Wenye ndoa piteni hapa kwa ushauri

Wenye ndoa piteni hapa kwa ushauri

House of Commons

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2013
Posts
2,189
Reaction score
2,206
Habari za keekend wapendwa.

Leo Jumapili nakwenda kuimaliza vibaya. Nikiwa nitulia hapa nyumbani mke wangu ameomba simu yangu ili ampigie mtu maana simu yake ilikuwa haina credit, nikampa mi nikaingia chumbani kupumzika, amekuja chumbani amefura, akauliza namba yake nimeisevu kwa jina gani?

Mi nikamjibu kuwa nimesevu kwa jina la "Madam" Hapo ndio kivumbi kikaanza, kwanini unasevu hivo? Mbona hujasevu mrs?Akaendelea," ina maana una mtu mwingine ndio mkeo? Huyo ndie ulie msevu mrs? Akaendelea tangu leo mi sio mkeo, na ndg zako waondoke hapa kwangu...."

Mi muda huo nilikuwa nimepigwa butwaa, namsikiliza, baadae nikamwambia kusevu jina hilo ni kukupa heshima, nikamwambia ile simu nyingine nimesevu kwa jina la 'mrs' wala sina maana mbaya.

Kwa kweli baadae akasema hata simu yake haina thamani maana ni ya hela ndogo (akimaanisha simthamini maana nimemnunulia simu ya bei ndogo), na kwa maana nyingine akimaanisha yupo mwanamke ninaye mthamini na ndie huenda nimemsevu kwa jina la 'mrs' akasema mambo mengi sana, lakini mi nikiangalia sijamkosea jambo kubwa kiasi cha maneno anayoyasema. Imefikia mahali nikaivunja simu yake.

Eti wanajanvi, ni kosa mkeo kumsevu kwa jina la 'madam' Nipeni mchango wenu tafadhari, maàna bado mgogoro upo na kwa sasa ameondoka sjui amekwenda wapi. Ila katika kufoka kwake nimemsikia akisema hii kesi anaipelwka kwa mchungaji, nadhani ameenda huko kupeleka kesi.

Nipeni ushauri tu ili niona namna ya kumaliza tatizo hili.
 
We utamwandikaje madamu mkeo? Hivi kweli huna jina la kumwandika? Kwanini hata usiandike mama fulani. Pia kuna majina mengine mengi sana ambayo ni mazuri na tunaweza kuwaita wake zetu. Unasubiri uje umuenzi mkeo akiwa kashakufa au?
 
Cha msingi jiamini tuu, kama hana ushahidi kwamba unakamchepuko...

Mkeo inaonesha anautashi mdogo wa kuwaza na kufikiria, pia kutafsiri mambo....


Upendo halisi haupimwi na thamani ya kitu bali ni moyo wa mtu kukupa kitu husika...

Mtafute mkeo mueleze kwa upole tuu, ataelewa...

Kuanzia leo msevu vizur mkeo...unaeza msevu "sweetheart" honey" my darlin....

Msevu vizuri ili ajisikie vizuri...usipende kumwekea mazingira akakuwazia tofaut
 
Madam ni sahihi kabisa, labda anahasira za vitu vingine kwahiyo hilo limekua katika sehemu ya kuvutuga
 
Noted, nitafanya..


Cha msingi jiamini tuu, kama hana ushahidi kwamba unakamchepuko...

Mkeo inaonesha anautashi mdogo wa kuwaza na kufikiria, pia kutafsiri mambo....


Upendo halisi haupimwi na thamani ya kitu bali ni moyo wa mtu kukupa kitu husika...

Mtafute mkeo mueleze kwa upole tuu, ataelewa...

Kuanzia leo msevu vizur mkeo...unaeza msevu "sweetheart" honey" my darlin....

Msevu vizuri ili ajisikie vizuri...usipende kumwekea mazingira akakuwazia tofaut
 
Kweli hisia anazo ila kipindi kirefu kadri miaka 5 iliyopita, ila ni mtu wa kushikilia mambo ya nyuma

Madam ni sahihi kabisa, labda anahasira za vitu vingine kwahiyo hilo limekua katika sehemu ya kuvutuga
 
Kuna sababu ya kandika jina hilo madam.... lakini kikubwa ni kwamba madam lina maana gani kwako na kwake... na ni wakati wa kumwambia kwanini uandike madam na ulipo andika ulikua unamaanisha nini mkae mukubaliane. Ila mimi mwenyewe hapo hilo jina halijakaa sawa.
 
Pole mkuu kwakweli wanawake wanatupeleka mputamputa sana cha muhm nikuwa mvumilivu tu mkuu yana mwisho hayoo
 
Maadam ulaya ni mwanamke anaewauza wenzie kwa wanaume au mmiliki wa danguro.Msevu kwa jina zuri tu inatosha e.g Honey,,switihat na etc
 
Japo jina lina ukakasi kidogo, lakini sioni ni kwa vipi imeweza kumpandisha hasira hadi kufikia ugomvi wa kiwango hicho. Ninachokiona ana mashaka na mienendo yako tangu mda mrefu na hii ni sababu tu ya kutoa kile kilichoujaza moyo wake. Kaa chini tafakari safari ya maisha yenu. Ugomvi mkubwa mpaka wa kupelekana kwa mchungaji hauwezi kuletwa na jina "Madam". Kuna sababu iliyobackground. Ichunguze
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom