dudus
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 24,856
- 56,841
Wadau;
Kuna tabia moja ni kama umeshazoeleka hususan kwenye mabaa. Kanuni za afya zinawataka wenye mabaa na migahawa kuwa na sink au chombo cha maji safi na sabuni kwa ajili ya wateja kunawa kabla na baada ya kula au baada ya kwenda haja.
Kutokana na utaratibu huo, mabaa mengi huweka ndoo za maji "safi" somewhere kwa ajili ya wateja kujinawia na kwa kawaida ndoo hizi zenye mfuniko huwa na koki so mteja anafungulia na kujinawia zake. Pamoja na ndoo, baa nyingi huwa na vyombo vingine kama mabirika, majagi, mabakuli, na vyombo (chupa za plastiki zilizotobolewa mifuniko) vya sabuni za maji kwa ajili ya wahudumu kumhudumia mteja pale alipo badala ya mteja kufuata ndoo.
Imekuwa desturi, wahudumu wakishamnawisha mteja, chombo cha sabuni hutupwa mle mle kwenye bakuli la maji machafu waliyokwisha nawia wateja. Pia birika au jagi la maji "safi" huwekwa humo humo ndani ya bakuli. Ikumbukwe chombo cha sabuni kina tundu hivyo ni rahisi uchafu walionawa wateja kuingia kwenye chombo cha sabuni!
Tabia zaidi ni kwamba maji "safi" yakiisha kwenye jagi au birika, jagi au birika hilo hilo ambalo limo ndani ya bakuli lenye maji machafu waliyoanawaia wateja husukumizwa ndani ya ndoo ya maji "safi" na kujazwa maji mengine! Ndoo moja inaweza kusukumizwa mabirika au majagi mengi yaliyonawisha wateja wengi na wenye uchafu wa kila aina!
Kwa wazoefu wa kupata huduma kwenye mabaa iwe huduma za vinywaji au vyakula hawatakuwa wageni na utaratibu huu ambao umerasimishwa huku mamlaka husika zikiwa zimelala! Hii kitu ni hatari sana kwa afya za wananchi! Kwa kutolea mfano, mlioko Dodoma nendeni kwenye zile baa maarufu kwa kuku na nyama choma mtakutana na tabia hii halafu wahusika hawana hata wasiwasi! Mambo ni hayo hayo kwenye mabaa na maeneo mengine yanayotoa huduma za vinywaji na vyakula!
Tabia nyingine, wahudumu wengi kama sio wote hawana desturi ya kunawa wanapotoka maliwatoni. Akikurupuka huko huyooo kaunta kumbebea mteja kinywaji, glass, na tishu! Ukimshtukia jibu ni rahisi tu "nimenawa mle chooni" wakati inaeleweka chooni kwenyewe maji hamna na hata yangekuwepo usafi mle ndani ni mdogo mno!
Mamlaka husika amkeni na timizeni wajibu wenu!
Kuna tabia moja ni kama umeshazoeleka hususan kwenye mabaa. Kanuni za afya zinawataka wenye mabaa na migahawa kuwa na sink au chombo cha maji safi na sabuni kwa ajili ya wateja kunawa kabla na baada ya kula au baada ya kwenda haja.
Kutokana na utaratibu huo, mabaa mengi huweka ndoo za maji "safi" somewhere kwa ajili ya wateja kujinawia na kwa kawaida ndoo hizi zenye mfuniko huwa na koki so mteja anafungulia na kujinawia zake. Pamoja na ndoo, baa nyingi huwa na vyombo vingine kama mabirika, majagi, mabakuli, na vyombo (chupa za plastiki zilizotobolewa mifuniko) vya sabuni za maji kwa ajili ya wahudumu kumhudumia mteja pale alipo badala ya mteja kufuata ndoo.
Imekuwa desturi, wahudumu wakishamnawisha mteja, chombo cha sabuni hutupwa mle mle kwenye bakuli la maji machafu waliyokwisha nawia wateja. Pia birika au jagi la maji "safi" huwekwa humo humo ndani ya bakuli. Ikumbukwe chombo cha sabuni kina tundu hivyo ni rahisi uchafu walionawa wateja kuingia kwenye chombo cha sabuni!
Tabia zaidi ni kwamba maji "safi" yakiisha kwenye jagi au birika, jagi au birika hilo hilo ambalo limo ndani ya bakuli lenye maji machafu waliyoanawaia wateja husukumizwa ndani ya ndoo ya maji "safi" na kujazwa maji mengine! Ndoo moja inaweza kusukumizwa mabirika au majagi mengi yaliyonawisha wateja wengi na wenye uchafu wa kila aina!
Kwa wazoefu wa kupata huduma kwenye mabaa iwe huduma za vinywaji au vyakula hawatakuwa wageni na utaratibu huu ambao umerasimishwa huku mamlaka husika zikiwa zimelala! Hii kitu ni hatari sana kwa afya za wananchi! Kwa kutolea mfano, mlioko Dodoma nendeni kwenye zile baa maarufu kwa kuku na nyama choma mtakutana na tabia hii halafu wahusika hawana hata wasiwasi! Mambo ni hayo hayo kwenye mabaa na maeneo mengine yanayotoa huduma za vinywaji na vyakula!
Tabia nyingine, wahudumu wengi kama sio wote hawana desturi ya kunawa wanapotoka maliwatoni. Akikurupuka huko huyooo kaunta kumbebea mteja kinywaji, glass, na tishu! Ukimshtukia jibu ni rahisi tu "nimenawa mle chooni" wakati inaeleweka chooni kwenyewe maji hamna na hata yangekuwepo usafi mle ndani ni mdogo mno!
Mamlaka husika amkeni na timizeni wajibu wenu!