Habarindiyohiyo
JF-Expert Member
- Aug 11, 2008
- 263
- 13
Wenyeviti 11 wa mikoa wa CHADEMA wamepinga uamuzi wa Dr Slaa wa kutengua uteuzi wa David Kafulila. Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi la leo tarehe 14 Novemba, ambalo halijataza majina wala mikoa ya wenyeviti hao, wenyeviti hao wanaelezwa kuutafsiri uamuzi huo kuwa ni kuendeleza kambi za uchaguzi wa chama hicho wa septemba 2009.
Habari hiyo inaeleza kuwa wenyeviti hao wanaamini kwamba David Kafulila alikuwa ndiye kinara wa kambi ya Zitto Kabwe. Habari inaeleza kwamba wenyeviti hao wanamsubiri Dr Slaa kwenye kikao cha Kamati kuu ya chama hicho kilichopangwa kufanyika Nov 27 na 28 waweze kumpinga.
Habari hiyo imemnukuu Katibu wa CHADEMA mkoa wa Kigoma akieleza kwamba wao bado wanamtambua David Kafulila kuwa ni Afisa wa chama kwa kuwa hajapewa barua rasmi na makao makuu kuelezwa kwamba uteuzi wake umetenguliwa.
Aidha katibu huyo, anayefahamika kwa jina la Msafiri Wamalwa amemueleza Kafulila kuwa ni Afisa anayetoka katika Mkoa wake Jimbo la Kigoma Kusini ambapo ni kati ya maeneo ambayo chama hicho kimefanya vizuri katika uchaguzi wa serikali za mitaa.
Kwa upande wake David Kafulila ameeleza kuwa alipokea mwaliko wa kuhudhuria kikao kilichoitishwa na Mo Ibrahim hapa Tanzania chini ya Katibu wa zamani wa UN Koffi Annan
......ndiyohiyo
Habari hiyo inaeleza kuwa wenyeviti hao wanaamini kwamba David Kafulila alikuwa ndiye kinara wa kambi ya Zitto Kabwe. Habari inaeleza kwamba wenyeviti hao wanamsubiri Dr Slaa kwenye kikao cha Kamati kuu ya chama hicho kilichopangwa kufanyika Nov 27 na 28 waweze kumpinga.
Habari hiyo imemnukuu Katibu wa CHADEMA mkoa wa Kigoma akieleza kwamba wao bado wanamtambua David Kafulila kuwa ni Afisa wa chama kwa kuwa hajapewa barua rasmi na makao makuu kuelezwa kwamba uteuzi wake umetenguliwa.
Aidha katibu huyo, anayefahamika kwa jina la Msafiri Wamalwa amemueleza Kafulila kuwa ni Afisa anayetoka katika Mkoa wake Jimbo la Kigoma Kusini ambapo ni kati ya maeneo ambayo chama hicho kimefanya vizuri katika uchaguzi wa serikali za mitaa.
Kwa upande wake David Kafulila ameeleza kuwa alipokea mwaliko wa kuhudhuria kikao kilichoitishwa na Mo Ibrahim hapa Tanzania chini ya Katibu wa zamani wa UN Koffi Annan
......ndiyohiyo