Maji ya dafu hayapikiwi chai!
Hee!
Ulikuwa unataka kutufikishia ujumbe gani ati?
Nilivyomuelewa mimi ni kwamba,
Mkishavunja dafu....
Kwani wewe ukimaliza kuvunja dafu huwa unafanyaje?
Ni swali gumu kwa kuwa sijawahi kukaa pwani!
Lakini nahisi kinacho baki ni kukinga maji yake na kunywa!
Au sio Madame B?
Hapa naona tunapishana Kiswahili.
Haya wewe unaweza ukakinga na kuyanywa?
Yana ladha gani,au chumvichumvi au ugwadu au matamu?
Kwa hiyo umekubali kuwa maij ya dafu hayapikii chai!
Maji ya dafu hayapikiwi chai!
Nilivyomuelewa mimi ni kwamba,
Mkishavunja dafu....
Kwani wewe ukimaliza kuvunja dafu huwa unafanyaje?
Haswaa! St. Paka Mweusi. Raha ya dafu kwanza likatwe juu juu, kisha kinywewe kwa staili yeyote ile kama kwa mrija sawa kama kwa kunjwa kawaida sawa ila sharti ukimaliza kunywa yake maji ili upate chakula yake sharti ulichokowe!Eh,makubwa haya,siku hizi Dafu huvunjwa...??Mi najua dafu hukatwa kisha huchokolewa..