Will a weakened America emerge victorious against communist China?

Huu mjadala kuhusu "weakened America" sanjari na mijadala mingine inayofanana na huu haijaanza leo. Wamarekani na wasomi/wanazuoni mashuhuri wakiwemo kina Samuel Huntington walikuwa wakijadili kuhusu "kudhoofika kwa Marekani" tangu miaka ya 50. Kama mitandao ya kijamii ingekuwepo kuanzia kipindi hicho ikiwemo JamiiForums yetu, ni dhahiri nasi tungekuwa tumekwisha jadili humu muda mrefu sana kuhusiana na suala hili.

Mjadala huu umekuwa sasa kama utamaduni wa mara kwa mara wa Wamarekani. Tangu kipindi cha uimara wa Umoja wa Kisovieti (USSR) uliochochea mapinduzi makubwa ya kiyasayansi zikiwemo operesheni mbalimbali za anga za mbali, kuwepo kwa migogoro mbalimbali ukiwemo ule wa mafuta wa mwaka 73 pamoja na kuwepo kwa vita mbalimbali zilizoihusisha Marekani tangu miaka ya 50, mjadala huu na mingine inayofanana na huu imekuwa ikishamiri.

Katika kipindi chote hicho, wanazuoni walikuwa wakiutazama mwenendo wa utawala wa Marekani katika masuala mbalimbali ya kidunia na kuilinganisha nchi hiyo na mataifa mengine duniani. Leo hii tunaizungumzia China kama mpinzani mkuu wa Marekani katika masuala mbalimbali ya kidunia. Lakini, kipindi cha miaka ya 50 mpaka miaka ya 70 mwishoni, Umoja wa Kisovieti ama USSR ndiyo nchi iliyokuwa akitazamwa kama mpinzani mkuu atakaye pelekea "anguko la Marekani" kwa miaka kadhaa ijayo.

Baada ya USSR kuanza kudhoofika miaka ya 80, wasomi wetu haohao wakahamia kwa Mjapani na kumtaja kama mpinzani mkuu wa Marekani katika masuala mbalimbali hasa kiuchumi. Wasomi, kina Stanley Hoffmann na wengineo walikuwa miongoni mwa wapinzani wakubwa sana wa sera za Marekani miaka ya 80 na walituambia kuhusu habari hiihii ya "anguko la Marekani" huku wakilitumia anguko la USSR kama mfano. Mwaka 1990 na kuendelea, Japan ikaangukia katika mgogoro wa kiuchumi, habari ya Japan ikaishia hapo.

Hivi sasa, wasomi wetu wamehamia kwa Mchina. China sasa inatajwa kama mpinzani mkuu wa Marekani katika muktadha uleule wa kina Japan pamoja na USSR.

Ninachotaka kusema ni kuwa, mjadala huu si jambo geni. Umekuwa ni mjadala wa kujirudia kila baada ya wakati fulani. Wasomi wa miaka ya 50 waliujadili, wasomi wa miaka ya 70-80 wakauendeleza mjadala. Na hivi sasa, wasomi wa miaka hii nao wanajadili kitu kilekile na huenda mjadala ukaendelezwa na wasomi wa miongo kadhaa ijayo na kuendelea. Who knows! Lakini kama ni suala la "weakened America to emerge victorious against communist China" ama kinyume na hapo, muda utatupatia majibu sahihi. Tofauti na hapo, acha tuendelee tu kuuendeleza mjadala.

Asante!
You nailed it man....
 
Unaelewa kwanza kwa nini Dollar ya Marekani ndio currency inayotumika zaidi katika biashara ya kimataifa ?

Hayo mataifa makubwa yatakapoacha kutumia dola ya Marekani yatatumia sarafu gani mbadala ambayo itakubaliwa mara moja tu na mataifa yote?

Unafahamu biashara kubwa ya kimataifa ni kati ya makampuni binafsi yaliyoko nchi tofauti na sio biashara kati ya serikali? Hayo mataifa makubwa yatayaambia makampuni binafsi pia yaachane na matumizi ya dollar?

Hifadhi ya nchi(reserves) ambazo nyingi ziko kwenye dola ya Marekani zitafanywaje na hizo nchi? Watakubali kuzipoteza zote?

Hili swali la itakuaje mataifa makubwa yakiacha kutumia dola ya Marekani halina mashiko au ni "moot" ndio maana hakuna wenye akili wanaopoteza muda wao kulijibu.
Uko sahihi kabisa lakini kitu kimoja ambacho nadhani unasahau kukisema kwa hayo mataifa yote ambayo yaliwahi kulinganishwa na Marekani: Ujerumani Magharibi, Umoja wa Kisovieti na Japan hazijawahi kuwa na uchumi mkubwa kuliko Marekani wala kumshinda nguvu ya soko. Umoja wa kisovieti katika ubora wake miaka ya 60's ilikuwa ni asilimia 30 hadi 40 ya GDP ya Marekani. Marekani alikuwa bora katika GDP, PPP na muuzaji mkubwa wa bidhaa na huduma.

Sasa tukichambua uchumi na historia, Marekani alikuwa taifa lenye nguvu duniani kiuchumi mwaka 1872 baada ya kuwa na PPP kubwa kuliko mataifa yote duniani. Hadi kufika mwaka 1900 PPP ikamuwezesha Marekani kuwa taifa lenye uchumi imara kuliko yote. Mwaka 2009 Uchina ndiyo likawa taifa lenye PPP kubwa kuliko Marekani, sasa nadhani tukizungumza Uchumi, PPP huleta faida kibao kwa taifa lolote duniani lile linalofuata mfumo wa soko huru.

Kingine ni kwamba Japan, USSR na Ujerumani Magharibi hayajawahi kuwa The Biggest Exporters of Merchandise hadi kuweza kumtishia Marekani. Mataifa ambayo yamewahi kushika hii nafasi ni Imperial Germany mwaka 1900 na Dola la Muingereza kabla ya 1900. Taifa linalokuwa tajiri kuliko yote duniani ni lile ambalo linauza bidhaa nyingi pamoja na huduma kuliko taifa jingine lolote lile duniani, Marekani imeshika nafasi hii tokea mwaka 1945. Mwaka 2014 IMF ikatangaza kwamba Uchina ndiyo The Greatest Exporter of Merchandise. Marekani amefika hapo alipo kwasababu ya soko lililojengwa kuanzia kipindi cha The Gilded Age na World Wars.

Nafurahi sana kwamba umewalete wakina Huntington na Hoffman: Sasa kama umesoma vizuri, matatizo haya yalianza na Charles De Gaulle baada ya Marekani kuachana na The Gold Standard na kuanza kutumia Fiat Money. Watu kama Charles De Gaulle wakasema kwamba Marekani imefilisika na utajiri wake wote umeisha: Wakina Huntington walifanya chambuzi wakizingatia hili.

Ukweli mchungu ni kwamba Marekani imefika miaka ya 80 ikiwa na hali mbaya sana kiuchumi na Ronald Raegan alikopa sana pesa kutoka taasisi za ndani na nchi za nje. Swali lao hawa wasomi wote ni hili: Siku mataifa makubwa yanaacha kutumia dollar (The Fiat Money) unadhani Marekani itapona ??? Swali hili halijatolewa majibu mpaka leo.

Hoja kubwa ya Graham T Allison, Kishore Mahbubani na Joseph Nye siyo The Decline of America kama wakina Huntington wanavyosema kwenye The Clash of Civilization, but rather The Relative Decline of America. Marekani anaweza kuwa na uchumi huu-huu ambao anao sasa lakini Uchina akiendelea kukua kwa kasi hii basi atakuwa na uchumi mkubwa mara mbili ya Marekani hadi kufika 2070. Suala zima la Relative Decline halikuguswa kabisa na Huntington wala Hoffman, kama kuna sehemu wamelizungumzia tuoneshane.

Ahsante sana.
 
Back
Top Bottom