MKWEAMINAZI
JF-Expert Member
- May 28, 2023
- 930
- 1,299
Hakika nichukue nafasi hii kumpongeza Mwanasheria Mkuu Mstaafu wa Kenya kwa kuonesha uzalendo kwa nchi yake juu ya kutaka wabunge wa viti maalum wasiwepo ili kuwapunguzia mzigo wa kodi wananchi masikini wa Kenya.
Ni imani yangu hata serikali ya Tanzania inafaa kuiga suala hili kwa kuwaondoa wabunge Viti Maalum Bungeni kwani hawana tija yoyote kwa wenye nchi ambao ni wananchi masikini wa Tanzania.
Nimekuwa nashangaa sana kuona Bunge na Serikali ya Tanzania kuendelea kuwakumbatia wabunge 19 wasio na chama badala ya kuwafukuza ili kupunguza idadi ya wabunge viti maalum huku wakijua ni uvunjifu wa Katiba.
Wabunge hao ni batili kwani upatikanaji wao haukufuata utaratibu uliopo kisheria na ndio maana wakafukuzwa na chama chao lakini bado Bunge na Serikali linawalipa mishahara na posho ambazo ni kodi na matozo yanayolipwa na masikinini.
Wabunge wa viti maalum wafutwe kuokoa fedha za walipa kodi.
Ni imani yangu hata serikali ya Tanzania inafaa kuiga suala hili kwa kuwaondoa wabunge Viti Maalum Bungeni kwani hawana tija yoyote kwa wenye nchi ambao ni wananchi masikini wa Tanzania.
Nimekuwa nashangaa sana kuona Bunge na Serikali ya Tanzania kuendelea kuwakumbatia wabunge 19 wasio na chama badala ya kuwafukuza ili kupunguza idadi ya wabunge viti maalum huku wakijua ni uvunjifu wa Katiba.
Wabunge hao ni batili kwani upatikanaji wao haukufuata utaratibu uliopo kisheria na ndio maana wakafukuzwa na chama chao lakini bado Bunge na Serikali linawalipa mishahara na posho ambazo ni kodi na matozo yanayolipwa na masikinini.
Wabunge wa viti maalum wafutwe kuokoa fedha za walipa kodi.