Natamani hata tungekuwa na jina jingine linalomwelezea kali zaidi kuliko hili. His government is the most hopeless ever na yeye anaonekana hata hajali. Imefika mahali binafsi sielewi kazi ya serikali ni nini na kwanini tuendelee kulipa kodi kwani barabara zimejaa potholes (hapa Dar), hospitalini hakuna dawa na mama wajawazito wanajifungulia sakafuni, shule hazina waalimu wala madawati (nina uncle anasoma std 4 hapa dar, juzi nimegombana naye how come bag limechoka ndani ya mwezi mmoja akanieleza kumbe hilo ndio dawati lake, anakaa chini na kuandika juu ya bag kama dawati). Shule nyingi za Dar ni std 6 na 7 tu ndio wenye madawati. Nikiorodhesha matatizo hapa sitayamaliza lakini tuliowapa dhamana ya kutuongoza wako poa wanaona hamna shida. Natamani tupate solution ya kudumu ili tusijeruhusu tena mtu asiye na uwezo kuwa rais bila kujali anatoka chama gani.