Wenye tabia hii naomba muache, sio ustaarabu!

Wenye tabia hii naomba muache, sio ustaarabu!

Aine

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2010
Posts
1,603
Reaction score
489
Utakuta umeenda hospitali umepanga foleni na pengine mnaingia kwa namba kumuona daktari, unakaa zaidi ya masaa hata 3 unasogea tu kwenye foleni yako, ghafla anakuja mtu hapangi foleni, wala namba hana wala appointment na daktari hana, anaingia kwa daktari wanapiga stooooori kama saa moja hivi au zaidi nyie mmekaa tu kusubiri,mnabaki kusikia vicheko tu nje jamani hii inakuwaje, mimi sioni kama huu ni ustaarabu, hospitali huenda wagonjwa, hatuendi kupiga stori, kama una stori na daktari sikatai ila subiri muda wa lunch au hata baada ya kazi, watu wengine wanazidiwa na kupata madhara makubwa kwa kuchelewa kuhudumiwa na daktari.

Nawaomba sana watu wenye tabia hiyo muache, sio ustaarabu kabisa, mjue watu wakienda hospitali wanaumwa hawaendi kucheza au kujionyesha.

Pia viongozi wa hospitali mliangalie hili.
 
pole yako ila huwa inaboa sana....hata ka haendi kupiga stori

mwingine anaingia kutibiwa then huyo anatoka nyie mko kwenye

folen inakera sana
 
pole yako ila huwa inaboa sana....hata ka haendi kupiga stori

mwingine anaingia kutibiwa then huyo anatoka nyie mko kwenye

folen inakera sana
hii ni kawaida ya hospitali nyingi sana, mimi nilishaona Tumaini na sehemu zingine
 
Heheh!!

Labda hao wanaokwepa foleni ni wagonjwa mahututi wa ndani kwa ndani, akisubiria foleni anaweza kuzirai mara moja:glasses-nerdy:
 
ukitaka kui-enjoy nchi hii juana na daktari,polisi,mwanasiasa,mwanajeshi la sivyo utakuwa kila siku unateseka wewe
 
vipi ulikwenda kuwagongea mlango na kuwafahamisha kwamba walifanyalo sio sahihi?
Nalog off
 
Heheh!!

Labda hao wanaokwepa foleni ni wagonjwa mahututi wa ndani kwa ndani, akisubiria foleni anaweza kuzirai mara moja:glasses-nerdy:
hakuna kitu kama hicho, anaingia akiwa anacheka na anatoka akiwa anacheka, hakuna cha umaututi hapo, ni kukosa ustaarabu tu
 
ukigundua hivyo unamtafuta incharge faster au unakinukisha lolz..

chezea kuumwa wewe
 
Mimi nikigundua kama kuna dalili ya story ndani ni kugonga na kuingia akinitoa nasubiri kidogo nikiona bado nafanya tena mpaka watajua tu. Hiyo sio Hospitali tu bali na sehemu nyingine.
 
ukitaka kui-enjoy nchi hii juana na daktari,polisi,mwanasiasa,mwanajeshi la sivyo utakuwa kila siku unateseka wewe
Bora ujuane na wengine ila sio polisi, polisi akikujua tu kila wakati anakuja na sababu ili umpe rushwa ukiwa na tatizo, hata sehemu ya kukusaidia utasikia anakwambia boss anataka kitu kidogo kumbe yeye ndio anataka.
 
Back
Top Bottom