Dah hata mie nimeusikia huo wimbo,ni kweli kwa maneno aliyoyaongezea unaweza sema alijitabiria kifo chake..wimbo unateka sana hisia za mtu..kiufupi jamaa alikuwa jembe maeneo mengi hadi kwenye uimbaji.
maneno aliyo yaongeza,yamenigusa kwani ni kama aliona mauti
Maneno yanasema
Siku nikifa,watu watasema hakuna wa kuziba pengo langu
Hata wabaya wangu,watabeba jeneza langu
Watu watasema,ametutoka msanii tuliye mpenda.
" nitayainua macho yangu nitazame milima , msaada wangu utatoka wapi ?msaada wangu u katika bwana , aliyezifanya mbingu na nchi, asiuachu mguu wako usogezwe , asisinzie akulindaye; naam hata sinzia wala hata lala usingizi, yeye aliye mlinzi wa israel. Bwana ndiye mlinzi wako; bwana ni uvuli mkono wako wa kuume . Jua halitakupiga mchana , wala mwezi wakati wa usiku. Bwana atakulindana mabaya yote , atakulinda nafsi yako. Bwanaatakulinda utokapo na uingiapo, tangu sasa na hata milele.
jaman wimbo wa kn umenigusa sana, naweza sema alijitabiria kifo ama nafsi yake ilimtuma pasipo kujua kujitabiria kifo. hasa pale aliimba "hata wanaonichukia watabeba jeneza langu" hakika alikuwa anaaga indirect... rip kn!
Wakuu nimetembelea blog ya wavuti nimeona script ambayo ameshawahi kuigiza marehemu kanumba kwenye igizo la baragumu, yule mtoto alieigiza nae ndiye LULU? kwani nimeona kama amefanana nae, kwa anaemjua vizuri tafadhari tuambie
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.