We are the other people

mwananthropolojia ,unashangaza sana
'
Unahusishaje mambo mawili yasiyohusiana?
'
Nimekueleza kwa uwazi kuhusu tatizo lako la kubagua maandiko,huelewi
'
If you believe that there is a "contradiction" in the bible,you put whole bible in jeopard
'
Maneno ya Yesu kutokuhubiri injili kwa mataifa,halafu mwishoni kuwaagiza waende ulimwenguni ni kujikinza kwa mujibu wako,sasa unawezaje kuniambia kuwa hakuna kujikinza kwingine kwenye biblia?
'
Utakua na kazi kubwa sana kututhibitishia ni maandiko yapi ni sahihi na yapi sio sahihi na itabidi utuambie umetumia kipimo gani kuyabagua maandiko hayo
'
Halafu ni wapi nimesema Yesu amehubiri injili kwa mataifa?Acha kusema uongo
'
Nakushauri Either uikatae biblia yote au uikubali yote
'
Kama utaendelea na mtindo huu mjadala huu utakua mgumu sana
'
Utakua mgumu kwa kuwa ninapokupa ushahidi unasema ni fabrication,sasa tutafika kweli?

ok we unaonaje tukubali biblia nzima ni kweli hata kama tunaona contradictions au tuikatae kutokana na mambo yanayokinzana ndani ya kitabu na kutuchanganya?

huku tukijarib kwa nguvu zote kutafuta kamstari kamoja kamoja ili kujiridhisha kwamba na sisi wa mataifa, Mungu wa Israel hajatusahau

maana najaribu kutafuta nabii au mtume asiye mwisrael kwenye kitabu hata la agano jipya na bado sijampata ,sasa najiuliza hivi Mungu wa Israel ni wetu kweli? au tuwathibitishe akina mwingira kama manabii ili turidhishe nafsi zetu?
 
ok we unaonaje tukubali biblia nzima ni kweli hata kama tunaona contradictions au tuikatae kutokana na mambo yanayokinzana ndani ya kitabu na kutuchanganya?

huku tukijarib kwa nguvu zote kutafuta kamstari kamoja kamoja ili kujiridhisha kwamba na sisi wa mataifa, Mungu wa Israel hajatusahau

maana najaribu kutafuta nabii au mtume asiye mwisrael kwenye kitabu hata la agano jipya na bado sijampata ,sasa najiuliza hivi Mungu wa Israel ni wetu kweli? au tuwathibitishe akina mwingira kama manabii ili turidhishe nafsi zetu?



ahahahahahaaaaaaaaaaaaaaaaa_nimeipenda sana hiyo ya kusema hatuna nabii yeyote wa mataifa zaidi ya kina mwingira and allies,......huu ni msumari wa moto....kwetu sisi waamini wa hizi dini za mapokeo.
 
mwananthropolojia ,
Inaonekana nazungumza lugha ngumu sana,jambo ambalo hunielewi
'
Ni kwamba,wewe unadai Yesu hakuja kwaajili ya ulimwengu bali kwa Waisraeli tu
'
Fahamu kuwa Yesu anapatikana kwenye Biblia TU,hakuna kitabu kingine kinachomzungumzia mtu aitwae Yesu,hivyo nilazima pale tutakapokua tunajadili kama ni kweli Yesu alikuja kwa Waisraeli au duniani ni lazima tuitumie Biblia kama back up
'
Kama tunakubaliana hilo ni lazima tukubaliane kwanza kama hiyo Biblia ni sahihi
'
Hili hatujakubaliana na inaonekana wewe una mashaka nayo
'
Kwa mujibu wa Biblia yenyewe,aliezungumza toka Mwanzo mpaka Ufunuo ni Mungu yuleyule,hii inamaana kama hukubaliani na sehemu moja tayari umemtilia mashaka Mungu wa kwenye Biblia na Biblia yenyewe
'
Kama umeitilia mashaka Biblia hata huyo Yesu unaetaka tumjadili anakua na mashaka na hata uwepo wake unauweka mashakani
'
Unakua mashakani kwa kuwa,kama watu wameweza kuifabricate baadhi ya sehemu wameshindwaje kuedit Biblia nzima?
'
Je huyo Yesu sio wa kutunga?Maana hakuna mahali anapatikana tofauti na kwenye biblia
'
Kwanini hiyo mistari unayodai inasema Yesu ni kwaajili ya Israeli tu isiwe ya fake?
'
Au huyo Yesu wako sio wa kwenye Biblia?
'
Hizo quote zako kutoka kwenye Biblia sio "vimistari"
'
Kama unaonadhani Biblia ina contradictios,haifai kutumiwa na yeyote kati yetu mimi na wewe kama back up kwa sababu tayari umeonesha mashaka na ushahidi wako mwenyewe
'
Ndugu yangu unajicontradict!
 
Last edited by a moderator:
mwananthropolojia ,
Inaonekana nazungumza lugha ngumu sana,jambo ambalo hunielewi
'
Ni kwamba,wewe unadai Yesu hakuja kwaajili ya ulimwengu bali kwa Waisraeli tu
'
Fahamu kuwa Yesu anapatikana kwenye Biblia TU,hakuna kitabu kingine kinachomzungumzia mtu aitwae Yesu,hivyo nilazima pale tutakapokua tunajadili kama ni kweli Yesu alikuja kwa Waisraeli au duniani ni lazima tuitumie Biblia kama back up
'
Kama tunakubaliana hilo ni lazima tukubaliane kwanza kama hiyo Biblia ni sahihi
'
Hili hatujakubaliana na inaonekana wewe una mashaka nayo
'
Kwa mujibu wa Biblia yenyewe,aliezungumza toka Mwanzo mpaka Ufunuo ni Mungu yuleyule,hii inamaana kama hukubaliani na sehemu moja tayari umemtilia mashaka Mungu wa kwenye Biblia na Biblia yenyewe
'
Kama umeitilia mashaka Biblia hata huyo Yesu unaetaka tumjadili anakua na mashaka na hata uwepo wake unauweka mashakani
'
Unakua mashakani kwa kuwa,kama watu wameweza kuifabricate baadhi ya sehemu wameshindwaje kuedit Biblia nzima?
'
Je huyo Yesu sio wa kutunga?Maana hakuna mahali anapatikana tofauti na kwenye biblia
'
Kwanini hiyo mistari unayodai inasema Yesu ni kwaajili ya Israeli tu isiwe ya fake?
'
Au huyo Yesu wako sio wa kwenye Biblia?
'
Hizo quote zako kutoka kwenye Biblia sio "vimistari"
'
Kama unaonadhani Biblia ina contradictios,haifai kutumiwa na yeyote kati yetu mimi na wewe kama back up kwa sababu tayari umeonesha mashaka na ushahidi wako mwenyewe
'
Ndugu yangu unajicontradict!

Eiyer kwanza unaposema ni kitabu kimoja tu kinachomzungumzia yesu unakua unakosea kwani kuna vitabu vingi tu vilivyoandikwa kipindi hicho sambamba na injili,ngoja nikutajie, kuna kitabu kinaitwa nag hammadi library,diatessaroni by Tatiani,apostolic fathers na Antiquities of the jews by Josephus ambao wote wanathibitisha kwamba yesu aliexist na siku ya kutundikwa msalabani inathibitishwa kwamba aliwekewa bango linalosema mfalme wa wayahudi haikusema kwamba ni mfalme wa ulimwengu.

hizo stori za ufufuo na kuwaambia wanafunzi wake waende kwa mataifa zinapatikana kwenye biblia tu maana hata quran inakataa hakufufuka bali ulikua uvumi tu,ila uthibitisho wa kwamba yesu alipata kuishi upo na ni mwingi mpaka kwenye rekodi za warumi zipo kwamba walimtundika yesu kristo mfalme wa wayahudi

na ukivisoma hivyo vitabu utagundua hawaelezei kwamba alikuja kuiokoa dunia bali inaelezea harakati zake za kujaribu kuikomboa israel kutoka kwenye makucha ya mkoloni wa wakati huo roman empire na vitabu vingine vinaongelea mambo ya imani ila hakuna nasisitiza palipoisema alikuja kwajili ya kuuokoa ulimwengu

halaf mi sipati tabu kuquote mistari kwa sababu zimejaa kuanzia mwanzo mpaka ufunuo. wanaelezea kuhusu mungu wa israel na kwamba kazi yake kubwa aliyokua akifanya ni kuwaokoa,kuwalinda,saa nyingine kuwaadhibu waisrael na unabii wake wote ni kuhusu watu wake wa israel .

so kwangu haina tabu,yani zimejaa kitabu kizima ni wewe ndugu yangu unayehangaika kutafta mistari michache ili kuweza kuiridhisha nafsi yako kwamba yesu alikuja kwajili yetu na mungu wa israel nae ni mungu wetu,wakati huyo mungu anapigana vita na mataifa mengine na anawakataza waisrael wasiabudu miungu mingine,kwa maana anajua kuna miungu mingine wa mataifa soma biblia yako utaona vita vyake na miungu wengine
 
Hapa kuna kazi kubwa,tena sana
'
mwananthropolojia,hapa namzungumzia Yesu Kristo ambae atauhukumu ULIMWENGU HUU
'
Yesu aliekuja kuupa ulimwengu UZIMA hapatikani mahali popote tofauti na kwenye biblia
'
Kwenye Quran hakuna Yesu kuna Isa,Isa siyo Yesu,ambae hakufa ni Isa
'
Wayahudi na Warumi hawakumkubali Yesu hivyo hata walichokiandika kumhusu hakiwezi kuaminiwa
'
Again kama unakubaliana na Biblia pale unapodhani inakuunga mkono unachodai na kudai imeghushiwa pale inapokana madai yako huo ni wehu,siwezi kuendelea na mjadala huu,nawaachia wengine watakaokubaliana nawe
'
Sasa nitabaki kuwa mtazamaji tu!
 
Last edited by a moderator:
Eiyer naona umechanganyikiwa kwani nimekupa vitabu vinavyosimulia kuhusu yesu,umebaki kuukana ukweli ingawa

naona una streess sana sahiz baada ya kuugundua ukweli,ni mambo ya kawaida ila utaamua mwenyewe uambatane na ukweli au ubaki kwenye uongo na dunia isiyokuhusu ukitegemea kwenda mbinguni sijui au kwenda kukaa nje ya hekalu la bwana kwenye behewa maana wewe sio myahudi ufunuo 11;2
 
Eiyer naona umechanganyikiwa kwani nimekupa vitabu vinavyosimulia kuhusu yesu,umebaki kuukana ukweli ingawa

naona una streess sana sahiz baada ya kuugundua ukweli,ni mambo ya kawaida ila utaamua mwenyewe uambatane na ukweli au ubaki kwenye uongo na dunia isiyokuhusu ukitegemea kwenda mbinguni sijui au kwenda kukaa nje ya hekalu la bwana kwenye behewa maana wewe sio myahudi ufunuo 11;2

Ni kama story ya Plato ya Allegory of the Cave, ukweli mchungu kuumeza, wapo wanaoona bora kuendelea na mapokeo hata kama wanamashaka nayo, kwa sababu ukweli unauma, ukweli unawatoa out of their comfort zone.

Sasa siku akija kujua kuwa hata hiyo the so called "the holy book" jamaa waliichakachua, sijui atapatwa na wazimu au ataendela kubishana na ukweli?

"Ukiijua kweli, nayo kweli itakuweka huru"
 
Ni kama story ya Plato ya Allegory of the Cave, ukweli mchungu kuumeza, wapo wanaoona bora kuendelea na mapokeo hata kama wanamashaka nayo, kwa sababu ukweli unauma, ukweli unawatoa out of their comfort zone.

Sasa siku akija kujua kuwa hata hiyo the so called "the holy book" jamaa waliichakachua, sijui atapatwa na wazimu au ataendela kubishana na ukweli?

"Ukiijua kweli, nayo kweli itakuweka huru"
Nimefutilia mabishano yenu,ni mazur maana wote mnapointi tena za msingi,ila muelewane kisha nasi tuanze kuchangiaaana zumekaa pembeni baada ya kuona mnabishana
 
Nimefutilia mabishano yenu,ni mazur maana wote mnapointi tena za msingi,ila muelewane kisha nasi tuanze kuchangiaaana zumekaa pembeni baada ya kuona mnabishana

Mkuu sidhani kama unahitaji mwaliko kuchangia hapa, weka vitu Mkuu!
 
kuwa binadamu
tunajua kuna pia kufanya makosa. lakini tuangalie nafasi zao katika
jamii! kama hao walikuwa watu wa mungu kweli, basi walikua wanaongozwa
na roho mtakatifu,na maamuzi yoyote yalikua yasifanyike bila kumconsult
roho mtakatifu.na kama walikua wakimconsult roho mtakatifu haiwezekani
wakakosea kwenye kutoa maagizo ya kiroho unless otherwise roho mtakatifu
hakua nao kwaiyo walikua wakifanya maamuzi bila kumconsult roho
mtakatifu.hii kupingana na kutoa maamuzi tofauti yaonyesha kabisa
walikua wakiongozwa na utashi wao na si wa Mungu

suala la Mungu kutugeuka si kweli! ni kama nilivyosema wanaisrael wana
Mungu wao na sisi pia tuna Mungu wetu,na Mungu wa Israel hajishughulishi
na sisi,akijishughulisha na sisi, lengo litakua kututawala na kuwafanya
watu wake waisrael wawe juu ya watu wengine wote.nadhani unafaham vita
walivyozipiga na miungu na jamii zingine ili kuweza kutwaa maeneo na
kuwatumikisha

maandiko ya biblia yana mafundisho mengi,kwetu inaweza kutumiwa kama
reference book kati ya vitabu vingi,ila usife moyo kwani na sisi tuna
Mungu wetu ambae nae anatenda miujiza na anasikiliza matatizo
yetu.jaribu kuzunguka maeneo mbalimbali ya Tz kuna maeneo ya maombi na
watu wanaenda wanatatuliwa matatizo yao bila kupitia kwa Mungu waisrael.
tofauti kati yetu na wao ni kwamba sisi hatujawahi andika vitabu kuhusu
Mungu wetu ila yupo hai

Mungu wetu ni nani?
 
Ni kama story ya Plato ya Allegory of the Cave, ukweli mchungu kuumeza, wapo wanaoona bora kuendelea na mapokeo hata kama wanamashaka nayo, kwa sababu ukweli unauma, ukweli unawatoa out of their comfort zone.

Sasa siku akija kujua kuwa hata hiyo the so called "the holy book" jamaa waliichakachua, sijui atapatwa na wazimu au ataendela kubishana na ukweli?

"Ukiijua kweli, nayo kweli itakuweka huru"

Huwa nawaambia watu kuwa hakuna jehanam wala ziwa la moto lakini hawanieleweli. Yesu mwenyewe aliona jinsi watu walivyo na mashaka na kutaka kulinda mapokeo yao bila kuyatafakari kwa uhuru na bila kutaka kusikia mtizamo tofauti na wa kwao. Mwishowe akawaambia kuna siku wataijua kweli na hiyo kweli itawaweka huru.

Jambo moja dhahiri ni kwamba dunia inabadilika na viumbe waliopo nao wanabadilika, fikra na mitazamo itabadilika, maarifa yataongezeka, uthubutu hata wa kuhoji mungu ni nani utakuwepo. Asiyetaka kutoka kwenye 'comfort zone' ataachwa. Imani zinaongezeka kila uchao, makanisa yanagawanyika kwa kasi, nyimbo zilizoimbwa makanisani tu sasa hivi zinashindanishwa kwenye majukwaa ya starehe. Bado mengi yanakuja na ajidhaniaye amesimama na aangalie asianguke.

Fikra mbadala siyo dhambi. Kadhalika imani tofauti siyo dhambi.
 
Thank you so much. You have made me read the book of Genesis again, and the first post on this thread sounds amazingly true. It continues to prove that there's God, and humans are spiritually connected to God, their keeper. I have enjoyed the discussion too, it's very enticing. I wish someone could help bring forth the connection between "the other people" and God, I believe there's a connection, they just can't be "godless"! Asante sana mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom