Zuberi Magoha
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 208
- 69
Ni Lazima niseme ukweli kuwa CHADEMA imeyumba mno na kama jitihada za makusudi hazijafanyika basi hiki chama kinakufa rasmi.
Haya Madudu ya akina Mbowe yanayoendelea kuanikwa na kutolewa utetezi usioeleweka yananifanya mimi niliyekuwa naichukia CCM nianze kutafakari upya kwani kwa sasa SIONI TOFAUTI YA CCM na CHADEMA (na huenda CHADEMA wanaweza kuwa hatari zaidi).
Nimefuatilia kiasi kauli za wabunge wa CHADEMA [ambao ndiyo wanafahamika sana] wakiongea kuhusu swala la Kitila, ZZK, Mwigamba -kwa kweli nimesikitika sana. Nimesikitika kwa kuwa mwanzoni niliwaona wabunge hawa kuwa vichwa ila kwa sasa nawaona viumbe hatari sana.
Ukiachilia mbali mbunge Lema ambaye yeye amekuwa haeleweki vema kwenye baadhi ya kauli zake kwa muda mrefu sasa, Mnyika, Mch. Msigwa na Lissu kwa kweli wameharibu CV zao vibaya mno kwa utumbo waliouongea kuhusiana na mgogoro unaofukuta Chadema. Sikuamini mtu kama Mnyika, Msigwa na Lissu wanaweza ku-support udikteta wa akina Slaa na Mbowe (na wengine wote) wa kuwaona wahaini watu ambao wanamawazo mbadala wa namna ya kumpata kiongozi wa chama. Mnyika ndo niliyekuwa namwamini sana lakini naye kajitosa kwenye siasa za ki-imla hata sijui kwa sababu gani.
Naomba nichukue fursa hii kuwapongeza wabunge na wanachama mahsusi wa Chadema ambao at least wameonyesha akili kwa kukaa kimya.
Ndiyo, pamoja na kwamba kukaa kimya wakati madudu yanaendelea ni unafiki, lakini ni heri ukae kimya uonekane una-akili kuliko kuongea ku-support madudu. Pongezi hizi ziende kwa Mbunge Joshua Nassari, Mbunge Halima Mdee, Wakili Mabere Marando, Prof. Safari na wengine wote ambao wamesahaulika wakati wa kutoa maoni haya.
UPDATES
Wakili Mabare Marando na Prof Safari nimewatoa rasmi kwenye list ya kupongezwa baada ya kusoma gazeti la Mtanzania wakisema wanaunga mkono maamuzi ya kamati kuu ya Chadema kwa maamuzi yaliyofanyika dhidi ya wale wanaoitwa wahaini. Vituko havitaisha Tanzania!
Sawasawa kabisa, hata uliyoyaandika hapo juu nayo ni kwa mujibu wa mtazamo wako. Kumbuka kuwa akina ZZK, Kitila na Mwigamba walivuliwa nafasi zao za uongozi ndani ya chama KABLA hata ya kupewa nafasi za kusikilizwa. Na kwa maana hiyo na MBOWE inatakiwa afukuzwe kwenye nafasi ya uongozi bila hata ya kusikilizwa baada ya KASHIFA nyingi dhidi yake KUIBULIWA. Nionavyo mimi kashfa ya Mbowe ni kubwa kuliko hata ya akina ZZK ya kupanga mkakati wa kugombea uongozi -kwanza hii haifai hata kuitwa kashfa labda kwenye chama kama CHADEMA chini ya utawala wa Mbowe.
Chadema hawezi kuwa mtu kama wewe.Kama hukuweza kuona ujinga wa Zitto kuazia miaka kadhaa na mwenendo wake ndani ya Chama kuweka makundi more than 2 times akina Shonza , mikoani leo kundi la Kitila na hata kuhamishia ofisi facebook basi una akili ndogo sana .Wabunge wanao ongea wana mandate ya kufanya hivyo ndani ya Chama sasa ukitegemea kilamtu aongee wakati ile ni taasisi ?
CHADEMA is a time bomb waiting to explode!.
Chama kilisimama kwenye misingi ya ulaghai na kuwaaminisha wananchi kuwa wao ni wapiga vita ufisadi na wakombozi wa wananchi but little known kuwa wao ndiyo walikuwa ni catalyst wa ufisadi kwa sababu chama kilikuwa kinaendeshwa na pesa za 'mafisadi'.
Nilipomuona Mabere Marando na yeye ameingia kwenye majukwaa ya siasa ya CHADEMA akipiga vita ufisadi wakati yeye ni wakili wa mafisadi, basi nikafamu kuwa timer ya bomb la ulaghai wa CHADEMA iko on.
Huu ni mwanzo tu wa mlipuko wa bomu na wajiandae kisaikologia kwa yanayokuja huko mbeleni.
Ni Lazima niseme ukweli kuwa CHADEMA imeyumba mno na kama jitihada za makusudi hazijafanyika basi hiki chama kinakufa rasmi.
msaliti ni mbowe,mmedanganywa kura ziliibiwa kumbe watu wamepiga pesa za mafisadi kama hii haijawavunja moyo kwenye siasa nitawaita majuha
Wewe mwenye akili nyingi sana kwa nini hukujiuliza toka mwanzo kwa nini hayo makundi (unayodai yalikuwepo, Pamoja na kwamba najua ni stori za mitaani) yatokee? Huoni kuwa ZZK alianza kupambana na udikteta wa akina Mbowe na Slaa muda mrefu? Na kwanini hayo unayoyasema (ya akina Shonza) HAYAKUINGIZWA KWENYE LIST YA MAKOSA ALIYOPEWA ZITTO? umesoma kweli wewe makosa yaliyoandikwa na akina Slaa dhidi ya ZITTO? Kinachonishangaza na nyie wapenzi wa Chadema ni kuwa karibu wote mnadhani ZZK ndo tatizo na kusahau wanaoiua demokrasia ya kweli ndani ya chama.
Nenda ukasome katiba ya chama chenu ujue mwenye mandate ya kuongea ni nani? Naona umeanza kuchanganya mambo kwa makusudi ili kuupotosha umma wa Jamii forum. It reaches a point when you need to accept challenges for your own benefits.
Nadhani mtoa hoja tungekupongeza sana kama ungekuja na njia mbadala ya kushugulikia chanzo cha mgogoro ndani ya CHADEMA; ambao kila mmoja anatambua kuwa ni "usaliti" wa ndg Zitto ndani ya chama.
Wewe kama mtu mwenye akili, weledi na busara ni vizuri kushauri bila upendeleo ili kukinusuru chama; ila ni wazi kabisa kwamba dawa pekee ya usaliti ni kutimua.
Huwezi kuvumilia pale unapo hujumiwa. Ushahidi wa kutosha uko wazi jinsi Zitto alivyo tumiwa na wabaya wa CHADEMA ili aue chama.
Kama naye alikuwa na tuhuma dhidi ya Mbowe, mbona kakaa kimya siku zote aje kufunguka leo baada ya kuchinjiwa baharini? Si angeongea mapema akiwa bado na heshima zake ndani ya chama ili watu wamwelewe na kuchangia hoja?
Kumbukeni Zitto analeta janja ya kuku kuwa na nguvu nyingi z kutaka kuruka na kukimbia mara tu akishakatwa kichwa.
Ni ujinga wa kufikiri uko hivi kama kweli ni mwana mageuzi huwezi kuwaza namna hii, haiwezekani kupata mabadiliko kamili bila kufuata hatua kwa hatua kama ulikuwa unasema uko katika harakati za kutafuta mabadiliko kisiasa na kimfumo lazima utambue jitihada ndogo za chama kikuu cha upinzani hasa Chadema, ila kama ulikuwa unatafuta mfano wa malaika Ndani ya chama wewe bado hujatambua unataka nini katika harakati hizi na uvivu zaidi wa kufikiri kama utasema iwapo hujaona malaika Ndani ya upinzani, eti ubaki ccm! ! Tujitambue
Chadema ni Ccm A na Ccm yenyewe imeshakuwa namba mbili. Yaani maovu ya CDM kwasasa ni zaidi ya wale CCM.
Nilishaandika hapa kwamba CHADEMA kiufupi ni CCM-B, na watu kama kina Mnyika ingawa wanaweza kuwa smart, wanaweza kuponzwa na mwenendo wa chama kizima.
Watu wakaona huyo Kiranga tu.
Na kwa kweli haya si yote, kuna mengine mabaya zaidi yamejificha.
Wanaosemana kwa mabaya hawaanzi kwa kuanika mabaya yote kwa kawaida, yale mabaya zaidi hubakishwa vita vikikomaa.
Nahofia kwamba yale machafu kabisa bado hatujayajua.