Kinyarwanda na kirundi ni lugha hiyo hiyo na ni kweli inaingiliana na kiha (namaanisha lugha ya waha wa kigoma), ingawa sina uhakika na kihangaza ila sitashangaa after all watu wote wa eneo hilo ni jamii moja iliyotenganishwa na mipaka ya kikoloni, unaweza ukakuta influence za kinyarwanda/kirundi as far as kwa wanyambo.
Labda nikukumbushe kuwa Rwanda na burundi zilikuwa nchi moja chini ya mfalme wa kitutsi zilitenganishwa shortly after mapinduzi. Nchi zote mbili zina watutsi, wahutu na watwa kwa nearly uwiano ule ule..Ni sawa na leo udai kimasai cha Tanzania ni lugha tofauti na kimasai cha kenya kisa mpaka wa sirari! Kinachobadilika ni dialect, i.e matamshi, for example mtu wa Arusha akizungumza kiswahili, mtu wa Dar atamshtukia kuwa huyu ni wa mkoani. Vile vile Tofauti ya hii lugha ya Rwanda na burundi ni hiyo tu ya matamshi as one moves away from the border between them lakini its the same language, save for a few words ambazo zimeongezeka kutokana na ule utenganisho niliokukumbushia.