Mama na Mwana Wazalendo Wapigania Uhuru wa Tanganyika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,918
30,259
MAMA NA MWANA WAZALENDO WAPIGANIA UHURU WA TANGANYIKA

Huenda historia ya Bi. Mwamtoro bint Chuma na mwanae Haydar Mwinyimvua ikawa ndiyo historia ya pekee ya mama na mwana wote wawili na kwa pamoja walikuwa katika TANU mstari wa mbele wakipigania uhuru wa Tanganyika.

Nyumba ya Bi. Mwamtoro ilikuwa nyuma ya ofisi ya TANU ikawa Mwalimu Nyerere alipokuwa anataka kufanya mkutano wa ndani alikuwa akimuomba Bi. Mwamtoro avunje ua wake waunganishe na ua wa TANU ipatikane nafasi kubwa kwa wanachama kukusanyika mahali pamoja.

Hili lilikuwa likifanyika na kufanya nyumba ya Bi. Mwamtoro kuwa moja ya viwanja na ngome ya TANU katika kupambana na wakoloni.

Rashid Mfaume Kawawa alipata kusema kuwa endapo nyumba hii inataka kuuzwa basi asiuziwe yeyote ila chama cha TANU kwa kuwa TANU ina historia kubwa na nyumba hiyo.

Nyumba iko nyuma ya Ofisi Ndogo ya CCM.

Inasikitisha kuwa ni watu wachache sana hivi sasa wanajua historia ya nyumba hii na historia hii ya mama na mwana.

1701029675909.png

 
Tanzania history yake ipo kimagumashi sana. Kujulikana alie mwanzo lakini wengine nao pia wamo. Unaweza kuwa na watoto 10 lakini mtoto wako wa mwanzo akafanya uitwe mama Omari hawa 9 walobakia majina yao yanabaki nayo wenyewe.
 
Tanzania history yake ipo kimagumashi sana. Kujulikana alie mwanzo lakini wengine nao pia wamo. Unaweza kuwa na watoto 10 lakini mtoto wako wa mwanzo akafanya uitwe mama Omari hawa 9 walobakia majina yao yanabaki nayo wenyewe.
Killa...
Katika historia hii uliloliona ni hilo tu?
 
Tuletee historia ya wasafisha choo wa ofisi za tanu,mana sasa kila takataka unayoifahamu ilamradi ni mvaa kobazi aliayeishi hapo gerezani alikua mpigania uhuru.
 
Safi sana endelea kutuhabarisha/kutujulisha/kutuelimisha,

ijapokuwa wengi wetu (mimi nikiwa mmoja wao) tumeathiriwa na mitizamo ya kidini na kuona kuwa wengi wanaotajwa wapo katika upande mmoja wa kidini(sababu inaweza kuwa ni kukariri imani fulani na kawaida ya majina yake) lakini haiondoi ukweli wa yale yaliyotokea zama hizo hivyo kongole sana

wewe ni hazina hivyo hakikisha haya unayaweka sawa na itapendeza zaidi pia kama hizi taarifa ukiweka katika tovuti au blog kwa kumbukumbu zijazo.
 
Safi sana endelea kutuhabarisha/kutujulisha/kutuelimisha,

ijapokuwa wengi wetu (mimi nikiwa mmoja wao) tumeathiriwa na mitizamo ya kidini na kuona kuwa wengi wanaotajwa wapi katika upande mmoja wa kidini(sababu inaweza kuwa ni kukariri imani fulani na kawaida ya majina yake) lakini haiondoi ukweli wa yale yaliyotokea zama hizo hivyo kongole sana

wewe ni hazina hivyo hakikisha haya unayaweka sawa na itapendeza zaidi pia kama hizi taarifa ukiweka katika tovuti au blog kwa kumbukumbu zijazo.
Just...
Ingia:
mohamedsaidsalum.blogspot.com
 
1701056807728.png

Abdul Sykes anamwambia mdogo wake Abbas, ''Nyerere anasafiri kwenda UNO na lazima adungwe sindano (vaccination).

Mimi siwaamini hawa Waingereza wasije wakamdhuru.
Hakikisha kuwa Nyerere anapata ''vaccination certificate,'' lakini hapigwi sindano''

Hivi ndivyo ilivyokuwa.
Nyerere hakuchoma sindano.

Vaccination Certificate ilipatikana lakini Mwalimu hakupiga sindano na akasafari kwenda New York bila ya kuchanjwa.
 
Uhuru wa Tanganyika ulipiganiwa mwaka gani?
Wanajeshi wangapi walikufa?
Uzalendo...
TATIZO LA MAJINA YA KIISLAM KATIKA KUMBUKUMBU YA VITA VYA MAJI MAJI (1905 – 1907) MAHENGE SONGEA

Katika kumbukumbu ya Vita Vya Maji Maji Songea sehemu inayotia simanzi kubwa ni pale penye kaburi kubwa la halaiki walipozikwa wazalendo 67 walionyanyua silaha dhidi ya dhulma za Wajerumani.

Hawa walihukumiwa kunyongwa.

Kando ya kaburi hili la halaiki kuna kaburi moja lililo peke yake.

Hili ni kaburi la Abdulrauf Songea Mbano aliyenyongwa peke yake na kuzikwa kwenye kaburi la peke yake.

Hapo Mahenge ilikuwapo orodha ya majina ya wote walionyongwa na kuzikwa hapo.

Robo tatu ya walionyongwa na kuzikwa hapo ni Waislaam.

Lakini karatasi hii yenye majina ya Kiislam yamewekwa mbele yakifuatiwa katika mabano na majina mengine ambayo si ya Kiislam.

Linaanza jina lake la Kiiislam kisha lingine mfano Abdulrahman (Dominic) Mputa Gama.

Ingekuwa kama siku kuchomekwa jina lingine jina lingesomeka kama hivi, ‘’Abdulrahman Mputa Gama.’’

Kazi hii ilifanywa na padre kutoka Peramiho aliyeletwa Mahenge kuwabatiza Waislam kwa ahadi kwa kuwa wakikubali kubatizwa hawatanyongwa.

Orodha hii yenye majina ya Kiislam hivi sasa imeondolewa na badala yake kuna orodha mpya yenye majina mengine ambayo yanasomeka kwa mfano wa hapo juu, ‘’Dominic Mputa Gama,’’ badala ya ‘’Abdulrahman (Dominic) Mputa Gama.’’

Labda tujiulize nani anafanya haya nani anamtuma nini nia ya kufanya hivi?

Lipi lisilotakiwa lijulikane katika historia ya Vita Vya Maji Maji?
 
Uzalendo...
TATIZO LA MAJINA YA KIISLAM KATIKA KUMBUKUMBU YA VITA VYA MAJI MAJI (1905 – 1907) MAHENGE SONGEA

Katika kumbukumbu ya Vita Vya Maji Maji Songea sehemu inayotia simanzi kubwa ni pale penye kaburi kubwa la halaiki walipozikwa wazalendo 67 walionyanyua silaha dhidi ya dhulma za Wajerumani.

Hawa walihukumiwa kunyongwa.

Kando ya kaburi hili la halaiki kuna kaburi moja lililo peke yake.

Hili ni kaburi la Abdulrauf Songea Mbano aliyenyongwa peke yake na kuzikwa kwenye kaburi la peke yake.

Hapo Mahenge ilikuwapo orodha ya majina ya wote walionyongwa na kuzikwa hapo.

Robo tatu ya walionyongwa na kuzikwa hapo ni Waislaam.

Lakini karatasi hii yenye majina ya Kiislam yamewekwa mbele yakifuatiwa katika mabano na majina mengine ambayo si ya Kiislam.

Linaanza jina lake la Kiiislam kisha lingine mfano Abdulrahman (Dominic) Mputa Gama.

Ingekuwa kama siku kuchomekwa jina lingine jina lingesomeka kama hivi, ‘’Abdulrahman Mputa Gama.’’

Kazi hii ilifanywa na padre kutoka Peramiho aliyeletwa Mahenge kuwabatiza Waislam kwa ahadi kwa kuwa wakikubali kubatizwa hawatanyongwa.

Orodha hii yenye majina ya Kiislam hivi sasa imeondolewa na badala yake kuna orodha mpya yenye majina mengine ambayo yanasomeka kwa mfano wa hapo juu, ‘’Dominic Mputa Gama,’’ badala ya ‘’Abdulrahman (Dominic) Mputa Gama.’’

Labda tujiulize nani anafanya haya nani anamtuma nini nia ya kufanya hivi?

Lipi lisilotakiwa lijulikane katika historia ya Vita Vya Maji Maji?
Mimi nimeulizia takwimu za vita vya uhuru...
Vilikuwa mwaka gani?
Wanajeshi wangapi wa Tz walikufa?
Wanajeshi wangapi wa jeshi pinzani walikufa?
Au vita vilikuwa kwenye vijiwe vya kahawa?
 
Mimi nimeulizia takwimu za vita vya uhuru...
Vilikuwa mwaka gani?
Wanajeshi wangapi wa Tz walikufa?
Wanajeshi wangapi wa jeshi pinzani walikufa?
Au vita vilikuwa kwenye vijiwe vya kahawa?
Uzalendo...
Wewe umeleta kibri na dharau dhidi yangu.

Mimi nimekukumbusha wazalendo waliopigania uhuru wa nchi hii kwa kunyanyua silaha.

Mimi siwezi kukurejeshea jeuri kwa jeuri.
Haya hayana tija na huharibu mjadala.
 
Tuletee historia ya wasafisha choo wa ofisi za tanu,mana sasa kila takataka unayoifahamu ilamradi ni mvaa kobazi aliayeishi hapo gerezani alikua mpigania uhuru.
Wewe leta yako ya wavaa pedi na rozari acha kuvunjia watu wazima heshima kwenye nyuzi zao.
 
Mimi nimeulizia takwimu za vita vya uhuru...
Vilikuwa mwaka gani?
Wanajeshi wangapi wa Tz walikufa?
Wanajeshi wangapi wa jeshi pinzani walikufa?
Au vita vilikuwa kwenye vijiwe vya kahawa?
Ana usimuliaji tu wa kikasuku lakini hua hawezi jibu hoja, na mara zote hua anatafuta exit strategy kama hvo
 
Back
Top Bottom