We Double Dare Them: Do it Again...Tunawathubutisha! Fanyeni Tena...

We Double Dare Them: Do it Again...Tunawathubutisha! Fanyeni Tena...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,092
Reaction score
43,265
Na. M. M. Mwanakijiji

Ni kana kwamba Oktoba 29 haikutokea. Wanaendelea kutenda kana kwamba yaliyotokea siku ile ya giza ni mambo tu ya kufikirika. Wanaendelea kutenda kana kwamba tunawaonea, tunawasingizia na kuwa yote yanayosemwa ni uzushi tu uliopitiliza. Wanajitahidi kupuuzia, kutokujali na kutenda kana kwamba damu waliyoimwaga si ya Watanzania.

Tunaambiwa katika kutetea kiti chake Rais aliidhinisha ubakaji, ulawiti wa watoto wetu na zaidi mauaji. Mwenyewe kasema "nguvu iliyotumika" inaendana na tishio lililokuwepo. Ati wangetumia nguvu kidogo wangeondolewa kwa mapinduzi (msisahau chama kinaitwa ni 'cha mapinduzi'). Kama walivyofanya kabla ya Oktoba 29 walitoa vitisho na mikwara ya nguvu na kweli kabisa wakaenda kutekeleza walichokipanga kiwe funzo kwa yeyote atakayewapinga.

Miili tuliyoiona imezagaa, picha za video na za kuganda tulizoziona za watu waliouawa kinyama na kuachwa hadharani kama vibudu vyote hivyo ni makosa ya Mange, Maria Sarungi, na wanaharakati. Kwamba, watu walioko Tanzania wanatakiwa kupiga makofi kila wakubwa hawa wanapopita, walioko Tanzania hawatakiwi kusema siyo kwa jina letu. Walioko Tanzania tunaambiwa ni lazima wakubaliwa kutawaliwa bila kujali wanavyotawaliwa. Mauaji ya Oktoba 29 ilikuwa ni "fanya fyoko ukione"; watawala wetu hawa walioshindwa wanarudia tena - 'fanyeni fyoko muone kama hatutawachinjilia mbali".

Wanatukumbusha vikundi visivyo vya serikali kama kule Sudan na sehemu nyingine ambavyo vilishiriki mauaji ya wananchi wao kwa jina la kuitetea serikali. Tunawasikia wengine wanajitokeza na kupiga mikwara kuwa wako tayari kuitetea serikali; hawa wanaweza kupewa silaha, za moto na za jadi kuingia mitaani kuua. Kama ilivyotokea Oktoba 29 hawa wauaji wa serikali hawahitaji kujitambulisha; vitambulisho vyao ni bunduki, alama zao ni bastola!

Ni kweli wataua tena; wameonja damu na wameongezeka hamu! Wanajua sasa hivi hawawezi kutawala tena kwa hoja; isipokuwa hoja za risasi na visasi! Zamani waliposhindwa hoja walikuwa wanaleta vihoja; sasa wameshindwa hoja kwa kasi sasa wanaleta risasi na visasi. Tunawathubutisha tena! Ueni tena wananchi wetu; jitangazeni mipango yenu, semeni kuwa mnaenda kuua tena kama mlivyofanya hadi Watanzania wote wasalimu amri!

Hawa wamenza kufanana na utawala ule dhalimu tuliowahi kuuona katika bara letu la Afrika; wamefanana kila kitu isipokuwa rangi tu. Watawala hawa wanataka kutawala kwa kuua; na niwe wa kwanza kutabiri baada ya mauaji yaliyopita na haya yajayo; Samia hatoweza kutoka madarakani; na hatoachwa atoke madarakani na watu wanaomtegemea kuwalinda. Sasa hivi naamini kuna uwezekano wa asilimia 99 watakapopendekeza Katiba Mpya wataondoa ukomo wa madaraka (term limits) ili Samia aendelee baada ya 2030. Atoke achekwe?

Lakini vyovyote vile ilivyo, kuelekea Disemba 9 wao ndio wanauamuzi wa kufanya; watoke waue tena mamia wengine au watafute hekima ya jinsi gani kudifuse the situation. Lakini kwa vile wameshajawa na roho ya ubabe na kuwa wanataka kulinda "dola" aka familia na maslahi yao uwezekano wa wao kurudi nyuma ni sifuri. Kweli hawa wanaweza kuua tena; lakini wajue kuwa wao wameshajifunza kuua na Watanzania wamejifunza kufa kwa ajili ya nchi yao.

Ila waue tena; ili waharakishe mwisho wao. Imebidi nifunge safari ya ghafla kuja kufuatilia ya mambo ya Disemba 9; tunakusanya ushahidi vizuri zaidi sasa kuliko ile Oktoba 29. We double dare them.. do it again. Please.
 
Ulipoa sana miaka michache iliyopita naona umerudi kama ulivyokuwa zamani.

Na. M. M. Mwanakijiji

Ni kweli wataua tena; wameonja damu na wameongezeka hamu! Wanajua sasa hivi hawawezi kutawala tena kwa hoja; isipokuwa hoja za risasi na visasi!
I'm hesitant to admit this, but when people feel cornered and desperate, and believe their very existence depends on maintaining power, they can resort to doing harm.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ni kana kwamba Oktoba 29 haikutokea. Wanaendelea kutenda kana kwamba yaliyotokea siku ile ya giza ni mambo tu ya kufikirika. Wanaendelea kutenda kana kwamba tunawaonea, tunawasingizia na kuwa yote yanayosemwa ni uzushi tu uliopitiliza. Wanajitahidi kupuuzia, kutokujali na kutenda kana kwamba damu waliyoimwaga si ya Watanzania.
Hongera kwa kurudisha uandishi
 
Naam

Nadhani unafahamu kitakachokwenda kutokea kwahiyo ilikuwa ni busara kuja na njia mbadala ya kusuluhisha haya mambo ili yaweze kuisha

Kutunishiana misuli kwa kuwaweka chambo watoto wa masikini mnakosea sana na hakika mtakuja kulipa hili

Kifo hakijawahi kuwa suluhisho la tatizo lolote watu tunaoshindana nao hatuwawezi kwa namna yoyote

Kila mwananchi anaelewa system ya Government ilivyo so haina haja ya kila dakika kuanzisha mathread ya kuchochea maaandamano

Hii inaonesha kwamba kuna watu ni wanufaika wakubwa wa haya maandamano, kuna watu ndo wanapopatia ugali wao that's why hawataki option nyingine yoyote zaidi ya hii waliyoichagua

Watanzania inatakiwa tuamke sio kila jambo ni la kubeba tu kama matahira tunashindwa hadi na kunguru ambaye akiona umeshika manati atakimbia eneo hilo kwa sababu anajua madhara yake

Kumshawishi raia masikini aende barabarani akiwa hana silaha yoyote ya moto huku mkijua kabisa atakachoenda kukutana nacho ni dhambi moja kubwa sana na hakika mtaenda kuchomwa motoni

Hao kina Hilda na Maria Sarungi wanashindwa nini kutoka Kenya huko kuja kuungana na wenzao huku kupamabania nchi yao.Wao ndo wanajiita mashujaa wa keyboard na kuna nyumbu za Tanzania zinaingia kweli barabarani aisee

Boniface Mwangi mwanaharakati maarufu Kenya kipindi cha maandamano ya Gen Z wa Kenya wala yeye hakuhamasisha akiwa Uganda au Tanzania bali alikuwa palepale Kenya na siku ya maandamano alikuwa front vile ndo inatakiwa

Kuna yule Aunt Lulu kabla ya kukengeuka alishawahi kukiri kuwa analipwa Milioni mbili kwa mwezi na Sativa kwa ajili ya kupost harakati tu hii inaonesha kuna pesa wanapata kupitia hayo mambo

Tunaizika nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe
 
Ndio ninachoogopa....soon magenge ya kulipiza visasi yataanza kazi
WAsije kudhania ni wao peke yao wanaweza kuwa na vikundi vya magenge haya; wanataka tufike ilikofika Zanzibar... watu wasile pamoja, wasizikane, na kususiana kila kitu. Hadi walazimishe "muafaka" mpya.
 
Kwa sasa tunachokiogopa ni Hofu tu tushazika ndugu na rafiki zetu 29 hatuna chakuhofia tena mwanzo ndio ulikua mgumu acha waendelee kuahupaza shingo
 
Naam

Nadhani unafahamu kitakachokwenda kutokea kwahiyo ilikuwa ni busara kuja na njia mbadala ya kusuluhisha haya mambo ili yaweze kuisha

Kutunishiana misuli kwa kuwaweka chambo watoto wa masikini mnakosea sana na hakika mtakuja kulipa hili

Kifo hakijawahi kuwa suluhisho la tatizo lolote watu tunaoshindana nao hatuwawezi kwa namna yoyote

Kila mwananchi anaelewa system ya Government ilivyo so haina haja ya kila dakika kuanzisha mathread ya kuchochea maaandamano

Hii inaonesha kwamba kuna watu ni wanufaika wakubwa wa haya maandamano, kuna watu ndo wanapopatia ugali wao that's why hawataki option nyingine yoyote zaidi ya hii waliyoichagua

Watanzania inatakiwa tuamke sio kila jambo ni la kubeba tu kama matahira tunashindwa hadi na kunguru ambaye akiona umeshika manati atakimbia eneo hilo kwa sababu anajua madhara yake

Kumshawishi raia masikini aende barabarani akiwa hana silaha yoyote ya moto huku mkijua kabisa atakachoenda kukutana nacho ni dhambi moja kubwa sana na hakika mtaenda kuchomwa motoni

Hao kina Hilda na Maria Sarungi wanashindwa nini kutoka Kenya huko kuja kuungana na wenzao huku kupamabania nchi yao.Wao ndo wanajiita mashujaa wa keyboard na kuna nyumbu za Tanzania zinaingia kweli barabarani aisee

Boniface Mwangi mwanaharakati maarufu Kenya kipindi cha maandamano ya Gen Z wa Kenya wala yeye hakuhamasisha akiwa Uganda au Tanzania bali alikuwa palepale Kenya na siku ya maandamano alikuwa front vile ndo inatakiwa

Kuna yule Aunt Lulu kabla ya kukengeuka alishawahi kukiri kuwa analipwa Milioni mbili kwa mwezi na Sativa kwa ajili ya kupost harakati tu hii inaonesha kuna pesa wanapata kupitia hayo mambo

Tunaizika nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe
Unafikiri tatizo ni kwa wanaotaka kuandamana tu; ni kana kwamba unaamini serikali haina makosa. Wakati wa utawala wa makaburu kuna watu walikuwa wanafaidika na utawala ule; hawakuwa tayari kuoneshea kidole; usikate tawi ulilokalia. Na makaburu waliua bana...
 
Kisasi lazima kitalipwa tu ni swala la muda. Mwenyewe hao wenye uniform wakikaa vibaya namrushia hata mate
Ha ha ha Mimi juzi nilikutana na Polisi nilimkata jicho Kali mpaka ajishitukia mwenyewe.

Nikipata nafasi ya kulipa KISASI nitalipa haraka
 
Unafikiri tatizo ni kwa wanaotaka kuandamana tu; ni kana kwamba unaamini serikali haina makosa. Wakati wa utawala wa makaburu kuna watu walikuwa wanafaidika na utawala ule; hawakuwa tayari kuoneshea kidole; usikate tawi ulilokalia. Na makaburu waliua bana...
Serikali ina makosa pia na wameshakiri wenyewe wamekosea

Tuwape room ya kujirekebisha na kutenda yale waliyoahidi.Tunachotaka kukifanya sisi ni kumporomoshea matusi mtu unayemdai akiwa amechelewa kurejesha na pesa akiwa bado kaishika mkononi mwake anaweza akaamua kuondoka nayo na asikulipe tena

Hizo habari za dunia kuangalia ndo zinawapoteza vijana kwanini tukariri njia moja tu ya kupambana na hawa madhalimu njia ambayo tumeona madhara yake

Njia ambayo tumeona wanachi wengi hawajaiunga mkono ndo maana tumeona misururu ya watu wakiondoka Dar kwenda vijijini

Kwenda barabarani na jiwe huku mwenzako akiwa na bunduki inaonesha jinsi gani tuna akili finyu

Kushawishiwa na kakikundi cha watu wachache hasa wanafahamika wa chama fulani waliopo nje ya nchi kuingia barabarani halafu wao wakichungulia kwenye computer zao kinachoendelea ni upumbavu

Tunawapenda ndugu zetu bado tunatamani kuwa nao na ndio maana hatutaki kuwapoteza hata Sativa hatamani kufa ndiyo maana badala ya kujeruhiwa na risasi akakimbia nchi kabisa ila eti anawashauri wale waliopona October 29 nao waende tena huku yeye akiwa nje ya nchi 😅🥲 inafurahisha na kuumiza sana
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ni kana kwamba Oktoba 29 haikutokea. Wanaendelea kutenda kana kwamba yaliyotokea siku ile ya giza ni mambo tu ya kufikirika. Wanaendelea kutenda kana kwamba tunawaonea, tunawasingizia na kuwa yote yanayosemwa ni uzushi tu uliopitiliza. Wanajitahidi kupuuzia, kutokujali na kutenda kana kwamba damu waliyoimwaga si ya Watanzania.

Tunaambiwa katika kutetea kiti chake Rais aliidhinisha ubakaji, ulawiti wa watoto wetu na zaidi mauaji. Mwenyewe kasema "nguvu iliyotumika" inaendana na tishio lililokuwepo. Ati wangetumia nguvu kidogo wangeondolewa kwa mapinduzi (msisahau chama kinaitwa ni 'cha mapinduzi'). Kama walivyofanya kabla ya Oktoba 29 walitoa vitisho na mikwara ya nguvu na kweli kabisa wakaenda kutekeleza walichokipanga kiwe funzo kwa yeyote atakayewapinga.

Miili tuliyoiona imezagaa, picha za video na za kuganda tulizoziona za watu waliouawa kinyama na kuachwa hadharani kama vibudu vyote hivyo ni makosa ya Mange, Maria Sarungi, na wanaharakati. Kwamba, watu walioko Tanzania wanatakiwa kupiga makofi kila wakubwa hawa wanapopita, walioko Tanzania hawatakiwi kusema siyo kwa jina letu. Walioko Tanzania tunaambiwa ni lazima wakubaliwa kutawaliwa bila kujali wanavyotawaliwa. Mauaji ya Oktoba 29 ilikuwa ni "fanya fyoko ukione"; watawala wetu hawa walioshindwa wanarudia tena - 'fanyeni fyoko muone kama hatutawachinjilia mbali".

Wanatukumbusha vikundi visivyo vya serikali kama kule Sudan na sehemu nyingine ambavyo vilishiriki mauaji ya wananchi wao kwa jina la kuitetea serikali. Tunawasikia wengine wanajitokeza na kupiga mikwara kuwa wako tayari kuitetea serikali; hawa wanaweza kupewa silaha, za moto na za jadi kuingia mitaani kuua. Kama ilivyotokea Oktoba 29 hawa wauaji wa serikali hawahitaji kujitambulisha; vitambulisho vyao ni bunduki, alama zao ni bastola!

Ni kweli wataua tena; wameonja damu na wameongezeka hamu! Wanajua sasa hivi hawawezi kutawala tena kwa hoja; isipokuwa hoja za risasi na visasi! Zamani waliposhindwa hoja walikuwa wanaleta vihoja; sasa wameshindwa hoja kwa kasi sasa wanaleta risasi na visasi. Tunawathubutisha tena! Ueni tena wananchi wetu; jitangazeni mipango yenu, semeni kuwa mnaenda kuua tena kama mlivyofanya hadi Watanzania wote wasalimu amri!

Hawa wamenza kufanana na utawala ule dhalimu tuliowahi kuuona katika bara letu la Afrika; wamefanana kila kitu isipokuwa rangi tu. Watawala hawa wanataka kutawala kwa kuua; na niwe wa kwanza kutabiri baada ya mauaji yaliyopita na haya yajayo; Samia hatoweza kutoka madarakani; na hatoachwa atoke madarakani na watu wanaomtegemea kuwalinda. Sasa hivi naamini kuna uwezekano wa asilimia 99 watakapopendekeza Katiba Mpya wataondoa ukomo wa madaraka (term limits) ili Samia aendelee baada ya 2030. Atoke achekwe?

Lakini vyovyote vile ilivyo, kuelekea Disemba 9 wao ndio wanauamuzi wa kufanya; watoke waue tena mamia wengine au watafute hekima ya jinsi gani kudifuse the situation. Lakini kwa vile wameshajawa na roho ya ubabe na kuwa wanataka kulinda "dola" aka familia na maslahi yao uwezekano wa wao kurudi nyuma ni sifuri. Kweli hawa wanaweza kuua tena; lakini wajue kuwa wao wameshajifunza kuua na Watanzania wamejifunza kufa kwa ajili ya nchi yao.

Ila waue tena; ili waharakishe mwisho wao. Imebidi nifunge safari ya ghafla kuja kufuatilia ya mambo ya Disemba 9; tunakusanya ushahidi vizuri zaidi sasa kuliko ile Oktoba 29. We double dare them.. do it again. Please.
Magufuli alivyoua na kukandamiza watu ulifurahia sana!! Huna moral ethics za kuzungumzia tena haya mzee mpumbavu!!
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ni kana kwamba Oktoba 29 haikutokea. Wanaendelea kutenda kana kwamba yaliyotokea siku ile ya giza ni mambo tu ya kufikirika. Wanaendelea kutenda kana kwamba tunawaonea, tunawasingizia na kuwa yote yanayosemwa ni uzushi tu uliopitiliza. Wanajitahidi kupuuzia, kutokujali na kutenda kana kwamba damu waliyoimwaga si ya Watanzania.

Tunaambiwa katika kutetea kiti chake Rais aliidhinisha ubakaji, ulawiti wa watoto wetu na zaidi mauaji. Mwenyewe kasema "nguvu iliyotumika" inaendana na tishio lililokuwepo. Ati wangetumia nguvu kidogo wangeondolewa kwa mapinduzi (msisahau chama kinaitwa ni 'cha mapinduzi'). Kama walivyofanya kabla ya Oktoba 29 walitoa vitisho na mikwara ya nguvu na kweli kabisa wakaenda kutekeleza walichokipanga kiwe funzo kwa yeyote atakayewapinga.

Miili tuliyoiona imezagaa, picha za video na za kuganda tulizoziona za watu waliouawa kinyama na kuachwa hadharani kama vibudu vyote hivyo ni makosa ya Mange, Maria Sarungi, na wanaharakati. Kwamba, watu walioko Tanzania wanatakiwa kupiga makofi kila wakubwa hawa wanapopita, walioko Tanzania hawatakiwi kusema siyo kwa jina letu. Walioko Tanzania tunaambiwa ni lazima wakubaliwa kutawaliwa bila kujali wanavyotawaliwa. Mauaji ya Oktoba 29 ilikuwa ni "fanya fyoko ukione"; watawala wetu hawa walioshindwa wanarudia tena - 'fanyeni fyoko muone kama hatutawachinjilia mbali".

Wanatukumbusha vikundi visivyo vya serikali kama kule Sudan na sehemu nyingine ambavyo vilishiriki mauaji ya wananchi wao kwa jina la kuitetea serikali. Tunawasikia wengine wanajitokeza na kupiga mikwara kuwa wako tayari kuitetea serikali; hawa wanaweza kupewa silaha, za moto na za jadi kuingia mitaani kuua. Kama ilivyotokea Oktoba 29 hawa wauaji wa serikali hawahitaji kujitambulisha; vitambulisho vyao ni bunduki, alama zao ni bastola!

Ni kweli wataua tena; wameonja damu na wameongezeka hamu! Wanajua sasa hivi hawawezi kutawala tena kwa hoja; isipokuwa hoja za risasi na visasi! Zamani waliposhindwa hoja walikuwa wanaleta vihoja; sasa wameshindwa hoja kwa kasi sasa wanaleta risasi na visasi. Tunawathubutisha tena! Ueni tena wananchi wetu; jitangazeni mipango yenu, semeni kuwa mnaenda kuua tena kama mlivyofanya hadi Watanzania wote wasalimu amri!

Hawa wamenza kufanana na utawala ule dhalimu tuliowahi kuuona katika bara letu la Afrika; wamefanana kila kitu isipokuwa rangi tu. Watawala hawa wanataka kutawala kwa kuua; na niwe wa kwanza kutabiri baada ya mauaji yaliyopita na haya yajayo; Samia hatoweza kutoka madarakani; na hatoachwa atoke madarakani na watu wanaomtegemea kuwalinda. Sasa hivi naamini kuna uwezekano wa asilimia 99 watakapopendekeza Katiba Mpya wataondoa ukomo wa madaraka (term limits) ili Samia aendelee baada ya 2030. Atoke achekwe?

Lakini vyovyote vile ilivyo, kuelekea Disemba 9 wao ndio wanauamuzi wa kufanya; watoke waue tena mamia wengine au watafute hekima ya jinsi gani kudifuse the situation. Lakini kwa vile wameshajawa na roho ya ubabe na kuwa wanataka kulinda "dola" aka familia na maslahi yao uwezekano wa wao kurudi nyuma ni sifuri. Kweli hawa wanaweza kuua tena; lakini wajue kuwa wao wameshajifunza kuua na Watanzania wamejifunza kufa kwa ajili ya nchi yao.

Ila waue tena; ili waharakishe mwisho wao. Imebidi nifunge safari ya ghafla kuja kufuatilia ya mambo ya Disemba 9; tunakusanya ushahidi vizuri zaidi sasa kuliko ile Oktoba 29. We double dare them.. do it again. Please.
D9 ni ngumu kufanikiwa ktokana na BAD TIMING pamoja na kuvaliwa njuga na Maria Sarungi, ambae ni COMMERCIAL ACTIVIST.

Yeye huwa akipewa FUNGU huwa hana Muda wa kufanya TATHMINI ni mbele kwa mbele
 
Naam

Nadhani unafahamu kitakachokwenda kutokea kwahiyo ilikuwa ni busara kuja na njia mbadala ya kusuluhisha haya mambo ili yaweze kuisha

Kutunishiana misuli kwa kuwaweka chambo watoto wa masikini mnakosea sana na hakika mtakuja kulipa hili

Kifo hakijawahi kuwa suluhisho la tatizo lolote watu tunaoshindana nao hatuwawezi kwa namna yoyote

Kila mwananchi anaelewa system ya Government ilivyo so haina haja ya kila dakika kuanzisha mathread ya kuchochea maaandamano

Hii inaonesha kwamba kuna watu ni wanufaika wakubwa wa haya maandamano, kuna watu ndo wanapopatia ugali wao that's why hawataki option nyingine yoyote zaidi ya hii waliyoichagua

Watanzania inatakiwa tuamke sio kila jambo ni la kubeba tu kama matahira tunashindwa hadi na kunguru ambaye akiona umeshika manati atakimbia eneo hilo kwa sababu anajua madhara yake

Kumshawishi raia masikini aende barabarani akiwa hana silaha yoyote ya moto huku mkijua kabisa atakachoenda kukutana nacho ni dhambi moja kubwa sana na hakika mtaenda kuchomwa motoni

Hao kina Hilda na Maria Sarungi wanashindwa nini kutoka Kenya huko kuja kuungana na wenzao huku kupamabania nchi yao.Wao ndo wanajiita mashujaa wa keyboard na kuna nyumbu za Tanzania zinaingia kweli barabarani aisee

Boniface Mwangi mwanaharakati maarufu Kenya kipindi cha maandamano ya Gen Z wa Kenya wala yeye hakuhamasisha akiwa Uganda au Tanzania bali alikuwa palepale Kenya na siku ya maandamano alikuwa front vile ndo inatakiwa

Kuna yule Aunt Lulu kabla ya kukengeuka alishawahi kukiri kuwa analipwa Milioni mbili kwa mwezi na Sativa kwa ajili ya kupost harakati tu hii inaonesha kuna pesa wanapata kupitia hayo mambo

Tunaizika nchi yetu kwa mikono yetu wenyewe
Suluhisho gani la maana na la kudumu litapatikana kwa kumtishia yule ambae unataka msuluhishwe nae?

Badala ya kuwalaumu wanaotaka kudai haki yao bila silaha mikononi ulipaswa kuwalaumu wale wenye silaha ambao wako tayari kuzitumia ili wasisikie madai na vilio vya wale ambao kodi zao ndio zimenunua hizo silaha.

Watapungukiwa nini wakiwaachia waandamane bila kuwadhuru? Si ndio watasikia vizuri machungu yao na masikitiko yao?

Inatakiwa tukubali kuwa wenye nchi wana haki ya kusikilizwa na kuheshimiwa. Kuwabeza na kuwatisha hakuwatendei haki.

Amandla...
 
Back
Top Bottom