AbuuMaryam
JF-Expert Member
- Dec 26, 2015
- 2,537
- 4,517
بسم الله الرحمن الرحيم.
Mimi ni mwalim wa dini na imam katika msikiti ulipo eneo ninalo ishi...
Kwa nafasi yangu huwa napokea kesi na migogoro mbalimbali kusuluhisha na kushauri.
Nina wito huu kwa wanandoa wa dini zote na mamlaka zote zinahusika na masuala ya ndoa na muunganiko wa kijamii;
1. Mke na mume. Mapenzi ni kama kiumbe chochote kile...Huzaliwa, hukua, hustawi na mwishoni hupata maradhi(ambayo ndio migogoro ya ndoa) na mwishoe hufa kabisa.
2. Chondechonde wanandoa...Usikubali wala usilazimishe kuishi na mtu ambae wazi anaonekana hakupendi tena kwa ishara zote atakazokuonesha kuwa hakupendi bila shaka...Au usiishi na kuforce kuishi na mtu ambae humpendi.
3. Kwakuwa ndoa iliasisiwa na mapenzi. Basi yanapoisha mapenzi...Na ndoa vilevile haina kazi tena...
4. Watoto wasitumike kama sababu ya kulazimisha watu wasiopendana waishi pamoja, hao watoto walikuja kwa wakati wao, wakakuta watu wamependana ndipo wakapatikana wao...Watoto hawakuwa chanzo cha wazazi wao kukutana. Wamekuja baadae. Kwahiyo wasitumike kama sababu ya kulazimisha mapenzi yaliyokufa.
5. Ukiona humpendi mtu tena kama unaweza na unamuamini anaweza kuhimili utakapomwambia kuwa humpendi. Basi mwambie. Kama huwezi. Potea kabisa kwenye upeo wa macho yake. Kwa kipindi kidogo ili azoee kuishi bila wewe.
6. Ukiona unampenda mtu lakini yeye hakupendi tena... Kubali...Ndio maisha...Nyanyuka hapo...Pukusa makalio yako...Piga hatua moja mbili tatu...Songa mbele maisha yanaendelea... Kila lenye mwanzo halikosi mwisho .
Kwa sababu mapenzi ni kama daladala. Siti uliyokalia leo. Alikalia mtu jana. Hivyo kesho atakalia mtu mwingine...Haya ndio maisha.
7. Hukuzaliwa na mtu...Kiasi kwamba kwakuwa umependana na mtu kwenye maisha yako...Basi kutengana lazima iwe ni kifo...La hasha...Kwa sababu kabla yake huyo mtu unayempenda uliishi vizuri tu bila tabu...Iweje iwe tabu baada yake ..Kubali songa mbele utapata mwingine. Naye utaachana nae utaenda kwa mwingine...Ndio maisha...
8. Inapotokea unamfuatilia mwenza wako. Jipime na ujikadirie. Hayo unayoyafuatilia utakapoyaona unaweza kustahamili...? Yaani kwa mfano ukigundua mkeo anachepuka. Unaweza ukafanya maamuzi ya kumuacha? Kama huna uwezo huo unafuatilia ya nini? Kubali kuwa mume zoba upate unachokusudia...Ila kama ukifuatilia ukagundua anakusaliti ..Unaweza kumuacha. Achana nae tupa kule.
9. Usikubali kufa, kudhurika wala kubeba dhambi ya kuua mtu bure, wala dhambi ya kudhuru mtu ambae hata hujui kitovu chake kilidondokaje...Huo ushetani...Uzuzu Upoyoyo...Upumbavu na ujinga wa hali ya juu.
10. Ukiona umefumaniwa live na mwenzio. Ule msamaha unaopewa baada ya fumanizi usiuamini kamwe...Na wewe songa mbele endelea maisha na huyo uliyefumaniwa naye.
Ukiona eti nimekusamehe. Ujue ni bomu la kisasi linaandaliwa kwa ajili yako...Usirudi nyuma. Utajutia milele.
11. Polisi, mahakama, bakwata, mabaraza ya usuluhishi katika taasisi zote za kidini. Jamani linapokuja kwenu gogoro lolote la ndoa baina ya wanandoa.
Msiwarudishe wakayazungumze au kuwalazimisha waendelee kuishi pamoja hali ya kuwa bado wana migogoro...Tena wasaidieni hata kuwatenganisha kwa muda au hata milele panapobidi.
Kwa sababu mpaka limefika kwenu. Ujue wao binafsi limewashinda ..
Na huku mkijulisha vyombo vya usalama ili kufuatilia usalama wa baina ya wanandoa ili wasije leteana madhara wenyewe kwa wenyewe.
Mwisho;
Tusisahau kuwa sisi ni binadamu watu...Tuwe na roho za kiutu...Tusiendekeze za kishetani kudhuriana kisa...A mere thing eti "Nampenda" eti "Amenisaliti"!.
Mimi ni mwalim wa dini na imam katika msikiti ulipo eneo ninalo ishi...
Kwa nafasi yangu huwa napokea kesi na migogoro mbalimbali kusuluhisha na kushauri.
Nina wito huu kwa wanandoa wa dini zote na mamlaka zote zinahusika na masuala ya ndoa na muunganiko wa kijamii;
1. Mke na mume. Mapenzi ni kama kiumbe chochote kile...Huzaliwa, hukua, hustawi na mwishoni hupata maradhi(ambayo ndio migogoro ya ndoa) na mwishoe hufa kabisa.
2. Chondechonde wanandoa...Usikubali wala usilazimishe kuishi na mtu ambae wazi anaonekana hakupendi tena kwa ishara zote atakazokuonesha kuwa hakupendi bila shaka...Au usiishi na kuforce kuishi na mtu ambae humpendi.
3. Kwakuwa ndoa iliasisiwa na mapenzi. Basi yanapoisha mapenzi...Na ndoa vilevile haina kazi tena...
4. Watoto wasitumike kama sababu ya kulazimisha watu wasiopendana waishi pamoja, hao watoto walikuja kwa wakati wao, wakakuta watu wamependana ndipo wakapatikana wao...Watoto hawakuwa chanzo cha wazazi wao kukutana. Wamekuja baadae. Kwahiyo wasitumike kama sababu ya kulazimisha mapenzi yaliyokufa.
5. Ukiona humpendi mtu tena kama unaweza na unamuamini anaweza kuhimili utakapomwambia kuwa humpendi. Basi mwambie. Kama huwezi. Potea kabisa kwenye upeo wa macho yake. Kwa kipindi kidogo ili azoee kuishi bila wewe.
6. Ukiona unampenda mtu lakini yeye hakupendi tena... Kubali...Ndio maisha...Nyanyuka hapo...Pukusa makalio yako...Piga hatua moja mbili tatu...Songa mbele maisha yanaendelea... Kila lenye mwanzo halikosi mwisho .
Kwa sababu mapenzi ni kama daladala. Siti uliyokalia leo. Alikalia mtu jana. Hivyo kesho atakalia mtu mwingine...Haya ndio maisha.
7. Hukuzaliwa na mtu...Kiasi kwamba kwakuwa umependana na mtu kwenye maisha yako...Basi kutengana lazima iwe ni kifo...La hasha...Kwa sababu kabla yake huyo mtu unayempenda uliishi vizuri tu bila tabu...Iweje iwe tabu baada yake ..Kubali songa mbele utapata mwingine. Naye utaachana nae utaenda kwa mwingine...Ndio maisha...
8. Inapotokea unamfuatilia mwenza wako. Jipime na ujikadirie. Hayo unayoyafuatilia utakapoyaona unaweza kustahamili...? Yaani kwa mfano ukigundua mkeo anachepuka. Unaweza ukafanya maamuzi ya kumuacha? Kama huna uwezo huo unafuatilia ya nini? Kubali kuwa mume zoba upate unachokusudia...Ila kama ukifuatilia ukagundua anakusaliti ..Unaweza kumuacha. Achana nae tupa kule.
9. Usikubali kufa, kudhurika wala kubeba dhambi ya kuua mtu bure, wala dhambi ya kudhuru mtu ambae hata hujui kitovu chake kilidondokaje...Huo ushetani...Uzuzu Upoyoyo...Upumbavu na ujinga wa hali ya juu.
10. Ukiona umefumaniwa live na mwenzio. Ule msamaha unaopewa baada ya fumanizi usiuamini kamwe...Na wewe songa mbele endelea maisha na huyo uliyefumaniwa naye.
Ukiona eti nimekusamehe. Ujue ni bomu la kisasi linaandaliwa kwa ajili yako...Usirudi nyuma. Utajutia milele.
11. Polisi, mahakama, bakwata, mabaraza ya usuluhishi katika taasisi zote za kidini. Jamani linapokuja kwenu gogoro lolote la ndoa baina ya wanandoa.
Msiwarudishe wakayazungumze au kuwalazimisha waendelee kuishi pamoja hali ya kuwa bado wana migogoro...Tena wasaidieni hata kuwatenganisha kwa muda au hata milele panapobidi.
Kwa sababu mpaka limefika kwenu. Ujue wao binafsi limewashinda ..
Na huku mkijulisha vyombo vya usalama ili kufuatilia usalama wa baina ya wanandoa ili wasije leteana madhara wenyewe kwa wenyewe.
Mwisho;
Tusisahau kuwa sisi ni binadamu watu...Tuwe na roho za kiutu...Tusiendekeze za kishetani kudhuriana kisa...A mere thing eti "Nampenda" eti "Amenisaliti"!.