Wito: Unapopata Nafasi, Wafariji wagonjwa na wenye uhitaji

Mtende

JF-Expert Member
Sep 27, 2010
6,385
7,295
Heri ya mwaka mpya wanafamilia wa JF, naamini kila mmoja amemaliza mwaka salama pamoja na misukosuko mingi tuliyopitia, ni Mwaka mwingine tena tuombe heri kwa kila tunalofanya.

Moja kwa moja niende kwenye mada, imekua desturi kwangu na familia kila tunapopata nafasi tunapita mahospitali au vituo vya watoto yatima kuwafariji kwa chochote hata kidogo ikiwa ni kama sehemu ya sadaka.

Jana tulikwenda Ocean road kuwaona wagonjwa wa Cancer, kiukweli moyo wangu umevunjika sana, nimejikuta nina huzuni kubwa na simanzi lakini na woga pia kutokana na hali za wagonjwa, wengine wamekaa hospitali kwa zaidi ya miezi sita na familia zao zimewatelekeza hawana msaada wa namna yoyote na wapo katika hali ya ugonjwa na maumivu makubwa, akina mama na watoto wametelekezwa na hawana wa kuwapelekea japo mahitaji muhimu kama vile pads, pants,sabuni za kuogea, vocha nk
Wengine hospitali pamekua kama second home kwao na hawana hata mtu wa kwatia moyo wala kuwafariji japo kwa maneno mazuri ( nimesme tu MSHUKURU MUNGU HATA KWA AFYA ULIYONAYO)

Nilifarijika baada ya kuwaona akina mama wa kisomali, wahindi na jamii ya watu wa Asia wakitoa misaada kama vyakula, pads, nguo, sabuni za kuoga na niliambiwa kwamba hao akina mama kila siku asubuhi na jioni hufika kuwagawia wagonjwa chai/uji chakula cha mchana na cha jioni pia, ni kama wanapeana zamu, hawakauki pale hospitali

On the other side nilipata maswali mengi sana nilipowaza viongozi na waumini wa makanisa makubwa kama kwa Mwamposa, KKT, RC, akina Mwingira, Kakobe, Gwajima na sadaka zote wanazopokea wanashindwa japo kurudisha upendo kwa jamii yenye uhitaji, nilikutana na mchungaji mmoja underground alikua anawaombea wagonjwa akaniambia hata akina Mwamposa kabla hawajawa wakubwa walikua wanapita kuwaombea wagonjwa lakini sasa wanatembea na mabodigadi

nawapongeza sana Waislamu, wahindi wasomali kwa upendo wao juu ya wale wagonjwa, Wakristo tujifunze jambo, tusiishie tu kupeleka sadaka zetu kwa wachungaji wachumia tumbo, tuwakumbuke na hawa wenye uhitaji, nayo ni sadaka kuvwa Mbele za Mungu

Mwisho, niseme nimejifunza jambo kubwa sana, kuna watu wanateseka na magonjwa ya kila aina, wamekata tamaa na hawana matumaini ya kuendelea kuishi, sisi ambao ni wazima tunatembea na kucheka na tunafuhia na familia zeti, hebu kila tunapopata nafasi tupite hospitali mbalimbali kuwafariji wagonjwa kwa chochote, hasa wale waliotelekezwa na familia zao na hawana msaada wowote, hata kama huna pesa au chochote cha kuwapa, neno lako la faraja linaweza kumpa uponyaji wa nafsi na tumaini jipya la kuishi na pengine tabasamu kwenye uso wake.

Mungu awabariki na kuwapa afya njema.
 
Heri ya mwaka mpya wanafamilia wa JF, naamini kila mmoja amemaliza mwaka salama pamoja na misukosuko mingi tuliyopitia, ni Mwaka mwingine tena tuombe heri kwa kila tunalofanya.

Moja kwa moja niende kwenye mada, imekua desturi kwangu na familia kila tunapopata nafasi tunapita mahospitali au vituo vya watoto yatima kuwafariji kwa chochote hata kidogo ikiwa ni kama sehemu ya sadaka.

Jana tulikwenda Ocean road kuwaona wagonjwa wa Cancer, kiukweli moyo wangu umevunjika sana, nimejikuta nina huzuni kubwa na simanzi lakini na woga pia kutokana na hali za wagonjwa, wengine wamekaa hospitali kwa zaidi ya miezi sita na familia zao zimewatelekeza hawana msaada wa namna yoyote na wapo katika hali ya ugonjwa na maumivu makubwa, akina mama na watoto wametelekezwa na hawana wa kuwapelekea japo mahitaji muhimu kama vile pads, pants,sabuni za kuogea, vocha nk
Wengine hospitali pamekua kama second home kwao na hawana hata mtu wa kwatia moyo wala kuwafariji japo kwa maneno mazuri ( nimesme tu MSHUKURU MUNGU HATA KWA AFYA ULIYONAYO)

Nilifarijika baada ya kuwaona akina mama wa kisomali, wahindi na jamii ya watu wa Asia wakitoa misaada kama vyakula, pads, nguo, sabuni za kuoga na niliambiwa kwamba hao akina mama kila siku asubuhi na jioni hufika kuwagawia wagonjwa chai/uji chakula cha mchana na cha jioni pia, ni kama wanapeana zamu, hawakauki pale hospitali

On the other side nilipata maswali mengi sana nilipowaza viongozi na waumini wa makanisa makubwa kama kwa Mwamposa, KKT, RC, akina Mwingira, Kakobe, Gwajima na sadaka zote wanazopokea wanashindwa japo kurudisha upendo kwa jamii yenye uhitaji, nilikutana na mchungaji mmoja underground alikua anawaombea wagonjwa akaniambia hata akina Mwamposa kabla hawajawa wakubwa walikua wanapita kuwaombea wagonjwa lakini sasa wanatembea na mabodigadi

nawapongeza sana Waislamu, wahindi wasomali kwa upendo wao juu ya wale wagonjwa, Wakristo tujifunze jambo, tusiishie tu kupeleka sadaka zetu kwa wachungaji wachumia tumbo, tuwakumbuke na hawa wenye uhitaji, nayo ni sadaka kuvwa Mbele za Mungu

Mwisho, niseme nimejifunza jambo kubwa sana, kuna watu wanateseka na magonjwa ya kila aina, wamekata tamaa na hawana matumaini ya kuendelea kuishi, sisi ambao ni wazima tunatembea na kucheka na tunafuhia na familia zeti, hebu kila tunapopata nafasi tupite hospitali mbalimbali kuwafariji wagonjwa kwa chochote, hasa wale waliotelekezwa na familia zao na hawana msaada wowote, hata kama huna pesa au chochote cha kuwapa, neno lako la faraja linaweza kumpa uponyaji wa nafsi na tumaini jipya la kuishi na pengine tabasamu kwenye uso wake.

Mungu awabariki na kuwapa afya njema.

Naam,
Hii ni ibada njema sana. Ninachowaomba, mkienda kuwafariji wahitaji na wagonjwa msipige picha na kuanza kuzirusha mitandaoni na kwenye mitivii. Ukifanya hivyo unaharibu sadaka yako. Vinginevyo neno lako hili ni la kutembea nalo maishani.
 
Happy new year kwako pia Mtende,
Naomba tu niseme, hata sisi it's just a matter of when, we're not so special kwamba wanayopitia wenzetu sisi hatutapitia, huu ni mwendo wa kupokezana vijiti kwamba leo ndio fate yao, kesho itakuwa ya mwingine and eventually itafika zamu yetu.

Waliotangulia kupata majanga tuna kila sababu ya kuwatembelea na kuwapa faraja huku na sisi tukijiandaa kwa namna tutapokea maumivu yetu.

Sipingani na ulichoandika though, Ila tukumbuke hatuko special, kila mtu atakinywea kwa namna na wakati wake.
 
Naam,
Hii ni ibada njema sana. Ninachowaomba, mkienda kuwafariji wahitaji na wagonjwa msipige picha na kuanza kuzirusha mitandaoni na kwenye mitivii. Ukifanya hivyo unaharibu sadaka yako. Vinginevyo neno lako hili ni la kutembea nalo maishani.
Huwezi kupata nguvu ya kupiga hata picha kwa hali niliyowaona nayo wale wagonjwa, hata usingizi kwangu umekua wa tabu, nimejikuta naamini kweli kifo kipo
 
Happy new year kwako pia Mtende,
Naomba tu niseme, hata sisi it's just a matter of when, we're not so special kwamba wanayopitia wenzetu sisi hatutapitia, huu ni mwendo wa kupokezana vijiti kwamba leo ndio fate yao, kesho itakuwa ya mwingine and eventually itafika zamu yetu.

Waliotangulia kupata majanga tuna kila sababu ya kuwatembelea na kuwapa faraja huku na sisi tukijiandaa kwa namna tutapokea maumivu yetu.

Sipingani na ulichoandika though, Ila tukumbuke hatuko special, kila mtu atakinywea kwa namna na wakati wake.
Indeed Eli79
 
Heri ya mwaka mpya wanafamilia wa JF, naamini kila mmoja amemaliza mwaka salama pamoja na misukosuko mingi tuliyopitia, ni Mwaka mwingine tena tuombe heri kwa kila tunalofanya.

Moja kwa moja niende kwenye mada, imekua desturi kwangu na familia kila tunapopata nafasi tunapita mahospitali au vituo vya watoto yatima kuwafariji kwa chochote hata kidogo ikiwa ni kama sehemu ya sadaka.

Jana tulikwenda Ocean road kuwaona wagonjwa wa Cancer, kiukweli moyo wangu umevunjika sana, nimejikuta nina huzuni kubwa na simanzi lakini na woga pia kutokana na hali za wagonjwa, wengine wamekaa hospitali kwa zaidi ya miezi sita na familia zao zimewatelekeza hawana msaada wa namna yoyote na wapo katika hali ya ugonjwa na maumivu makubwa, akina mama na watoto wametelekezwa na hawana wa kuwapelekea japo mahitaji muhimu kama vile pads, pants,sabuni za kuogea, vocha nk
Wengine hospitali pamekua kama second home kwao na hawana hata mtu wa kwatia moyo wala kuwafariji japo kwa maneno mazuri ( nimesme tu MSHUKURU MUNGU HATA KWA AFYA ULIYONAYO)

Nilifarijika baada ya kuwaona akina mama wa kisomali, wahindi na jamii ya watu wa Asia wakitoa misaada kama vyakula, pads, nguo, sabuni za kuoga na niliambiwa kwamba hao akina mama kila siku asubuhi na jioni hufika kuwagawia wagonjwa chai/uji chakula cha mchana na cha jioni pia, ni kama wanapeana zamu, hawakauki pale hospitali

On the other side nilipata maswali mengi sana nilipowaza viongozi na waumini wa makanisa makubwa kama kwa Mwamposa, KKT, RC, akina Mwingira, Kakobe, Gwajima na sadaka zote wanazopokea wanashindwa japo kurudisha upendo kwa jamii yenye uhitaji, nilikutana na mchungaji mmoja underground alikua anawaombea wagonjwa akaniambia hata akina Mwamposa kabla hawajawa wakubwa walikua wanapita kuwaombea wagonjwa lakini sasa wanatembea na mabodigadi

nawapongeza sana Waislamu, wahindi wasomali kwa upendo wao juu ya wale wagonjwa, Wakristo tujifunze jambo, tusiishie tu kupeleka sadaka zetu kwa wachungaji wachumia tumbo, tuwakumbuke na hawa wenye uhitaji, nayo ni sadaka kuvwa Mbele za Mungu

Mwisho, niseme nimejifunza jambo kubwa sana, kuna watu wanateseka na magonjwa ya kila aina, wamekata tamaa na hawana matumaini ya kuendelea kuishi, sisi ambao ni wazima tunatembea na kucheka na tunafuhia na familia zeti, hebu kila tunapopata nafasi tupite hospitali mbalimbali kuwafariji wagonjwa kwa chochote, hasa wale waliotelekezwa na familia zao na hawana msaada wowote, hata kama huna pesa au chochote cha kuwapa, neno lako la faraja linaweza kumpa uponyaji wa nafsi na tumaini jipya la kuishi na pengine tabasamu kwenye uso wake.

Mungu awabariki na kuwapa afya njema.
Kwanza mshkuru muumba kwa kukupa wasaa wa kufika hapo hosp ni jambo adhimu sana muumba akuongoze kwa hilo.

Lakini pia sisi tunafundishwa mara nyengine uwapo na shida binafsi toa sadaka huku ukimuomba muumba akuhurumie ma kukuondolea machungu au tatizo au shida yako.

Lakini pia twapaswa kujenga utaratibu wa kuwatembelea wagonjwa wafungwa mayatima kwa kufanya haya kutasaidia kulainisha nyoyo zetu na kuwafikiria wahitaji na kwa hili naamini baraka na neema nyingi kutoka kwa muumba zitatushukia.
 
Kwanza mshkuru muumba kwa kukupa wasaa wa kufika hapo hosp ni jambo adhimu sana muumba akuongoze kwa hilo.
Lakini pia sisi tunafundishwa mara nyengine uwapo na shida binafsi toa sadaka huku ukimuomba muumba akuhurumie ma kukuondolea machungu au tatizo au shida yako.
Lakini pia twapaswa kujenga utaratibu wa kuwatembelea wagonjwa wafungwa mayatima kwa kufanya haya kutasaidia kulainisha nyoyo zetu na kuwafikiria wahitaji na kwa hili naamini baraka na neema nyingi kutoka kwa muumba zitatushukia.
Amen, Umesema kweli kabisa, Mungu atuwezeshe kwa kweli
 
Barikiwa sana Mtende ,umenifanya niongeze moja ya ratiba zangu kwa mwaka huu iwe ni kutembelea wagonjwa..kusema ukweli naendaga hospitali kuona ndugu,jamaa au pengine nikiumwa lakini kupitia bandiko hili umetukumbusha jambo la msingi.

Uzima tulionao unatudanganya sana,lakini naungana na wewe tukipata wasaa wa kwenda kuona wagonjwa kwa hakika tutaona ni kwa namna gani Mungu ametubariki kwa neema hii ya uzima.
 
Barikiwa sana Mtende ,umenifanya niongeze moja ya ratiba zangu kwa mwaka huu iwe ni kutembelea wagonjwa..kusema ukweli naendaga hospitali kuona ndugu,jamaa au pengine nikiumwa lakini kupitia bandiko hili umetukumbusha jambo la msingi.

Uzima tulionao unatudanganya sana,lakini naungana na wewe tukipata wasaa wa kwenda kuona wagonjwa kwa hakika tutaona ni kwa namna gani Mungu ametubariki kwa neema hii ya uzima.
Amen, Mungu akuwezeshe ndugu
 
Ni sadaka nzuri sana,
Mimi tarehe 26 Dec i took my beloved wife tukasafir kwenda kusalimia wafungwa katika gereza moja huko kaskazini.

Tulitenga kiasi cha pesa tukanunua mahitaji basics kwenye duka la magereza na kuwapelekea. Tulipatwa na huzuni sana lakn naamini kwetu ilikuwa ni ibada nzuri kwa mwaka huu.

Kuanzia mwaka huu tumejipangia kuwa na utaratibu wa kutembelea vituo vya watoto yatima, wagonjwa na wahitaji mbalimbali.
 
Heri ya mwaka mpya wanafamilia wa JF, naamini kila mmoja amemaliza mwaka salama pamoja na misukosuko mingi tuliyopitia, ni Mwaka mwingine tena tuombe heri kwa kila tunalofanya.

Moja kwa moja niende kwenye mada, imekua desturi kwangu na familia kila tunapopata nafasi tunapita mahospitali au vituo vya watoto yatima kuwafariji kwa chochote hata kidogo ikiwa ni kama sehemu ya sadaka.

Jana tulikwenda Ocean road kuwaona wagonjwa wa Cancer, kiukweli moyo wangu umevunjika sana, nimejikuta nina huzuni kubwa na simanzi lakini na woga pia kutokana na hali za wagonjwa, wengine wamekaa hospitali kwa zaidi ya miezi sita na familia zao zimewatelekeza hawana msaada wa namna yoyote na wapo katika hali ya ugonjwa na maumivu makubwa, akina mama na watoto wametelekezwa na hawana wa kuwapelekea japo mahitaji muhimu kama vile pads, pants,sabuni za kuogea, vocha nk
Wengine hospitali pamekua kama second home kwao na hawana hata mtu wa kwatia moyo wala kuwafariji japo kwa maneno mazuri ( nimesme tu MSHUKURU MUNGU HATA KWA AFYA ULIYONAYO)

Nilifarijika baada ya kuwaona akina mama wa kisomali, wahindi na jamii ya watu wa Asia wakitoa misaada kama vyakula, pads, nguo, sabuni za kuoga na niliambiwa kwamba hao akina mama kila siku asubuhi na jioni hufika kuwagawia wagonjwa chai/uji chakula cha mchana na cha jioni pia, ni kama wanapeana zamu, hawakauki pale hospitali

On the other side nilipata maswali mengi sana nilipowaza viongozi na waumini wa makanisa makubwa kama kwa Mwamposa, KKT, RC, akina Mwingira, Kakobe, Gwajima na sadaka zote wanazopokea wanashindwa japo kurudisha upendo kwa jamii yenye uhitaji, nilikutana na mchungaji mmoja underground alikua anawaombea wagonjwa akaniambia hata akina Mwamposa kabla hawajawa wakubwa walikua wanapita kuwaombea wagonjwa lakini sasa wanatembea na mabodigadi

nawapongeza sana Waislamu, wahindi wasomali kwa upendo wao juu ya wale wagonjwa, Wakristo tujifunze jambo, tusiishie tu kupeleka sadaka zetu kwa wachungaji wachumia tumbo, tuwakumbuke na hawa wenye uhitaji, nayo ni sadaka kuvwa Mbele za Mungu

Mwisho, niseme nimejifunza jambo kubwa sana, kuna watu wanateseka na magonjwa ya kila aina, wamekata tamaa na hawana matumaini ya kuendelea kuishi, sisi ambao ni wazima tunatembea na kucheka na tunafuhia na familia zeti, hebu kila tunapopata nafasi tupite hospitali mbalimbali kuwafariji wagonjwa kwa chochote, hasa wale waliotelekezwa na familia zao na hawana msaada wowote, hata kama huna pesa au chochote cha kuwapa, neno lako la faraja linaweza kumpa uponyaji wa nafsi na tumaini jipya la kuishi na pengine tabasamu kwenye uso wake.

Mungu awabariki na kuwapa afya njema.
Mkuu asante sana kunikumbusha hili jambo,tatizo ni kujiona hatuna cha kutosha kusaidia wenye uhitaji wakati budget ya kuchepuka kila mwezi karibu laki 2. Naanza January hiihii ili nipate na nguvu ya kusahau michepuko
 
Mimi nimeshuhudia tulivyokua hosp (leba) huyo mmoja tumbo lake lilijaa fungus aisee inatisha, ukiwa hosp unajifunza mambo mengi sana

Pia nimeshawaona wagonjwa wa kisukari wawili, mmoja alipata kidonda mguuni kupelekea mguu wake kuvimba na kua na vidonda mguu mzima (unatisha) mwingine alipata kipele makalioni akakitumbua basi akaanza kuumwa hadi kufa!!

Aliteseka sanaaaaa, damu ilifika 3 ukimuona kitandani utasema hamna kitu na mtu alikua na mwili wake tu alikaa hosp more than a year akirudi nyumbani baada ya siku 2 mnarudi tena hosp

Nimepoteza mtoto mwaka jana, ila namshukuru Mungu kwa uhai na afya njema hadi sasa
 
Mkuu asante sana kunikumbusha hili jambo,tatizo ni kujiona hatuna cha kutosha kusaidia wenye uhitaji wakati budget ya kuchepuka kila mwezi karibu laki 2. Naanza January hiihii ili nipate na nguvu ya kusahau michepuko
Mungu Akutangulie ndugu, bila hata pesa, hawa watu wanahitaji upendo na faraja
 
Mimi nimeshuhudia tulivyokua hosp (leba) huyo mmoja tumbo lake lilijaa fungus aisee inatisha, ukiwa hosp unajifunza mambo mengi sana

Pia nimeshawaona wagonjwa wa kisukari wawili, mmoja alipata kidonda mguuni kupelekea mguu wake kuvimba na kua na vidonda mguu mzima (unatisha) mwingine alipata kipele makalioni akakitumbua basi akaanza kuumwa hadi kufa!!

Aliteseka sanaaaaa, damu ilifika 3 ukimuona kitandani utasema hamna kitu na mtu alikua na mwili wake tu alikaa hosp more than a year akirudi nyumbani baada ya siku 2 mnarudi tena hosp

Nimepoteza mtoto mwaka jana, ila namshukuru Mungu kwa uhai na afya njema hadi sasa
Pole sana dear Pisi kali Mungu akutie nguvu, tunahitaji kuwafariji sana hawa watu, naamini Mungu atatupa wa kutufariji nasisi tunapokutana na hali hizo maana hujafa hujaumbika
 
Heri ya mwaka mpya wanafamilia wa JF, naamini kila mmoja amemaliza mwaka salama pamoja na misukosuko mingi tuliyopitia, ni Mwaka mwingine tena tuombe heri kwa kila tunalofanya.

Moja kwa moja niende kwenye mada, imekua desturi kwangu na familia kila tunapopata nafasi tunapita mahospitali au vituo vya watoto yatima kuwafariji kwa chochote hata kidogo ikiwa ni kama sehemu ya sadaka.

Jana tulikwenda Ocean road kuwaona wagonjwa wa Cancer, kiukweli moyo wangu umevunjika sana, nimejikuta nina huzuni kubwa na simanzi lakini na woga pia kutokana na hali za wagonjwa, wengine wamekaa hospitali kwa zaidi ya miezi sita na familia zao zimewatelekeza hawana msaada wa namna yoyote na wapo katika hali ya ugonjwa na maumivu makubwa, akina mama na watoto wametelekezwa na hawana wa kuwapelekea japo mahitaji muhimu kama vile pads, pants,sabuni za kuogea, vocha nk
Wengine hospitali pamekua kama second home kwao na hawana hata mtu wa kwatia moyo wala kuwafariji japo kwa maneno mazuri ( nimesme tu MSHUKURU MUNGU HATA KWA AFYA ULIYONAYO)

Nilifarijika baada ya kuwaona akina mama wa kisomali, wahindi na jamii ya watu wa Asia wakitoa misaada kama vyakula, pads, nguo, sabuni za kuoga na niliambiwa kwamba hao akina mama kila siku asubuhi na jioni hufika kuwagawia wagonjwa chai/uji chakula cha mchana na cha jioni pia, ni kama wanapeana zamu, hawakauki pale hospitali

On the other side nilipata maswali mengi sana nilipowaza viongozi na waumini wa makanisa makubwa kama kwa Mwamposa, KKT, RC, akina Mwingira, Kakobe, Gwajima na sadaka zote wanazopokea wanashindwa japo kurudisha upendo kwa jamii yenye uhitaji, nilikutana na mchungaji mmoja underground alikua anawaombea wagonjwa akaniambia hata akina Mwamposa kabla hawajawa wakubwa walikua wanapita kuwaombea wagonjwa lakini sasa wanatembea na mabodigadi

nawapongeza sana Waislamu, wahindi wasomali kwa upendo wao juu ya wale wagonjwa, Wakristo tujifunze jambo, tusiishie tu kupeleka sadaka zetu kwa wachungaji wachumia tumbo, tuwakumbuke na hawa wenye uhitaji, nayo ni sadaka kuvwa Mbele za Mungu

Mwisho, niseme nimejifunza jambo kubwa sana, kuna watu wanateseka na magonjwa ya kila aina, wamekata tamaa na hawana matumaini ya kuendelea kuishi, sisi ambao ni wazima tunatembea na kucheka na tunafuhia na familia zeti, hebu kila tunapopata nafasi tupite hospitali mbalimbali kuwafariji wagonjwa kwa chochote, hasa wale waliotelekezwa na familia zao na hawana msaada wowote, hata kama huna pesa au chochote cha kuwapa, neno lako la faraja linaweza kumpa uponyaji wa nafsi na tumaini jipya la kuishi na pengine tabasamu kwenye uso wake.

Mungu awabariki na kuwapa afya njema.
Naungana nawee mti wa Mtende
 
Back
Top Bottom