Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Mwanaume anapohisi kuwa ni dhaifu katika kafanya mapenzi, yaani jogoo wake hawiki huwa anajitengenezea njia za kujitetea, ili kuonyesha kwamba yeye siyo dhaifu. Bila shaka hata wewe unayesoma hapa unaweza kuwa shahidi wa jambo hili.
Kwa mfano watu ambao wana kasoro za kimwili na ambao wanaamini kwamba kasoro hizo zimewapunguzia ukamilifu wao huwa ni wakorofi au wanakuwa na tabia zisizovutia.
Hiyo inatokana na juhudi zao za kutaka kuonyesha kwamba wao sio dhaifu.Wanaume ambao huwa wana udhaifu katika uwezo wa tendo la ndoa na wakautambua udhaifu huo, mara nyingi ni watu wenye kero kubwa sana kutokana na maumbile au malezi na mazingira.
Kwa kawaida mwanaume hujihisi kuwa kamili kama ana uwezo wa kutosha wa kushiriki tendo la ndoa. Kama uwezo huo ni mdogo kwake au hana kabisa ni lazima atajihisi kuwa na mapungufu makubwa.Mwanaume amezaliwa na kulelewa akiwa na imani kwamba uanaume wake hukamilishwa na uwezo wake wa katika tendo la ndoa.
Mwanaume anapohisi kwamba ana kasoro katika uwezo wake wa kushiriki tendo la ndoa, hujihisi unyonge, hiyo ni hatua ambayo hawezi kuipinga, kuna ambao wanajitenga kabisa na jambo hilo na huamua kutolishiriki, kama wameoa hushiriki na wake zao (kama wana uwezo kidogo) kama hawana kabisa uwezo wa kushiriki jambo hilo hawaoi.
Kama udhaifu huo umewakuta wakiwa ndani ya ndoa , mara nyingi ndoa huvurugika. Wale wasiokatishwa tamaa na hali zao huwa wanashiriki kwenye tendo hili bila kujali. Lakini kinachotokea ni kwamba, kwa sababu wao ni dhaifu na wanajua kwamba ni dhaifu, hujitahidi sana kutafuta kila njia ili wanawake wanaokutana nao wawalindie siri za udhaifu wao.Miongoni mwa njia wanazotumia ni pamoja na kuhonga fedha nyingi sana kwa wanawake hao.
Baadhi hufikia hata hatua za kuwajengea nyumba au kuwanunulia magari wanawake hao, ikiwa ni juhudi zao katika kutafuta kufichiwa siri. Inawezekana kabisa wao wenyewe wakawa hawajui ni kwa nini wanatoa fedha nyingi kwa wanawake hao bali hufanya hivyo kwa sababu hiyo.
Wao wenyewe wanaweza kuamini kwamba wanatoa fedha au kuwapa mali wanawake hao kwa sababu wanawapenda. Hii siyo kweli.
Kwa mfano watu ambao wana kasoro za kimwili na ambao wanaamini kwamba kasoro hizo zimewapunguzia ukamilifu wao huwa ni wakorofi au wanakuwa na tabia zisizovutia.
Hiyo inatokana na juhudi zao za kutaka kuonyesha kwamba wao sio dhaifu.Wanaume ambao huwa wana udhaifu katika uwezo wa tendo la ndoa na wakautambua udhaifu huo, mara nyingi ni watu wenye kero kubwa sana kutokana na maumbile au malezi na mazingira.
Kwa kawaida mwanaume hujihisi kuwa kamili kama ana uwezo wa kutosha wa kushiriki tendo la ndoa. Kama uwezo huo ni mdogo kwake au hana kabisa ni lazima atajihisi kuwa na mapungufu makubwa.Mwanaume amezaliwa na kulelewa akiwa na imani kwamba uanaume wake hukamilishwa na uwezo wake wa katika tendo la ndoa.
Mwanaume anapohisi kwamba ana kasoro katika uwezo wake wa kushiriki tendo la ndoa, hujihisi unyonge, hiyo ni hatua ambayo hawezi kuipinga, kuna ambao wanajitenga kabisa na jambo hilo na huamua kutolishiriki, kama wameoa hushiriki na wake zao (kama wana uwezo kidogo) kama hawana kabisa uwezo wa kushiriki jambo hilo hawaoi.
Kama udhaifu huo umewakuta wakiwa ndani ya ndoa , mara nyingi ndoa huvurugika. Wale wasiokatishwa tamaa na hali zao huwa wanashiriki kwenye tendo hili bila kujali. Lakini kinachotokea ni kwamba, kwa sababu wao ni dhaifu na wanajua kwamba ni dhaifu, hujitahidi sana kutafuta kila njia ili wanawake wanaokutana nao wawalindie siri za udhaifu wao.Miongoni mwa njia wanazotumia ni pamoja na kuhonga fedha nyingi sana kwa wanawake hao.
Baadhi hufikia hata hatua za kuwajengea nyumba au kuwanunulia magari wanawake hao, ikiwa ni juhudi zao katika kutafuta kufichiwa siri. Inawezekana kabisa wao wenyewe wakawa hawajui ni kwa nini wanatoa fedha nyingi kwa wanawake hao bali hufanya hivyo kwa sababu hiyo.
Wao wenyewe wanaweza kuamini kwamba wanatoa fedha au kuwapa mali wanawake hao kwa sababu wanawapenda. Hii siyo kweli.