Wedding Anniversary

Wedding Anniversary

Fixed Point

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2009
Posts
11,304
Reaction score
12,753
Ndugu zangu wapendwa, leo tarehe 9/10 ni kumbukumbu ya agano langu la ndoa kati yangu na mpenzi wangu miaka 13 iliyopita.

Namshukuru sana Mungu wangu kwa kunipa huyu rafiki yangu kuwa mwenzangu. Ni jambo ambalo sijawahi kulijutia katika miaka yote 13 niliyoishi naye. Nazidi kumwomba Mungu tuzidishe upendo katika haya maisha tuliyoyachagua.

Nawaomba pia rafiki zangu wenye mapenzi mema mzidi kutuombea maisha yenye Upendo, Baraka na Neema.
 
wedding-anniversary-311.JPG
 
wow!! congrats FP, may GOD bless your marriage and let you enjoy it till the end.big up pia kwa anniversary hiyo not everyone is blessed with that!!! am just praying that i will also be blessed with a grace of living marriage life with someone special someday.
 
wow!! congrats @FP, may GOD bless your marriage and let you enjoy it till the end.big up pia kwa anniversary hiyo not everyone is blessed with that!!! am just praying that i will also be blessed with a grace of living marriage life with someone special someday.
Amen my dear.
Dont worry, I am very sure there is someone special out there for you. May the God Almighty Bless you with the power to recognise that person.
 
Hongera sana dada yangu FP kwa kutimiza miaka 13 ya ndoa. Kwa kweli unastahili sifa na pongezi maana si wote ambao wamebahatika kupata wenzi bora wa maisha na wakadumu nao kwa mda mrefu huku wakiishi kwa amani, afya na furaha...Lakini pamoja na hayo yote, sifa na shukrani ziende kwa Mungu muweza wa yote aliyekujalia hekima na akili ya kuweza kuchagua mwenzi bora wa maisha.

Sina mengi ya kusema zaidi ya kukutakia mema na baraka tele katika safari yako ya maisha ya ndoa...Mungu awaongoze katika safari hii ya maisha yenu, kila mfanyalo mlifanye pamoja naye...awajalie muweze kujenga familia bora na yenye kumpendeza Mungu...Hongereni sana katika kusherehekea siku hii ya leo...na ninawatakia kila heri na baraka tele katika safari hii ya maisha yenu ya duniani...Mungu awabariki sana.
 
Back
Top Bottom