Wezi wa mtandao wanaswa Buguruni

Wezi wa mtandao wanaswa Buguruni

Abdull Kazi

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2012
Posts
344
Reaction score
306
watu watatu akiwemo miongoni mwao akiwamo mwanamke mmoja wamenaswa muda huu ktk eneo la buguruni wakituhumiwa kuendesha wizi wa mtandao.

mbinu wanazodaiwa kutumia ni kuwafuatilia watu wanaoweka fedha ktk simu kwa kujua namba zao za simu na jina kisha hutengeneza kitambulisho cha chenye jina la muhusika na kwenda kurenew line hiyo.

inadaiwa leo ni mara ya pili kutaka wapatiwe line ya namba ambayo mwanzo walifanikiwa kutoa hela za mtu ambaye aliidai kampuni ya tigo.
 
Sasa namba ya siri wanaipataje?
Na watarenew vipi wakati original line bado inakuwa hewani?
 
Sasa namba ya siri wanaipataje?
Na watarenew vipi wakati original line bado inakuwa hewani?

namba yoyote uki-renew ile ya awali ina-scrumble immediately, ila namba ya siri ndo sijui wanafanyaje lakini katika technology lolote linawezekana. kama software za waisrael hamna ambapo wanashindwa kuingia na kama a wangekuwa wezi hakuna technology yoyote ya kuwazuia kuingia katika mfumo wowote. kama yule jamaa aliuawa kule dubai mpalestina Mahmoud_Al-Mabhouh‎ jamaa waliingia kwenye mfumo kielectronic wa hotel wa kufungulia milango wakamalizia chumbani kwake
 
hujajibu swali ndugu, inaelekea umekurupuka kuuleta huu uzi hapa bila kukusanya taarifa sahihi za kutosha,. Unapo renew line lazima uonyeshe kitambulisho chenye taarifa zako za kweli na utaulizwa leseni ya udereva, kadi ya kupigia kura n.k ! Watakachofanya kampuni ya simu husika ni kujaribu kufananisha hizi taarifa zako na zile zako za awali ndipo wakutatulie tatizo lako,. Pili lazima uandike angalau namba tano za simu ulizowasiliana nazo mara ya mwisho,. Tatu huwezi kupewa namba yako ya siri na kama ukitaka kuibalisha ya mwanzo huna budi kuingiza ile ya awali! Sijua kama utachomoka hapa,. Wengi wamejaribu wamekwama maana siyo rahisi kama watu wachache wanavyowaza kama wewe mleta mada,..
 
Buguruni kumekuwa na vijiwe vya kufanyia mipango ya uharifu na polisi wanajua na wanalinda vijiwe hivyo.
Kijiwe maarufu kinaitwa kwa Zero. Pale kwa Zero ni barabarani tu, hakuna choo, jiko la kupikia wala sehemu maalum ya kukaa wateja.
Sehemu hiyo hufunguliwa kila siku usiku tu na kukesha mpaka alfajiri kama vile night club.
Pale pamekuwa kijiwe maarufu cha kupanga uhalifu na pahala pekee pa kujipatia huduma muhimu kama bangi, unga, madada poa na mabwabwa.
Polisi kituo kikuu cha Buguruni kipo mita mbili tu kutokea pale lakini wala hawajishugulishi na uhalifu unaopangiwa pale.
Hii mipango yote kama ya hawa mabwana waliokamatwa huwa inapangiwa palepale huku wakijiliwaza kwa kiroba na mrungi na bangi mpaka kunapambazuka wanaanza kuwashambulia wapita njia hasa waki na mama wanaodamkia kwenye mihanjo yao na kuwanyanganya pochi na simu zao.
Polisi hivi intelijensia yenu ni kuzuia maandamano ya wapinzani tu?
Siku zote kumbuka "prevention is much better than cure"
 
namba yoyote uki-renew ile ya awali ina-scrumble immediately, ila namba ya siri ndo sijui wanafanyaje lakini katika technology lolote linawezekana. kama software za waisrael hamna ambapo wanashindwa kuingia na kama a wangekuwa wezi hakuna technology yoyote ya kuwazuia kuingia katika mfumo wowote. kama yule jamaa aliuawa kule dubai mpalestina Mahmoud_Al-Mabhouh‎ jamaa waliingia kwenye mfumo kielectronic wa hotel wa kufungulia milango wakamalizia chumbani kwake
Hiyo kazi ni ya Mossad tu wengine hawawezi
 
Buguruni kumekuwa na vijiwe vya kufanyia mipango ya uharifu na polisi wanajua na wanalinda vijiwe hivyo.
Kijiwe maarufu kinaitwa kwa Zero. Pale kwa Zero ni barabarani tu, hakuna choo, jiko la kupikia wala sehemu maalum ya kukaa wateja.
Sehemu hiyo hufunguliwa kila siku usiku tu na kukesha mpaka alfajiri kama vile night club.
Pale pamekuwa kijiwe maarufu cha kupanga uhalifu na pahala pekee pa kujipatia huduma muhimu kama bangi, unga, madada poa na mabwabwa.
Polisi kituo kikuu cha Buguruni kipo mita mbili tu kutokea pale lakini wala hawajishugulishi na uhalifu unaopangiwa pale.
Hii mipango yote kama ya hawa mabwana waliokamatwa huwa inapangiwa palepale huku wakijiliwaza kwa kiroba na mrungi na bangi mpaka kunapambazuka wanaanza kuwashambulia wapita njia hasa waki na mama wanaodamkia kwenye mihanjo yao na kuwanyanganya pochi na simu zao.
Polisi hivi intelijensia yenu ni kuzuia maandamano ya wapinzani tu?
Siku zote kumbuka "prevention is much better than cure"

Kmanda Kova uko wapi katika hili pamoja na intelijensia yako?
 
washazoe hao kuwaibia wateja wao. na ndo maana jamaa wa kitengo cha tigo pesa wanzidi kuwa wanene kila siku iendayo kwa mola kutokana na michezo ya kib wege------- kama hii.
 
Back
Top Bottom