Wengi wapo kwenye ndoa

Wengi wapo kwenye ndoa

Uchawi wa ndoa ni unyenyekevu tu basi.
Hao uliozungumzia hawana mambo mengi huenda wanakuwa wanyenyekevu. Unyenyekevu si udhaifu.
 
Hapana mkuu, ndoa za siku hizi ushenzi mtupu, ni heri kuwa bachela kuliko kujiingiza kwenye shimo la ndoa.
Tatizo jamii ya siku hizi haijawekeza katika kuwaandaa vijana kuishi maisha ya ndoa. Na hii inapelekea vijana wengi kujikuta ndani ya ndoa bila kujua wameingia vipi.
Hapo ndo shida inapoanzia mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao ulowataja kuwa hawana mambo mengi, ni wazi pia hawana matarajio makubwa maishani.... kinachoponza ndoa ni ujuaji au kutarajia vitu vya kufikirika.

Wewe bado upo kwa shemeji yako, si unamwona dadako ni wa kawaida tu..!!
 
Sijui kwanini vijana wengi siku hizi wanaona ndoa ni mkosi au balaa ? Ila mimi napenda niwaeleze tu kwamba kama Kuna jambo lenye furaha duniani no Ndoa Kama utaweza kujua siri ya ndoa ambayo ni uvumilivu lakni hayo mengine mnayoyapenda ni ushetani na ubatili mtupu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NDOA SIO SIFA MKUU NA SIJAONA UMUHIMU WAKE
USISUBUTU KUINGIA HUKO UTAJUTA KILA KUKICHA TUNAWAAMULIA KESI MARA KUCHAPIWA MARA MATATIZO MARA MKE HAPENDI NDUGU ZANGU


SIWEZI INGIA KWENYE ILO SHIMO WE TATUFA WATOTO BASI KUOA WAACHIE WALUGALUGA

NA MDA SI MREFU WATAKUJA KUJIFARIJI HAPA

Kwahyo utak kuoa??


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
NDOA SIO SIFA MKUU NA SIJAONA UMUHIMU WAKE
USISUBUTU KUINGIA HUKO UTAJUTA KILA KUKICHA TUNAWAAMULIA KESI MARA KUCHAPIWA MARA MATATIZO MARA MKE HAPENDI NDUGU ZANGU


SIWEZI INGIA KWENYE ILO SHIMO WE TATUFA WATOTO BASI KUOA WAACHIE WALUGALUGA

NA MDA SI MREFU WATAKUJA KUJIFARIJI HAPA
Mkuu kumbe ulishaharibiwa siku nyingi? Pole sana mkuu wengine tumetulia tu tunashangaa wanaolaani ndoa walipata hitilafu wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vijana wengi wa kiume waliozaliwa Sinza Dar hawaoi
Vijana wengi wakiume waliozaliwa Kaloleni Arusha hawaoi
 
Asilimia kubwa ya wanawake ambao nimesoma nao, shuleni hawakuwa na mambo mengi, hawakuwa na mvuto kiviile, hawakuwahi kutokea hata kwenye top 20, yaani kiujumla walikuwa washamba washamba hivi. Leo hii wapo kwenye ndoa.

Hata vijana wangu niliowafundisha, wale ambao darasani walikuwa vilaza, regardless ya personality zao. Wengi wapo kwenye ndoa.

Sijui kama wanafurahia au laah! Lakini wapo kwenye ndoa zao. Upande wa pili sasa ni balaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Upande wa pili upi?? Wa welevu na wakali wa mahesabu darasani??
 
Back
Top Bottom