NGAYANIMO
Member
- Feb 17, 2026
- 36
- 55
DAZ BABA - ELIMU DUNIA.
VERSE.. ( AFANDE SELE)
We ni mfungwa sasa 'si mtu huru/
Ukilalamika sana utakuwa kama unakufuru/
Tu..!!
Lazima ujue sisi ni vifaranga na maisha ni kama mwewe/
Mama yetu ni elimu’ ulio mkataaga we mwenyewe/
zamani..!!
Ulimkataa elimu ya duniani 'ukampiga hadi mwalimu darasani/
Hukusikia la Muadhini wala la mnadi Swala hukuliamini/
Umri ulikudanganya ukawa mbabe shuleni/
Sasa ndio hivyo uko nasi gerezani/
Jiamini mdogo wangu 'kwani jela sio kaburini au kwa Mungu/
Umetengwa na jamii, hujatengwa na dunia hii/
Jifunze kupokea furaha sawa na huzuni/
Kumbuka kwamba tabu na raha zipo duniani/
Zipo kwa ajili ya watu na watu ndio mi na wewe/
Kila mmoja atabeba madhambi yake mwenyewe /
'imeandikwa..!!
Kama umekunywa sumu sasa ya nini uombewe.?
Eenh..?
Sasa ya nini uombewe?
Suleimani msindi a.k.a afande sele member wa Crew ya Watu pori & Ghetto boys msanii kutoka Mji kasoro bahari Morogoro alifanya kweli katika wimbo huu wa msanii
David Selestine Nyika a.k.a Daz baba kutoka kundi la "
" Dangerous Zone Nundaz " au kwa kifupi Daz nundaz ..
Msanii Daz baba alicopy jina la msanii wa Marekani Kwa USA, Daz ni jina la jamaa anaitwa Daz Dillinger, alikuwa mtu wa karibu sana na marehemu 2Pac.
Lakini pia hata huu wimbo wa "Elimu Dunia " Daz baba alitumia Idea ya wimbo wa Marehemu Lucky Dube mwimbaji wa nyimbo Aina ya Reggae kutoka Afrika ya kusini..
Wimbo huo unaojulikana kwa jina la " Prisoner " unaweza ukaunganisha matukio yaliyosemwa na Daz baba katika wimbo wake wa " Elimu Dunia" maudhui yake yanamfanano kabisa na lycris za msanii luck dube kwenye wimbo wake wa "prisoner"
Hukusikia la "Muadhini"(Anaeita adhana) wala la "Mnadi Swala"(anaeinadi swala kuashiria muda wa ibada umefika).
Ukwaju wa kitambo
0767 542 202
Tuwekane sawa hapo ni msanii Afande sele akiwa na shabiki yake na sio Daz baba..
Andiko lililopita la msanii "Pablo " lilileta usumbufu wa uwepo wa maswali & lawama nyingi kwangu mwandishi...
Soma kwa makini andiko before ujacoment