Nimefika pale kituoni bado siamani amini, ila nisha jiandaa kwamba sio issue ndogo. Kilichonishangaza kwa mda ni kumkuta linda mule ndani. Na kiukweli she didnt look good at all. And she was the last person i needed. Mjue mpaka mi mtu mzima naamua kumchomeka bisu mtu mjue yalionikuta sio madogo.
Najua una hamu sanaa ya kujua kwanini nilimchoma kisu Hans naomba fundi utulize mshono huo. Ishu ilianzia mbali sanaa. Mnooo. Like evry other night mare inaanza kama story nzuri ila mwishowe ndo inakengeuka. Anyway ndo nishafanya nilichofanya wala sijutiii kabisaa. I never wanted to be a star, then i became a star overnight then now i am muderer overnight.
It all started baada ya Sam kunusurika kufumania kwa mara ya 2. Bado nilikuwa sitaki kumwambia. Bado nilikiwa na chekecha. Sam alishanifanyia umalaya sanaa yule boya. So design kama nalipiza vile twende aste aste chali yangu. Mambo yakikwenda yalivokwenda.
Bada ya Hans kuondoka nikaanza kumtongoza upyaaa. Hatakiii! Anauliza ushamwambia? Namwambia bado. Ndo mwisho wa mawasiliano. Nikakata tamaa, nikaamua kwa Sam kurudi siwezi, i am already past that with or without Hans. Na mimi nikaanza kumpotezea. Ikapita wiki kimya kimya. Nikasema duuuuh kweli ngoma ya kitoto haikeshi. Akaanza ungese wa kumpost mdada mwengine Insta. Nikasema naiweka wapi sura yangu. Kila mtu anajua niko na huyu shoga. Najuuuta. Nilimkumbuka Sam kwa asilimia 20 labda. Nika mu unfollow na kumblock kabisaa. Nikatoa oda akija dukani afukuzwe kabisaa. Sipendagi uhanisi.
Siku hio niko home, saa 7 nasikia mtu anafungua mlango. Nikajua yeye si ana funguo. Nikasema bora nimpore funguo zangu. Kumuonaaa ananilegezaga nguvu. Naona kama namuoneaaa sijui kwasababu ya umri wake. Nikaamua tu nikiache Diplomasia. Kaingia anaanza kuvua nguo. Nikamwambia vaa takataka zako acha funguo zangu sepaaa. Akauliza niende wapi sahizi? Nikamwambia kwa uliempost. Anisaidie na mimi kidogo maana tunapostiwa wote. Akaguna akamalizia kuvua nguo akaenda kuoga.
Mi nawaza hata mkononi hajai, mtu mwenyewe Skinny nikianza kupigana nae man to man hapa si namvunja mtu mwenyewe manzi wa chugga ariff. Ni shigidiii aisee. Akatoka kuoga. Nikamwambia Hans toooo toka kweliii! Anajikausha uchi uchi. Anasema tatizo Kyle unapenda ubabe sanaa, nitoke kivipiii? Kama kuchukia nilitakiwa nichukie mimi, bwana wako kanusurika kutufumania, afu kununa unanuna wewe. Sio fair hivo baby. Unalalamika post post. Haya ngalia video kamili unune vizuri sasa. Akanipa simu. Kumbe video vixen wa wimbo uleee alionisikilizisha.
Ikabidi nibadili gear angani, nilikumisi sanaa, afu ulivoniacha siku ile sivo sivo. Akazima taaa. Nikasema afadhaliii. Akaja, ananiambia leo nina ukamee sanaa, sijapiga show tangu siku ile. Design sijui tukaiendeleze pale pale.Namwambia hapa hapa. Anauliza ile post ilikutia wivuu. Najibu ndioo. Namwambia uka ni block kabisaa. Anasema ndio. Basi hapo ndo kunishika kwa hasiraa. Na mimi nina hasira zangu. Nilimmisi kiukweli sababu anajua kunifikisha pale napotaka kwendaa.
Tumeenda vizuri kabisaa kwa kasi ya 4g, nikachukua machine nijiwekee. Wote tuko speed 120. Hamu inaweza kuniua. Akaniuliza ulimwambia? Nikasema ndio. Ilibidi niseme ndio. Ningesema suuu show ingeishia pale. Akatabasamu, akaweka kidogooo ndo nikvurugikaa kabisaa, namwambia baby nipe yote. Akaniuliza akasemaje ulivomwambia. Nikamwambia kasema Poa tuuu, yeye hana shida kabisaa. Akauliza Sam ndo kasema hivo? Nikamwambia ndio baby. Akasema nakuja mara moja.
Nilichosikia ni mlio wa gari inaondoka njeee. Gademmmuuuuuu! Ndo nikajiona ndeziii! Sam kasema poa haina noma! Aiseee kama uwongo nimefeli vibaya vibaya. Jamanii! Nikawaza nikafanyane na mtu mwingine? Nalalaje hivo. Ila hawezi kunifanya kama dogo. Dogo anafanya. Siku ile niliuza mechi ila nilipakwa tushombo. Nikamtumia meseji sorry nilidanganya. Mi Sam namuogopa, labda tumwambie wote. Akajibu sawa. Panga mkutano mi nitamwambia. Namwambia rudi basi kimojaa tu cha kulalia. Akasema mpaka umwambie Sam.
Kikao hakikwenda shwari, balaa lilikuwa kubwa. Sam akawekwa ndani. Kiukweli Sam simpendi tena ila ni zaidi ya kaka angu. Nisingekubali alale ndani. Kumtoa siwezi. Nikampigia Linda akaenda kumtoa. Linda na Sam wanapendana mda sanaaaa. Maana tangu dukani Sam alikuwa anamkata jicho la kiume siku ya kwanza kabisaa. La matamanio. Bwana akiwa wako hata azuge vipi unamjua. Siku ya double date Sam hakuniambia Linda kamtongoza, nilihisi Sam kamtongoza nikamtega tu linda. Na Linda akawa anamkata jicho hilo hilo la loost Sam. Hata alivomkalia uchi dukani nilimuona vizuri.sema nishajikatia tamaa, kwa Sam nilifika bei. Mpaka wanatiana ukumbini niliiona ile, maana walipotea wote, nikaenda chooni nikawasikia. Na nikajifanya mjinga. Sasa jiulize kwa moyo wangu huu wa jiwe dogo kanifanya nini mpaka nimchomeke bisu? Kama haya yote nilivumilia. What i respect Sam ukiachaa tamaa tamaa za fisi nafasi yangu kwake ilibakia pale pale.
Tukarudi nyumbani, akatoka usiku huo huo. Akaja na bag 3 za nguo ndo kahamia jumla. Niliona poaaa tu manake ni unlimited game. Mimi tu. Ngombe ninae ndani, maziwa bwerere. Siku hio sitaisahau, tulipiga show leo usiku mpaka kesho saa 10, kazi ni moja tu. Hamu yote iliniisha. Niwekwa na insta live. Dogo alikuwa na mzukaa balaa. Nikaona haya ndo maishaa maishaaa. Maisha ndo haya.
Dogo anajua kupenda, anajua kuharibuuu. Yaani alivosema kujibana hawezi hawezi kweliii. Kumbi kumbi. Anajaliiii. Anamwambia mama yake kuhusu mimi mpaka basi. Mama kila siku jioni lazima apige simu. Mama akaniletea zawadi ya chupi. Nikawaza sanaa anasitiri anapopumzika mwanae , au mwanae kamwambia sina chupi, au upendo tu, au ndo kashazifanyia mambo ya kiswahili sikuelewa. Niliivaa lakini. Mama mkwe akawa mpaka shoga angu. Namvalisha mimi. Kumsindikiza sasa mpaka saluni. Nilitegemea ataniletea mambo ya mkubwa kwa mwanangu walaa.
Kumloga Hans umpende mama yake. Akiwakuta na mama yake hivi labda mnataka kwenda mahali atatoa burungutu lote la pesa mfukoni. Mama mtu mstaarabu. Sio mgumu kuishi nae kabisaa. Anatupikia mda mwengine, anamfulia mwanae mpaka mimi. Na anapenda mambo ya mjini balaa. I was happy na hii familia. Nikaona naweza kuishi na hii familia hata miaka 20. I was happy i had a family.
Acha surprise, nimekaa zangu dukani, akaja akaniambia baby leo nina pesaa. Nataka tutokee. Nikamwambia ngoja niende home nika chenchi, akasema hamna twende tukanunue nguo. Akanipeleka mwenywe dukani, nikachukua nguo, akalipiaa. Sio kitu kikubwa ila nilifarijika saanaaa. Anasema tuone ilivokaa. Akanikumbusha Sam tulivogongana na Linda.
Akaanza kusema nataka mtoto. Hasemi direct anachomeka ningekuwa na ka junior mda huu nakabeba beba.Nikamwambia mtoto na ndoa. Akasema kama upo tayari namwita sheikh anakutia maji, unakuwa Kayla tunachoma ubaniii. Nikamwambia dini sibadilishi. Akasema ndo maana mi sikutaka ubadilishe, nikataka mtoto. Dini mwenyewe ukirdhia kwa kunipenda kwako utabadilisha kwa nafsi yako. He was so sweet!
Nikaanza kuumwa umwa, mpaka ufunguzi wa kina linda sikuweza kwenda. Nilikuwa najisikia vibaya sanaa. Akaja mama mkwe akaniambia una mimba wewe. Nikapima nikakuta kweli. Sherehe wiki nzimaa. Jina limeanza kutolewaa. Nadekezwaa balaa. Mimba ukiwa na mtu anaejua thamani yake raha sanaa.
Ikabidi nisafiri, akasema huendi peke yako, na hali hii, twende wote. Visa alitafuta mwenyewe. Safari nzima aliniuguzaa, nikashukuru alikuja. Na alinitunza kwa kweli. Kufanya kama kawaidaa. Nikamwambia mtoto atatoka mchafuu. Tumefunga mizigo tumerudi salama.
Nyumbani sasa kwenye kufungua mizigo ndo balaa lilipoanziaaa. Ugomvi, ugomvi na wewe. Zilianza ngumiii msione mama kija mkajua nilimwachia, tumezichapa. Tatizo langu pigana yangu chovhote kilicho mbele yangu, na siku hio kisu kikombele yangu. Akakidaka, nilipambana mpaka nikamchoma cha tumbo. Midamu mwaaaa. Nikampigia mama mkwe nishamuua mwanao. Akaja na watu fastaaa, ndo kuita polisi. Nikaletwa huku.
Linda sikujua kaja kwa kesi gani, sikuwa na shobo nae. Yeyendo alianza kushoboka. Ananiuliza kwanini umemchoma kisu Hans. Nikamuuliza na Hans unamtaka, Sam ashakushinda? Akasema usitaje hilo jina, nimempiga risasi hivooo sema marehemu Sam, Ina lillah wa inaallah rajioon! Sikustukaa. Akasema mbona hustukii. Nikamwambia nistuke nini kwa mfano? Namjua malaya mbwa, wewe si ulitembea nae nikiwa nae. Itakuwa umemfumaa hajuagi kujificha.
Ukapita ukimyaa mrefuuu. Nikamuita afande shostiii! Akaja nambie shoga angu. Nakuonaga instaaa! Nikamwambia eeeh, naomba panadol shoga angu na simu nimpigie mtu. Akaleta. Linda akasema na mimi, akaambiwa kelele weeee na msonyo juu. Nikamwambia mpe yule shoga angu pia. Akasema hapo sawa. Akapewa. Akanipa simu. Nikapiga kwa mama mkwe, ananiambia bora tumemuwahiii, sasa kwanini kwani ilikuwaje? Nikamwambia mama story ndefu sanaa. Nashukuru kama mwanao mzima. Nisamehe mie. Ananiambia nitakuja kesho kukuletea chai.
Linda anasema mbona wewe una tritiwa kwa upendeleo. Nikamwambia mimi star, na victim wangu star, wewe no body. Simu nilikaa nayo usiku kucha. Nikawapigia nyumbani. Linda akaomba. Nikamnyima, baadae nikamuonea imani nikampa. Akapiga ofisini kwake kuwaambia alipo. Akawapigia na watu wengine. Baadae nikarudisha kwa shostiii. Akaniomba selfie, shoga usinipost nitadhalilika.
Linda akaniambia niambie ilikuwaje nikupe ushauri, unaweza kuwa star ila haupo juu ya sheria. Nikamwambia Linda pambana na hali yako. Mi siwezi kukubali lawyer muuaji anitete kesi ya mauaji. Mwenzio Star kesho napandishwa mahakamani wa kwanza. Wewe bado upo sanaa. Tutakutana Segerea tukijaaliwa. Nina mengi kichwani niache nitulie.
Kesho kweli nikapandishwa mahakama ya mkazi kisutu, nikikabiliwa na makosa 6. Shambulio la mwili, kula njama za mauaji, kijaribu kuua. Kujeruhi kwa silaha kali, domestic violance, uharibifu wa mali, Nikasomewa pale mashtaka yote, media zimejaaa kama zote.Nikaulizwa ofcourse i pled NOT GUILTY to all six counts. Nikaambiwa haki zangu pale. Na nikapelekwa segerea mpaka tarehe ya kuanza kusikilizwa kesi.
Raha ya jela uingie na kosa KUBWA KUBWA. Nimefika pale, nikapangiwa VIP si star. Na kila mtu akishoboka kosa gani? Mauaji. Naonekana namba tasaaa ariiif. Sio kabisaa. Mahakamani walijaa watu wa chugga, mzee wangu alikuwepo, alitia huruma sikumuangalia mara mbili. Maana ana ma pressure na hii ishu ilimkalia vibaya sanaa.
Baada ya wiki nikakutana na Linda yupo on general population, kakonda sanaa. Maisha ya huku hayakumpenda kabisaa. Akaniambia I DONT KNOW ABOUT YOU KYLE BUT I AM GETTING OUTOF HERE SOON, I MUST, I HAVE TOO.BY ANY MEANS.
ITAENDELEA.