Wizara ya Elimu na TAMISEMI hamlioni hili? Chukueni hatuaI

kabwekasoma

JF-Expert Member
Jul 24, 2016
260
153
Kwa heshima na taadhima naomba kushauri suala la elimu kwa nia njema maana yake inaenda kuwa chakavu na mbaya kutokana na upungufu mkubwa wa rasilimali watu (waalimu) katika shule nyiingi ukianzia shule ya Msingi mpaka Sekondari.

Hali ni mbaya mashuleni kuanzia shule ya msingi kwani kuna baaadhi ya shule za msingi zina wanafunzi 800 lakini walimu waliopo hawazidi 9.Tunajua kuwa serikali inatumia pesa nyingi katika kugharamia elimu bure ili watoto wetu wapate elimu na mwitikio wa wazazi umekuwa mkubwa kwa wazazi kuwapeleka watoto mashuleni hivyo kufanya idadi ya wanafunzi kuwa kubwa.

Elimu yetu inachangamoto kubwa sana lakini kwa hili la waalimu Serikali ilitupie macho kwani kwa shule za msingi ni balaaa kubwa na ikumbukwe msingi mzuri wa elimu unajengwa kuanzia chini labda kama Serikali itakuwa imeamua kuwakusanya vijana pamoja mashuleni iliwapige soga na kisha kurudi nyumbani.

Ukija upande wa Sekondari huko ndo balaa zaidi kwani shule unaweza ukakuta haina mwalimu wa hesabu wala fizikia shuleni nzima Serikali imejitahidi kuajiri waalimu lakini mara nyingi inakuwa walimu 2000 ambapo kiwastanii kwa shule zilizopo Tanzania hata mwalimu mmoja mmoja hatoshi. Ubora wa elimu haupimwi kwa matokeo unapimwa kwa skills and competence ya mwanafunzi alionao kichwani.

Nashauri serikali iajiri walimu kwa shule za msingi Tanzania angalau walimu wa3 kila shule ya msingi na upande walimu wasayansi kwa shule za sekondari angalau wa5 kwa kila Shule Sekondari, TAMISEMI na Wizara ya Elimu najua ujumbe wangu utawafikia
 
Serikali inastaajabisha sana shule hazina walimu walimu wapo mitaani afu ule mpango wa jk wakusomesha walimu udom ungerudishwa ndani ya miaka kumi tatizo la uhaba wa walimu lingekwisha kabisa
 
Hii serikali ya Magu ni one man show, kwa kweli hali ya shule za sekondari ni mbaya mno hasa upande wa masomo ya sayansi, angalia waziri mkuu aliongea mwezi wa 11 kuwa wanaatarajia kuajiri walimu elfu 16 cha ajabu mpk leo kimya kimetawala, kumbe pm nae aliropoka tu bila kujua anachokiongea. Watanzania tunatumiwa kisiasa na hapa target nzima ni uchaguzi ujao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe sema unataka ajira,maana shule zetu zina vifaa na walimu wa kutosha. Tafuta kazi nyingine ujiajiri aisee
 
Wamechukua walimu wa sekondari wamempeleka msingi sijui Nani aliwatuma,halafu mnamsifia jafo,mwalimu alikua anafundisha mfano geography na literature msingi anaenda fundisha English tu.yena anapewa 5 mpaka la Saba wakati wenzie wanafundisha masomo zaidi ya 4,Sasa hii so hasara hii,na huko walikotoka 2018 nako Sasa Kuna shida ya walimu,masikini headmaster hawezi kumuandikia afisa elimu kwamba Nina shida ya walimu,si ataambiwa si uliwatoa tukawapeleka msingi,kwani hukujua kwamba utawahitaji?
Niishie hapa,mifano tunaiona huku mawilayani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe sema unataka ajira,maana shule zetu zina vifaa na walimu wa kutosha. Tafuta kazi nyingine ujiajiri aisee
niko inservice muda mrefu nahisi hata kabla ujazaliwa mimi nimeongea jwa uchungu kwani tunapoelekea msitakabari wa elimu yetu itabaki stori
 
Na kinachofurahisha hadi ushuri huu na hats kuyaona mazingira yalivuo ya elimu, ni jinsi shule hizo hizo zinavyofanya vizuri katika mitihani ya NEMC
 
Ni kweli Hali ni mbaya Sana, watoto ni wengi idadi ya walimu ni ndogo Sana alafu Kuna issue ya madawati , shule nyingi asa za msingi hazina madawati watoto wanakaa chini na maafisa elimu wanalijua Ila kwa sababu wanalinda vyeo vyao hawezi kuliongelea kwa ngazi ya Taifa.
 
Back
Top Bottom