Wimbi la watu kuomba nauli

Wimbi la watu kuomba nauli

Mwanakulipata

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2018
Posts
718
Reaction score
1,202
Habari ya weekend. Katika pita pita zangu hapa jijini Dar haswa maeneo ya centre, nimekuja kushtukia naombwa nauli na watu tofauti tofauti tena waweza kuta unaombwa mara mbili kwa siku moja.

“Samahani kaka nimetokea Kigogo nilikuwa naomba nauli niweze kurudi nyumbani, maana hapa nimepoteza nauli ya kurudi” hii ndo gia anayokuja nayo.

Hivi inawezekanaje watu wengi wapoteze nauli kwa wakati mmoja, na kama wanapoteza, mbona sisi hatuokoti hizo hela wanazopoteza. Au kuna mtu kashawahi kuokota hela stend?

Bila shaka huu ni usanii na sasa hivi ni kuwaepuka vikali.
 
We toa kwani ni pesa ngapi? Si ni 1000 au 700 unahisi utapungukiwa nini? Mi natoaga kama kanitapeli atajua yeye mi nasonga na yangu.

Mbona sometimes nakua bar halafu napigwa mzinga wa bia ya 3000+ na totally stranger na nampatia kiroho safi.

So hata ukiwa sober do the same
 
We toa kwani ni pesa ngapi? Si ni 1000 au 700 unahisi utapungukiwa nn? Mi natoaga kama kanitapeli atajua yy mi nasonga na yangu.

Mbona sometimes nakua bar halafu napigwa mzinga wa bia ya 3000 na totally stranger na nampatia kiroho safi.

So hata ukiwa sober so the same.
Ngoja siku nitaenda nae hadi kwa konda nimlipie nauli nione...maana sipendi uongo
 
Sio kupungukiwa mkuu, ni kukosa kabisa.. mtu katoka Mbagala huko kaenda Makumbusho, Masaki Posta ama Kariakoo kutafuta riziki(kazi), Ila unakuta mpaka mida inatembea hajala na hajapata chochote anaamua wacha nirudi, sasa na namna jua la Dar hvi linavyochoma anaamua kujipa hopes kua "Good people are still there, so let me try" huenda akapata atleast nauli ya kurudia.

Mtu kutumia kauli ya kupungukiwa ni namna ya kupunguza kulia shida zake kua "sina kitu" maana ukisikia hvo utaanza kuwaza hajala n.k, naamini sio kwamba wanapenda ni shida tu!.

Pia, wapo ambao yeye kazi yake ni kuomba hvo kila siku, hawa ndio tatizo.

So all in all, kama una uwezo muda huo, wewr msaidie tu alafu endelea na shughuli zako, kama huwezi ama hutaki mwambie tu "pole sana, sina kitu"

Tuzingatie kauli ya " TENDA WEMA, NENDA ZAKO" ukiwa una deal na situation kama hizi.
 
Hao ndiyo pia wazimu wetu ukitupanda wanatakiwa kutoa mchango wa buku 10 ujenzi wa mashule.

Waoneeni imani waja hawa wa mola kwa hakika mnawakwaza mno!
 
Dah mkuu ndio umekuja kunianika huku, sirudii tena 😀 😀
 
Mimi kuna teja aliniomba nimsaidie hela ya kula nikampa 2000 akashukuru na kuondoka, nikashangaa mbona hali hapahapa ninapokula nikajua labda ana chimbo lake anawekewa "wali wa kushiba" na bei nafuu. Nikaambiwa ni teja ile hela atanunulia bangi na Banana za kupima.

Mwingine nilitoka chuo akaniomba hela anachechemea, ana ukurutu na anadai amefanyiwa operation ya tezi dume (wanawake wanawaomba ke wenzao wakidai wana kansa ya kizazi, me wanaomba wenzao kuwa wana tezi dume). Nikampa 2000 ila kesho yake nikamkuta nje ya ghetto ameshika energy drink anatembea vizuri, hana ukurutu kumbe ilikuwa rangi amepaka. Nikajiona mjinga

Mwingine pale Segerea aliomba nauli nikampa kisha jioni akaniomba tena nikamwambia nishampa akatembea
 
Haya mambo yanaudhi sana.
Dodoma, niliombwa nauli na kipofu kabisa ni kipofu sio anaigiza, nikampa elfu 2 akaita bodaboda ampeleke bar akanywe pombe za kienyeji.
Niliumia sana japo elfu 2 sio hela nyingi ila kwangu niliona kama dharau kubwa. Siji kumpa hela ombaomba wa Dodoma hasa wakazi wa mkoa wa Dodoma watu wa hovyo sana.
 
Hawa watu wengi wao wanakua hawana shida ya nauli wanatumia nafasi hiyo kujipatia kipato.mm nlimpea jamaa mmoja nauli maeneo ya standi ya mwl nyerere pale mikocheni nikaja kutana nae tena maeneo hayo uzuri mm huwa simsahau mtu hata ipite miezi miwili nlimkataaa.
 
Habari ya weekend.. Katika pita pita zangu hapa jijini Dar haswa maeneo ya centre..nimekuja kushtukia naombwa nauli na watu tofauti tofauti tena waweza kuta unaombwa mara mbili kwa siku moja.

“Samahani kaka nimetokea Kigogo nilikuwa naomba nauli niweze kurudi nyumbani, maana hapa nimepoteza nauli ya kurudi” hii ndo gia anayokuja nayo...

Hivi inawezekanaja watu wengi wapoteze nauli kwa wakati mmoja..na kama wanapoteza mbona sisi hatuokoti hizo hela wanazopoteza..au kuna mtu kashawahi kuokota hela stend?

Bila shaka huu ni usanii na sasahivi ni kuwaepuka vikali..
Mbona nimeshakutana nao mara nyingi. ila chakufanya ndo kumwambia muuongozane pamoja kuelekea kituo cha Daladala anachotaka kupakia . Akikuanzishia "Elfu Layla" njiani na ww una mwacha ktk ya mataa unaendelea na safari zako nyegine. ... Usikusudie kufanya wema kisha unaendelea kujiuliza maswali bila majibu.
 
Ipo sana na si city centre tu hata moja nimekutana nayo juzi tu on ma way from tanga line bunt anajidai kusema ooh... nitashushwa njiani, nikamuuliza kwa nini? Eti nauli imekata... pumbaf!

Nilihama ile seat nilichokiona ni kweli wizi. Binti kashuka pale mi nimeshuka na tukapanda tena gari moja kuelekea tulikoenda na akalipa nauli.

Hao wapo sana tu
 
Sio kupungukiwa mkuu, ni kukosa kabisa.. mtu katoka Mbagala huko kaenda Makumbusho, Masaki Posta ama Kariakoo kutafuta riziki(kazi), Ila unakuta mpaka mida inatembea hajala na hajapata chochote anaamua wacha nirudi, sasa na namna jua la Dar hvi linavyochoma anaamua kujipa hopes kua "Good people are still there, so let me try" huenda akapata atleast nauli ya kurudia.

Mtu kutumia kauli ya kupungukiwa ni namna ya kupunguza kulia shida zake kua "sina kitu" maana ukisikia hvo utaanza kuwaza hajala n.k, naamini sio kwamba wanapenda ni shida tu!.

Pia, wapo ambao yeye kazi yake ni kuomba hvo kila siku, hawa ndio tatizo.

So all in all, kama una uwezo muda huo, wewr msaidie tu alafu endelea na shughuli zako, kama huwezi ama hutaki mwambie tu "pole sana, sina kitu"

Tuzingatie kauli ya " TENDA WEMA, NENDA ZAKO" ukiwa una deal na situation kama hizi.
Mkuu huu ni usanii...haiwezekani naombwa nauli na watu watatu kwa siku moja tena wanadai wamepoteza nauli...

Na kama anaomba omba ili apate ridhiki... Inakuaje mtu mzima hana ugonjwa wowote ule aombe hela... Kuna vilema wanapiga chepe huko nishawahi fanya kazi na kilema amekatika vidole anavidole viwili tu lakin anapiga saidia fundi...

Kwanini adanganye kwanza amepoteza nauli?
 
Mkuu huu ni usanii...haiwezekani naombwa nauli na watu watatu kwa siku moja tena wanadai wamepoteza nauli...

Na kama anaomba omba ili apate ridhiki... Inakuaje mtu mzima hana ugonjwa wowote ule aombe hela... Kuna vilema wanapiga chepe huko nishawahi fanya kazi na kilema amekatika vidole anavidole viwili tu lakin anapiga saidia fundi...

Kwanini adanganye kwanza amepoteza nauli?
Always pray and be thankful for where u are!.. kuna baadhi ya watu hata humu wamepitia changamoto nyingi sana... kuna wakati mtu unaishiwa akiba yako una njaa kali sana umetafuta kibarua chochote hta cha kubeba mizigo umekosa.. mbaya zaidi kuna watu kama mimi tunaweza kufa tunajiona maana swala la kuomba kwangu ni mtihani mkubwa sana, wanaoshindwa kuvumilia ndo hao..

Pia nilisema kuna watu ambao wameigeuza kua ni tabia, i think unaowazungumzia ni hao.

NB. Do not generalize, Since "All generalizations are wrong, possibly including this one".
 
Back
Top Bottom