WhatsApp inapoteza sana muda

WhatsApp inapoteza sana muda

Hiyo mitandao inapoteza muda sana, ndio mana wachina wamepangiwa muda huko wakutumia Tiktok haha na app wametengeneza wenyewe,sie huku mtu hafanyi kazi muda wote yupo humo bora wale wanaopata hela kupitia hiyo mitandao atleast! Kuna Mzungu mmoja yupo kwenye late 20s nilikua namfatilia kipindi chake cha live, Kwenye mtandao mmoja wa lugha akawa anasema yeye anapenda kusoma vitabu sana anaweza akakaa wiki hajashika simu,,,nilichoka wakati huku mtu asipoiona simu yake dakika 2 anaweza akapekekwa ICU kwa presha hahahah!!!
 
Kwa kweli hali ni mbaya sana, Kuna mfanyakazi mwenzangu wakike muda wote toka anaingia kazini mpaka anapotoka jioni yeye anatizama video tiktok, Dah anashangaza sana.
 
Hoja yako iko too General na ina Fallacies nyingi tu halafu hukuushirikisha vyema Ubongo wako Uliolala kabla ya kuja na huu Upuuzi.

Ina maana umeshindwa tu kujua kuwa kuna Watu wengine kutokana na Soko la Ajira kuwepo sasa wameamua Kujiongeza na Kubuni Miradi ili wapate Vipato na uwepo Wao 24/7 huko katika hayo Makundi ya WhatsApp ndiyo Ajira yao na Kunawalipa?

Una Hoja ya Msingi mahala fulani, ila ulichosahau ni Kuichakata Kwanza Logically na Kuiwasilisha na badala yake umekuja fully na Kisununu ( Chuki ) kwa Watu walioko katika WhatsApp Groups utadhani Bando za Wao kuwepo huko huwa unawatolea Wewe.
Popoma unakula sana ban kwasababu unatumia lugha kali katika uwasilishaji wako.
 
Hyo mitandao ni ofisi za watu , siku hyo mitandao ikizima hata Kwa wiki moja tuu , hasara ya hapo haielezeki.....
 
Hilo ni tatizo lako binafsi kama hauna time management.

Wengine unaona muda wote wapo humo hujui kwamba ndio ofisini kwao, sasa shida ipo kwako unayewaiga watu.
Kwahyo watu kama Mshana Jr hapa JF Ni ofisini kwao?
 
Usiombe ule Ganja alafu ndo uingie mtandaoni unaweza cheka mpaka udanje, ni kwere.
 
Habarini ndugu zangu.

Nimefuatilia kwa muda mrefu bila mashaka, kwamba Watanzania wengi tumechanganyikiwa na WhatsApp kuanzia asubuhi, mchana hadi alfajiri!

Watu wana magroup mpaka 50. Akiamka asubuhi anaanza kuview status za watu wake karibu 300 huko. Bado hajachangia kwenye magroup.

Watu hawafanyi kazi maofisi kwa sababu ya WhatsApp. Ni changamoto sana.

Tumerogwa fulani hivi.
Kila kitu kina faida na hasara kulingana na jinsi utakavyokitumia.

Kuna watu wanaendesha shughuli zao za kujipatia riziki kupitia WhatsApp.
 
Wewe utakuwa muuza bando si bure 😳 😳 😳 😳 😳
Walaa. Akili yako 'Mgando' ndiyo imewaza na kufikia ukomo wake hapo.

Ofisi nyingi siku hizi zitatumia internet kwa njia ya Fiber, Vodacom SupaKasi, ADSL TTCL na makolokolo mengine ya WiFi ambapo wafanyakazi wengi huona kama ni Bundle za bure kumbe Akili zao Utopolo tu kama wewe. Na ndiyo sababu hujikuta wakikeshea Mtandaoni kwa Mambo yasiyo na msingi wakidhani wanaikomesha kumbe wanajiumiza kwa kuzidi kurudi nyuma kimaendeleo kila leo.

Imagine: Kampuni ina Mkataba wa kuunganishiwa 100GB ya Fiber au Vodacom SupaKasi every month for a year alafu wewe na Tiktok yako sijui YouTube unataka kuimaliza. ITAKUULIA HAPO!!

Sasa narudia tena kukuuliza kwa mara ya pili, WEWE INAKUUMA NINI!!!?? Mfyuuu
 
Back
Top Bottom