Julieth Ms
Senior Member
- Nov 29, 2011
- 102
- 37
Jamani huyu wifi yangu amezidi dharau sana kaka angu anaumwa amelazwa Regency majirani zangu wamenisindikiza na wamemnunulia mgonjwa juice ya Azam box kubwa wifi yangu alivyo fika nakuona ile juice akauliza "nani ameleta uchafu huu yaani mnamletea mme wangu juice chafu hii mnataka ahalishe" heee si tukabaki tumeduwaa akabeba ile juice na kwenda kutupa kwenye dust bin imeniuma sana majirani zangu wameona aibu kwa kweli yaani inasikitisha ukurugenzi wake ndo unafanya adharau mpaka mali zinazo zalishwa hapa nchini? Mi nimempa jibu moja tu wifi si ungemsafirisha kaka akatibiwe ulaya avute hewa nzuri na anywe maji na juice nzuri? akanifyonya