R Mbuna
JF-Expert Member
- Dec 30, 2015
- 2,278
- 5,319
Habari za wakati huu wana MMU,
Jumamosi ya juzi nilivyotoka kazini nikawa sina mahali pakwenda kupumzika kama mnavyojua hiyo siku huwa tunafanya kazi nusu siku.
Mke wangu kipenzi alikuwa amesafiri so nikaona niende kwa mchepuko wangu bila kutoa taarifa kwake. Nilivyofika mlangoni nikaona kuna sandals za kiume sikuwa na shaka ila radio ilifunguliwa kwa sauti ya juu sana.
Niligonga mlango wala sikupata majibu yoyote ikabidi nimpigie simu lakini haikupokelewa.Ikabidi nisepe ila roho ilikuwa inaniuma sana.
Baada ya dakika tano wala sikuwa nimefika mbali akanibip nikampigia. Akasema nipo kwenye gari simu ilivyoita sikuisikia, nikamuuliza nyumbani kuna mtu akasema nyumba ameifunga so hakuna mtu. Nikasikia hasira sana yaani amenifanya mimi boya.
Ikabidi nigeuze nirudi mpaka pale kwake ili nihakikishe kama kweli hakuna mtu au niliangalia vibaya. Bahati nzuri pale nilimfungulia biashara ya kuuza duka na duka lilikuwa wazi nikaenda dukani nikajifanya nahitaji kununua bidhaa pale mara akatoka yeye alivyoniona alipata mshtuko mpaka akawa ameganda tu pale hata hajanisemesha mbaya zaidi alikuwa amevaa upande tu wa kanga.
Nikamuuliza umerudi saa ngapi hakujibu nikamwaambia endelea na maisha yako mama siwezi kupigana mimi.
Jana Jumapili ilipita kimya hakunisumbua wala nini ila leo nashangaa ghafla nakuta msg ya kuomba msamaha na maelezo kibao wala sijamjibu mpaka sasa na nilishatia nia ya kumuacha moja kwa moja kwasababu sina nguvu za kupigania papuchi.
Kwa wale wazoefu hivi roho inapouma kwa mchepuko wako kuchepuka katika nyumba unayolipia kodi ni dalili ya wivu au ni kujihisi umefanywa mjinga?
Jumamosi ya juzi nilivyotoka kazini nikawa sina mahali pakwenda kupumzika kama mnavyojua hiyo siku huwa tunafanya kazi nusu siku.
Mke wangu kipenzi alikuwa amesafiri so nikaona niende kwa mchepuko wangu bila kutoa taarifa kwake. Nilivyofika mlangoni nikaona kuna sandals za kiume sikuwa na shaka ila radio ilifunguliwa kwa sauti ya juu sana.
Niligonga mlango wala sikupata majibu yoyote ikabidi nimpigie simu lakini haikupokelewa.Ikabidi nisepe ila roho ilikuwa inaniuma sana.
Baada ya dakika tano wala sikuwa nimefika mbali akanibip nikampigia. Akasema nipo kwenye gari simu ilivyoita sikuisikia, nikamuuliza nyumbani kuna mtu akasema nyumba ameifunga so hakuna mtu. Nikasikia hasira sana yaani amenifanya mimi boya.
Ikabidi nigeuze nirudi mpaka pale kwake ili nihakikishe kama kweli hakuna mtu au niliangalia vibaya. Bahati nzuri pale nilimfungulia biashara ya kuuza duka na duka lilikuwa wazi nikaenda dukani nikajifanya nahitaji kununua bidhaa pale mara akatoka yeye alivyoniona alipata mshtuko mpaka akawa ameganda tu pale hata hajanisemesha mbaya zaidi alikuwa amevaa upande tu wa kanga.
Nikamuuliza umerudi saa ngapi hakujibu nikamwaambia endelea na maisha yako mama siwezi kupigana mimi.
Jana Jumapili ilipita kimya hakunisumbua wala nini ila leo nashangaa ghafla nakuta msg ya kuomba msamaha na maelezo kibao wala sijamjibu mpaka sasa na nilishatia nia ya kumuacha moja kwa moja kwasababu sina nguvu za kupigania papuchi.
Kwa wale wazoefu hivi roho inapouma kwa mchepuko wako kuchepuka katika nyumba unayolipia kodi ni dalili ya wivu au ni kujihisi umefanywa mjinga?