Wenzake na Mwl. Nyerere waliohusika kupigania uhuru wa Tanganyika ni kina nani? Tuwape hadhi yao

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,620
46,260
Kila historia ya uhuru wa Tanganyika inapozungumzwa jina linalokaribia kumeza historia yote ni Julius Kambarage Nyerere(JKN). Ukimuondoa Nelson Mandela wa Afrika kusini hakuna kiongozi mpigania uhuru aliyetandaza kivuli chake kwa nchi yake kama Mwl. Nyerere.

JKN ameacha "legacy" kubwa na ndefu. Ameandikwa katika kila kitabu cha historia nchi hii, madaraja, majengo, viwanja vya ndege, mabwawa ya umeme, barabara, shule, vyuo n.k vimepewa jina lake. JKN amekuwa rejea ya uongozi nchi hii, ukimkosoa JKN unaonekana kama mhaini na wafahidhina wa nchi hii.

Tofauti na Afrika Kusini ya Nelson Mandela ambapo wapigania uhuru wake wengi wameendelea kutajwa mfano wa Oliver Thambo, Steve Biko, Chris Hani, Govan Mbeki n.k Tanganyika na baadaye Tanzania ya Nyerere jina kubwa la harakati za uhuru ni JKN, majina mengine yanasikika kwa mbali sana au yamepotea kabisa.

Sote tunafahamu Nyerere alikuwa na wenzake wengi katika kutafuta uhuru wa nchi hii. Tungependa kuwafahamu na kujua mchango wao kupitia maandishi ya historia rasmi rasmi za serikali. Pia wangetendewa haki kama majina yao yangeanza kupewa masoko, madaraja, barabara, viwanja vya michezo, ofisi za serikali zinazojengwa Dodoma n.k
 
Nyerere alitofautiana na wengi haswa kwa kushikilia siasa za ujamaa. Ila ujamaa pamoja na mtatatizo yake, umejenga jamii bora kabisa. Watu wenye kuishi kiundugu.
 
Nyerere alitofautiana na wengi haswa kwa kushikilia siasa za ujamaa. Ila ujamaa pamoja na mtatatizo yake, umejenga jamii bora kabisa. Watu wenye kuishi kiundugu.
Pamoja na kutofautiana katika siasa za ujamaa na ubepari mchango wao katika harakati za uhuru ni muhimu utambulike.
Pia tuko kwenye ubepari kwa sasa.
 
Pamoja na kutofautiana katika siasa za ujamaa na ubepari mchango wao katika harakati za uhuru ni muhimu utambulike.
Pia tuko kwenye ubepari kwa sasa.
Vipo vitabu vimeandikwa ipo mitaa imeitwa kwa heshima za hao watu, wengine mpaka leo, wajukuu zao wanaendelea kufaidi keki ya taifa
 
Vipo vitabu vimeandikwa ipo mitaa imeitwa kwa heshima za hao watu, wengine mpaka leo, wajukuu zao wanaendelea kufaidi keki ya taifa
Inapaswa iwe kama Oliver Tambo International Airport au Walter Sisulu University, majina ya mitaa ni jambo dogo sana wanalofanyiwa watu wengi wa kawaida, wapigani uhuru wanahitaji hadhi ya juu sawa na daraja lao.
 
Inapaswa iwe kama Oliver Tambo International Airport au Walter Sisulu University, majina ya mitaa ni jambo dogo sana wanalofanyiwa watu wengi wa kawaida, wapigani uhuru wanahitaji hadhi ya juu sawa na daraja lao.
Una kitu umeona hakiko sawa, ni jambo fikirishi, pia harakati za ukombozi wa taifa letu haukuwa kiviile. Hakuna mtu alishika bunduki, unaweza ukaelewa, ata harakati hazikua kama SA au kwingineko.
 
Nyerere alitofautiana na wengi haswa kwa kushikilia siasa za ujamaa. Ila ujamaa pamoja na mtatatizo yake, umejenga jamii bora kabisa. Watu wenye kuishi kiundugu.
Mbona watu waliishi kiundugu toka enzi za ukoloni? Makabila yalioana na kuzaliana kabla ya uhuru. Wahehe walioa Wagogo, Wazaramo walioa Wasukuma, n.k kwa muda mrefu tuu kabla ya Nyerere.

Alichofanya Nyerere ni kuliweka taifa pamoja lisisambaratike kikabila, kiukanda, kidini n.k. Hili kweli anastahili sifa maana nchi za Afrika ni nchi bandia.

Ni wakoloni tuu walichora mistari kwenye ramani wakaita nchi bila kujali makabila, dini, kanda, n.k. Kuziweka pamoja kama taifa ni ngumu. Ila alikosea pale alipovamia Zanzibar. Zanzibar haitaki kutawaliwa kwa kupitia muungano.
 
Tofauti na Afrika Kusini ya Nelson Mandela ambapo wapigania uhuru wake wengi wameendelea kutajwa mfano wa Oliver Thambo, Steve Biko, Chris Hani, Govan Mbeki n.k Tanganyika na baadaye Tanzania ya Nyerere jina kubwa la harakati za uhuru ni JKN, majina mengine yanasikika kwa mbali sana au yamepotea kabisa.
Nelson Mandela alipoachiwa huru nchi ya kwanza aliyoitembelea ni Tanzania kuja kumshukuru Mwalimu JUlius Kambarage Nyerere, je unajua sababu?

Nyerere alihusika sana tu katika ukombozi wa nchi nyingi za Kiafrika kusini mwa equator, Afrika Kusini ya Mandela ikiwa ni mojawapo.

1654322576730.png
1654322197296.png

Unaowaona pichani ni baadhi ya viongozi Kusini mwa Afrika waliomshukuru Nyerere
kwa mchango wake katika harakati zao za ukombozi.​
 
Back
Top Bottom