijui wana maana gani? Ni afadhali waseme ukweli watu wachukue hatua stahiki.

Au ninasema uongo ndugu zangu? Kupanga ni kuchagua!
 
Taifa letu litakumbwa sana na mitihani katika hii miaka, kutokana na utawala kuwa wadhalimu.

Mungu hapendezwi na udhalimu wa viongozi kwa raia wanyonge.
Hapa kwetu, corona ilikuja halafu ikatoweka ghafla ndani ya muda usiozidi miezi mitatu, ila sehemu zingine bado ipo mpaka leo na ndiyo inazidi kushamiri. Nzige nao walikuja wakaishia nchi jirani, huku kwetu hawakugusa kabisa. Haya ndiyo majanga, si ndiyo? Halafu hao wenzetu ambao bado kwenye hali tete mpaka muda huu, wao unawashauri wasemeje? Ungekuwa raia wa nchi mojawapo ya hizo ungesemaje?
 
Wataalam wetu tatizo Sasa wanasema hao panzi hawana madhara Yale majani yanayoliwa sio madhara? sijui vichwani mwao kuna vitu gani.
 
Wataalam wetu tatizo Sasa wanasema hao panzi hawana madhara Yale majani yanayoliwa sio madhara? sijui vichwani mwao kuna vitu gani.
... ingekuwa maajabu hao panzi wasile kwani kiumbe hai chochote lazima kile; so, aina ya chakula, jinsi kinavyokula, na rate ya kula ndivyo vinavyokifanya kiwe kiumbe fulani; kiwe jinsi kilivyo.
 
Taifa letu litakumbwa sana na mitihani katika hii miaka, kutokana na utawala kuwa wadhalimu.

Mungu hapendezwi na udhalimu wa viongozi kwa raia wanyonge.
Hivi ninyi manaosema udhalimu. Udhalimu gani huo hebu tuambieni basi na sisi tuuelewe japo robo tu. Kila siku mnakuja na unfounded claims mara demokrasia imeminywa, mara wizi wa kura mara kile.

Hivi kabla ya Magufuli kuingia madarakani wewe ulikuwa na uhuru gani ambao sasa hivi hauna, najua wengi walikuwa wapiga madili tu na wezi wa mali za umma na kuuza madawa wamefungiwa mianya wanalalamika udhalimu bila wao kujua udhalimu waliokuwa wanausababisha kwa wananchi kukosa haki zao za msingi.

Ulikuwa unafanya kazi gani ambayo sasa hivi hauwezi kuifanya na ni kwanini hauwezi kuifanya na utawala huu umekudhulumu kitu gani?

Vyama vya siasa, nani kawakataza kufanya mikutano ya ndani? Mmembiwa mikutano ya hadhara ni kwa walioshinda, wabunge, madiwani na rais, wafanye maeneo yao kutekeleza waliyoahidi, muda wa kupinga ulishaisha kwenye kampeni na uchaguzi sasa ni kutekeleza yale waliyochagua wananchi. Sasa mnataka wenzenu waliochaguliwa wanatekeleza ninyi mnapiga kelele za kupinga. Haliwezekani hilo. Fanyeni mikutano ya ndani kuimarisha taasisi zenu kwa ajili ya 2025
 
Serikali imechukua tahadhari ili kuhakikisha nzige wa jangwani ambao ni tishio kwa mazao ya chakula na nyasi hawaingii nchini na kuleta madhara kwa wakulima na wafugaji, ikizingatiwa kuwa Tanzania inapakana na nchi zilizoathiriwa na wadudu hao.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya aliliambia HabariLEO kuwa, kutokana na hofu iliyokumba baadhi ya wakulima katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Kilimanjaro kutokana na kuibuka makundi makubwa ya wadudu waliodhaniwa kuwa ni nzige.

Alisema baada ya wizara yake kupata taarifa hizo ilipeleka wataalamu wake katika mikoa iliyoripoti wadudu hao hususani katika wilaya za Korogwe mkoani Tanga, Mwanga mkoani Kilimanjaro na Ilala jiji la Dar es Salaam.

Hata hivyo Kusaya alisema uchunguzi wa wizara ulibaini kuwa wadudu hao si nzige kama wananchi walivyodhani, bali ni panzi wanaofanana na nzige wasio na madhara katika sekta ya kilimo.

Alisema wadudu hao mara nyingi hujitokeza kila mvua zinaponyesha na imekuwa kawaida katika mikoa ya Tanga na Kilimanjaro kujitokeza kwa makundi katika vipindi vya mvua za vuli pamoja na za masika.

“Mpaka sasa serikali haina taarifa yoyote ya uwepo wa nzige wa jangwani nchini, hao walioonekana katika mikoa hiyo ni panzi wa kawaida ambao si tishio kwa mazao ya kilimo,”alisema.

Kwa mujibu wa katibu mkuu huyo, baada ya taharuki ya wananchi kutokana na uwepo wa wadudu hao na baada ya kujiridhisha kuwa hawana tatizo, wizara iliamua kutuma maofisa wengine kwa ajili ya kuwadhibiti ili kuondoa hofu kwa wananchi.

Hata hivyo, Uongozi wa Mtaa wa Buguruni Kisiwani jijini Dar es Salaam kulikokutwa makundi makubwa ya panzi, ulifikia maamuzi ya kuteketeza mazalia ya panzi hao ili kuondoa hatari inayoweza kulikabili eneo hilo katika siku za baadaye.

Viongozi wa mtaa huo walitumia moto kuteketeza mazalia ya wadudu hao ili kuweka mazingira salama ya wakulima wa mbogamboga katika eneo hilo linalozalisha mbogamboga kwa wingi katika jiji la Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Buguruni Kisiwani, Uwesu Uwesu, aliwatoa hofu wananchi na wakulima wa eneo hilo akisema wadudu hao watadhibitiwa ili kuondoa hofu iliyotanda kwa wananchi kuhusu hatari inayoletwa na uwepo wa wadudu hao.

“Hapa walikuja wataalamu wa Wizara ya Kilimo wakatuthibitishia kuwa wadudu hawa si nzige wa jangwani, bali ni panzi wanaofanana na nzige ambao hawana madhara kwa mazao ya wakulima,” alisema Uwesu.

Aliongeza kuwa, baada ya wataalamu kutoka wizarani kuwaelimisha kuhusu wadudu hao, waliwaita watu wa kupulizia sumu hali iliyowafanya wadudu hao kufa, ingawa baadaye lakini baadaye wakagundua kuwa wadudu hao walilikuwa wametaga mayai mengi.

Mkulima katika Wilaya ya Mwanga, Msami Mkwizu alithibitisha kuwepo kwa wadudu hao katika kata za Kifaru, Kileo, Usangi na Ugweno huku akisema kwa wakulima wazoefu wanawajua wadudu hao lakini kwa wakulima wapya walipata hofu na kiwewe wakidhani ni Nzige walioko Kenya.

Tanzania ni miongoni mwa nchi tatu kati ya nchi sita za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ambazo hazijaguswa na nzige wa jangwani tangu mwaka jana mpaka sasa. Nchi nyingine ni Rwanda na Burundi ambazo nazo hazijaripoti uwepo wa nzige wa jangwani katika maeneo yao.

Nzige wa jangwani walianzia katika nchi za Ethiopia, Sudan Kusini na Somalia na kuenea katika nchi ningine kama Eritrea, Kenya, Uganda na nchi za Mashariki ya Kati kama vile Saudi Arabia, Yemen, Pakistan na India.
Naomba Wahaya wote including Maxence Melo kuhamia kwenye hii mikoa kula hawa wadudu (panzi). Hatuhitaji dawa za kupulizia na kuua hawa wadudu wakati tuna Wahaya, Waangaza, Wasubi, na wala wadudu kibao hapa nchini.
 
Back
Top Bottom