Pole sana mumy ni mpito tu katika ndoa,huwa inatokea kuna vipindi tofauti tofauti. Mimi binafsi nionavyo katika kesi yako tatizo Lipo kwenye ubongo wako kiasi linaathiri mfumo mzima wa mwili wako.
Kikubwa umeyapa maisha kipaumbele zaidi kuliko sexy life, haupo happy na hali ya sasa mnayoishi, unatamani uende mbele zaidi na zaidi,moyo wako wote na akili yako yote ni kuwa na maisha fulani uyatakayo na sometimes unaona mambo hayaendi sawa kiasi kwamba inakuchanganya huoni lingine zaidi ya kutimiza ndoto zako.
Nini basi la kufanya? Jambo la kwanza be content with what you have,appreciate the way you are, badilisha namna unavyofikiri ili uweke kubadilika namna unavyoishi. Elewa kila jambo na wakati kuna wakati unahitaji kuwaza maisha na mambo yake na kuna wakati unabidi mwili uupe haki yake.
Jambo lingine usiwe mbinafsi kupitiliza, elewa nafasi ya mume wako katika maisha yako,labda nikuambie tu asilimia kubwa ya wanaume ni wazito sana kukubali ushauri wa mkewe katika swala la maendeleo,lazima aupitishe kwenye chekecheo lake mpka ajiridhishe kwamba hili linafaa wakati mwingine huchukua muda,huwa hawatuamni sana kwenye maamuzi/maoni yetu mpaka wastuck mahali ndo anakuja tena kwako kuomba ushauri. So inabidi uende naye taratibu kumuaminisha ndoto ulizonazo wapi unapataka,na hili husindikizwa na moyo wa upendo na hali ya kuwa karibu naye zaidi katika mapenzi mazito,ataziaminije ndoto zako ilihali haupo karibu naye?
Kuwa karibu zaidi na mume wako na huko ndiko feelings zitakuja na katika huo ukaribu ndiko tunakoshirikishana mambo yetu,mfano kutembea pamoja,kula pamoja,kuoga pamoja n.k, katika hali hiyo ndipo mabussiness idea yanaposhukaga,maplan ya kufa mtu yanapotokeaga,ndiko the happiest moment you can explain what you have.
Neno la Mungu linatuambia wawili ni afadhali kuliko Mmoja, hayo yote uyatamaniyo yatakuwa ni smooth iwapo utakuwa karibu zaidi na mume wako,utashangaa hutaamini, jua huyo unayeishi naye ni mtu muhimu sana kwa maisha yako ni life partner wako,Mpe uthamani wa hali ya juu,ni kila kitu katika yote uyahitajiayo,kama kuna tofauti tafadhali rekebisha tofauti hizo na ufurahie sexy life,katika ndoa sexy life inapokuwa nzuri hata maendeleo ya kiuchumi yanaponawiri zaid. Mshirikishe Mungu katika yote atakuwezesha yeye ni mkuu katika yote.