DALA
JF-Expert Member
- Aug 24, 2009
- 2,259
- 4,691
Amani iwe kwenu!
Najiuliza tu kama binadamu wa kawaida. Kule Afrika ya kusini ilitokea, kabla ya Nelson Mandela kuachiwa huru hadharani kulikuwa na mchakato uliopelekea yeye kuachiwa.
Watu kama Oliver Tambo na wapinagaji wengine waliokuwa nje hawakujua kwamba tayari Mandela alikuwa na majadiliano na Botha wakati ule na sehemu kubwa ya mjadala ulishafikia hatua ya makubaliano.
Mandela alitolewa kule Robben Island alipokuwa anatumikia kifungo chake na kupewa nyumba Cape Town ambapo alihudumiwa kifalme chini ya ulinzi mkali.
Kutoka pale, aliweza kwenda kwenye majadiliano kisirisiri na kupokea wageni kutoka upande wa serikali waliokuwa na kazi ya kufanya majadiliano juu ya mustakabali wa wazungu na mali zao pindi Mandela atakapoachiwa huru.
Ikumbukwe kwamba Mandela alifungwa muda mrefu hivyo wapiganaji kama Oliver Tambo ndo walikuwa na ufahamu wa hali halisi ya mapambano na serikali iliogopa kwamba wangepewa kina Tambo madaraka, makaburu wangekiona cha moto hivyo ilikuwa rahisi kujadiliana na Mandela ambaye kwa wakati ule, alishapondeka hasa na kukosa matumaini.
Kwake ile ilikuwa ni a second chance hivyo alikuwa tayari kuachia uchumi mikononi mwa makaburu huku yeye akishikilia bendera na kuwashashiwi weusi kuwasamehe makaburu.
Pamoja na kwamba ni jambo jema, ila bado najiuliza ile haraka ya Freeman Mbowe kwenda ikulu hata kabla ya kutulia angalau?
Sina uhakika kama alipata hata nafasi ya kushauriana na viongozi wa chama chake kwa ukaribu kujua hali halisi na kujenga msimamo wa pamoja?
Kwanini alienda peke yake?
Sina maana ya kwamba simuamini ila kwenye siasa hakuna ajali.
Hivyo najiuliza tu.
Naomba muongozo.
Najiuliza tu kama binadamu wa kawaida. Kule Afrika ya kusini ilitokea, kabla ya Nelson Mandela kuachiwa huru hadharani kulikuwa na mchakato uliopelekea yeye kuachiwa.
Watu kama Oliver Tambo na wapinagaji wengine waliokuwa nje hawakujua kwamba tayari Mandela alikuwa na majadiliano na Botha wakati ule na sehemu kubwa ya mjadala ulishafikia hatua ya makubaliano.
Mandela alitolewa kule Robben Island alipokuwa anatumikia kifungo chake na kupewa nyumba Cape Town ambapo alihudumiwa kifalme chini ya ulinzi mkali.
Kutoka pale, aliweza kwenda kwenye majadiliano kisirisiri na kupokea wageni kutoka upande wa serikali waliokuwa na kazi ya kufanya majadiliano juu ya mustakabali wa wazungu na mali zao pindi Mandela atakapoachiwa huru.
Ikumbukwe kwamba Mandela alifungwa muda mrefu hivyo wapiganaji kama Oliver Tambo ndo walikuwa na ufahamu wa hali halisi ya mapambano na serikali iliogopa kwamba wangepewa kina Tambo madaraka, makaburu wangekiona cha moto hivyo ilikuwa rahisi kujadiliana na Mandela ambaye kwa wakati ule, alishapondeka hasa na kukosa matumaini.
Kwake ile ilikuwa ni a second chance hivyo alikuwa tayari kuachia uchumi mikononi mwa makaburu huku yeye akishikilia bendera na kuwashashiwi weusi kuwasamehe makaburu.
Pamoja na kwamba ni jambo jema, ila bado najiuliza ile haraka ya Freeman Mbowe kwenda ikulu hata kabla ya kutulia angalau?
Sina uhakika kama alipata hata nafasi ya kushauriana na viongozi wa chama chake kwa ukaribu kujua hali halisi na kujenga msimamo wa pamoja?
Kwanini alienda peke yake?
Sina maana ya kwamba simuamini ila kwenye siasa hakuna ajali.
Hivyo najiuliza tu.
Naomba muongozo.