Wizara gani unadhani Waziri wake Ni Mzigo?

Tunalojukumu lakumsaidia Rais kuboresha utendaji. Lakini pia tunalo jukumu lakubainisha Mawazi na Manaibu Waziri wasio faa ili kuwafanya wakaze buti au kumfanya anayeteua kumtambua nakumweka kando.

Kwa kuanza natamani Waziri wa Sheria Kabudi abadilike nakufanya kazi kitaalamu kuliko anavyoendesha mambo kwa propaganda na kujionyesha yeye tu ndo kasoma.

Lakini nimwombe pia mdogo wangu Waitara aache au apunguze glass, awe serious akijua asipojirekebisha atakwenda kukalia benchi. Ameaminiwa na Mhe. Rais anashindwaje kuhifadhi hadhi aliyopewa?

Kitila Mkumbo namshauri atenganishe ualimu na Uwaziri, aondoke kwenye theory aje kwenye practical. Uvumbuzi utamsaidia la sivyo abaki mbunge

Wengine tujuzane
Wizara ya Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar ni mzigo eti. Wanadai Kisiwa cha Mafia ni cha Sultani kwa hiyo anataka kiende Zanzibar. Kwa nini asiombe na Lamu na Tanga na Mikindani na Sofala?
 
Back
Top Bottom