startergear
JF-Expert Member
- Jun 2, 2015
- 712
- 956
Naomba nikiri kwa mara ya Kwanza nimeanza kuichukia JF baada ya kusoma hili bandiko,,,,,kwanza mimi ntaweka na refence kabisa, cha kwanza unatakiwa ujue China ndio nchi yenye uchumi mkubwa kwa sasa kwa mujibu wa IMF (IMF Admits China Has Overtaken The US As The World’s Largest Economy; But Why Is The Media Silent? )
kumvimbia marekani usifikiri ni ishu ya kitoto ni lazima uwe nae sawa au umemzidi
si kweli kwamba china haina conglomerates kubwa duniani, sema sio maarufu kama za west na nyingine ni kubwa kuliko hata za west, Alibaba, Huwawei hizo ni kampuni ndogondogo China, katika makampuni 10 makubwa zaidi duniani , matano yametoka china manne us na moja saudi arabia, kampuni la kwanza na la pili kwa ukubwa duniani yote yametoka china (https://www.forbes.com/global2000/#142b81a9335d )
soko la hisa halimaanishi kwamba uchumi wako ndio mkubwa kuliko mwingine, na wala soko la hisa sio kigezo cha uchumi wa nchi ndio maana China hilo jambo sio ishu sana, Makampuni mengi ya china wanaorodheshwa marekani lakini mwisho wa siku faida kubwa inaenda kwenye makampuni ya china na sio marekani! ndio maana kuna baadhi ya makampuni trump aliyatoa sokola hisa marekani
Suala ya yuan kutokutumika kimataifa huu ni mfumo ambao china wanautaka wenyewe na yuan hawataki ipande thamani kuliko dola kwasababu ya kuvutia uwekezaji wa moja kwa moja! ukiwa na dola mia ni rahisi kuwekeza China kuliko marekani! dola 100 kwa marekani ni hela ya maji ya kunywa tu lakini ukiwa china hiyo hela unaweza fanyia mengi sana! Ndio maana mpaka kesho china hawezi pandisha thamani ya yuan ili kuvutia watu na marekani hua analalamika sana kila siku juu ya hili lakini hawez fanya lolote,mpaka kampuni kama telsa na apple kuwekeza china ndo ujiulize
China ni mtengeneza silaha mzuri tu, ila sio muuzaji silaha kila nchi na strategy yake, china, india na urusi ndo nchi pekee zina hypersonic missiles mpaka sasa hata hao marekani na israeli hawana ! china ina jeshi kubwa kuliko nchi yoyote duniani (29 Largest Armies In The World) , China ndo nchi yenye jeshi la majini kubwa kuliko nchi yoyote
(China Has The World’s Largest Navy. And It’s Getting Better, Pentagon Warns )
china ndo nchi inaoongoza kwa matumizi ya artificial intelligence duniani (China Leads in Practical AI | Enterprise IT News) na kampuni zinazojihusisha na AI ni nyingi China kuliko marekani
Kwa mara ya kwanza china imeipita marekani kwa mauzo ya filamu duniani (In 2020, China Surpassed America In Box Office Revenue ) china haiitaji hollywood tena bali hollywood ndo inahitaji china kwa sasa
kwenye cyber security china wapo vizuri sanaaa, waliwaibia NSA pentagon silaha ya kufanyia hacking (Chinese spies stole NSA hacking tools, report finds) na wakaitumia kuwa hack wao wenyewe kwa miaka kadhaa bila kushtukiwa, kwenye cyber securty China na Urusi wapo vizuri sana kuliko unavyofikiri
suala la vita , experience na vifaa kwenye vita vina advantage ndogo sana, marekani alipigwa na kataifa kadogo sana ( vietnam)lenye silaha duni sana na bila experience yoyote mpaka akakimbia akarudi kwako! vita ni teknik bana sio silaha wala experience! unaweza pigana vita miaka 20 mfululizo lakini ukaja kupigwa na mtu ambae hakuwahi kunyanyua hata jiwe maishani mwake! hakuna siku marekani atamvamia na kumpiga mchina, america hana uwezo huo hata china hawezi piga marekani! hizi nchi kamwe haziwez kuingia vitani kwasababu hakutakua na mshindi kati yao