Wilaya mpya ya Kisesa-Mwanza

Wilaya mpya ya Kisesa-Mwanza

Misungwi kunyang'anywa Usagara ni kuiua kabisa ila yote heri Usagara haipaswi kubaki Misungwi tena. Its mordenized than Misungwi itself.
Ni sawa tu na Magu kunyanganywa Kisesa . Inapoteza zaidi

Odhis *
 
Wilaya ya Magu imenyang'anywa chanzo cha mapato! Itapumulia mashine!
Kweli ndugu yangu.Kitendo tu cha kuiondoa Lamadi na kuipeleka mkoa mpya wa Simiyu kilikuwa ni mauaji ya kikatili kwa Wilaya ya Magu. Sasa hii ya kuinyofoa Kisesa kutoka Magu ndo balaa zaidi. Magu kwisha kabisa!
 
mmmh kayenze ipo igombe kutoka igombe mpaka misungwi unapita nyamagana mbn Nyamagana haijaguswa?
Kayenze ipo ilemela Ina njia mbili ya igombe haitumiki Sana badala yake inayotumika kwa Sana hivi Sasa ni njia ya kisesa ambapo wanapiti centre ya Sese ndio kayenze. Daladala ni elfu mbili tu kutoka stendi ya kisesa.

Mitano tena
 
Misungwi kunyang'anywa Usagara ni kuiua kabisa ila yote heri Usagara haipaswi kubaki Misungwi tena. Its mordenized than Misungwi itself.
Majiji makubwa Duniani ili yaendelee kukua ni lazima kumega maeneo ya jirani /suburban ili nayo yawe sehemu ya hadhi ya Majiji hayo.
Hii usaidia sana kuinua pato la Majiji husika na kuchagiza maendeleo kwenye maeneo mengi hasa yatokanayo na kushamiri kwa sekta za kukuza uchumi.
 
Kuipata Wilaya ya Kisesa Jimbo la Usagara Imefanyika kama ifuatavyo.

Wilaya ya Misungwi imetoa Kata 04 yaani
1. Kata ya Idetemya
2. Kata ya Usagara
3. Kata ya Fella
4. Kata ya Kanyerere.

Wilaya ya Magu imetoa yaani
1. Kata ya Kisesa
2. Kata ya Bujora
3. Kata ya Bukandwe
4. Kata ya Bujashi
5. Kata ya Mwamanga
6. Kata ya Kongoro


Wilaya ya Ilemela imetoa kata 03 yaani
1. Kata ya Nyamhongolo
2. Kata ya Sangabuye
3. Kata ya Kayenze

Hizo ndizo kata zitakazo unda Wilaya ya Kisesa Jimbo la Usagara.
Makao Makuu yatakua Fera Patakapokua na Bandari ya SGR
 
Back
Top Bottom